Shahidi wa nane kesi ya Sabaya: Mume wangu hakupigwa wala kunyang'anywa simu

Dr Restart

JF-Expert Member
Jul 15, 2021
3,132
16,357
Katika muendelezo wa kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili, Shahidi wa nane wa Jamhuri dhidi ya Sabaya ameieleza mahakama kuwa hakumshuhudia mumewe akipigwa kama alivyoeleza. Pia, ameeleza bayana kuwa simu zake hazikuchukuliwa kwa sababu mumewe alipofika alitoa simu alipokuwa amezificha Sehemu zake za siri.

Hii ni baada ya siku chache zilizopita Bakari Msangi kuieleza mahakama kuwa alipigwa karibia kufa kisha kufungwa pingu miguuni.

Kesi hiyo inaendelea kunguruma katika mahakama ya hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha chini ya Hakimu Mfawidhi Odira Omworo.

Hali hii imeleta mkanganyiko baada ya Shahidi huyo kwenda kinyume na ushahidi alioutoa mumewe.

Kesi imefikia pazuri.

-----
Shahidi wa nane wa Jamhuri katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya na wenzake amesema hajawahi kumuona Sabaya akiwa anampiga Mume wake Bakari Msangi.

Mbele ya Hakimu Mfawidhi Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, Odira Amworo akiulizwa maswali na wakili wa utetezi Dankan Oola, Shahidi huyo amesema kwa wakati wowote hakushuhudia Sabaya akimpiga Mumewe Bakari Msangi.

Amesema wakati Bakari anampigia simu waliongea na kumuambia ametekwa na baadaye aliposhuka kwenye gari ya Sabaya alikuwa wala hajafungwa pingu mguuni.

Shahidi huyu ameendelea kusema Mume wake hakuibiwa simu na aliporudi nyumbani alikuwa na simu zake zote na alimpa baada ya kuzitoa kwenye sehemu za siri.
 
yaani wewe umetotolewa jana tu na mamako leo hii unakurupuka eti umeanza kutembea kabla kutambaa na kusimama we ni kituko cha mwaka
Kheri yangu niliyetotolewa baada ya kupitia hatua zote muhimu kuliko wewe ambaye umezaliwa kabla ya wakati na akili imeenda kushoto.
 
Ulikuwa mahakamani wewe au unabwabwaja kama kibogoyo?

Basi toa taarifa iliyo sahihi ili kuthibitisha kama napotosha. Vinginevyo, funga bakuli lako.
Kuna kipindi mtu unaweza kukufuru bila sababu yaani. Ewe Mwenyezi Mungu kwanini unaruhusu nakutana na watu kama hawa kwa baadhi ya siku? Kweli Mungu hukuweza kuniepusha na kujibishana na mtu kama huyu? Anyway, kazi yako haina makosa baba, utakalo litimie! Nitalipokea 🙏
 
Unapotosha habari ili upate nini?
Chadema ni mpango wa shetani


USSR
Screenshot_20210810-121808.jpg
 
Member since July 15 2021!!
Endelea kutumika kama "tp".
Yaani basi watu wenye akili finyu uwezo wao wa kufikiri ni mdogo mno.

Kwani kuwa na umri mrefu au mfupi kuna athari gani na mawazo ya mtu? Au mnaona ninyi mliowahi ndiyo mmeyapatia sana maisha?
 

Shahidi Aeleza Alivyotishiwa Bastola na Sabaya​

August 9, 2021 by Global Publishers

sabaya-2.jpg


SHAHIDI wa nane wa Jamuhuri katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili, Magdalena Mallya(32) leo ameieleza Mahakama kuwa alitishiwa kwa bastola na Sabaya alipomfuata kumuomba amuachie mume wake Bakari Msangi aliyekuwa amemteka.



Akihojiwa na jopo la mawakili sita wa utetezi Mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Odira Amworo shahidi huyo amesema pia baada ya Msangi ambaye ni Diwani wa CCM kata ya Sombetini baada ya kuachiwa alikuwa na damu masikioni kutokana na kipigo.



Amesema wakati akiwa ametekwa Msangi alikuwa amefungwa pingu na kamba miguuni na alipofika hoteli ya Tulia, Sabaya aliruhusu wazungumze akiwa chini ya ulinzi. Akihojiwa na wakili Edmund Ngemela shahidi huyo amesema baada ya kutishiwa kwa bastola na kutukanwa aliripoti polisi.



Sehemu ya mahojiano ilikuwa hivi.

Wakili
: Unasema Sabaya alikutisha na bastola mdomoni.
Shahidi: Ndio.
Wakili: Pia alikutukana.
Shahidi: Ndio.



Wakili: Je, ni makosa alifanya.
Shahidi: Ndio.



Wakili: Je uliripoti polisi.
Shahidi: Ndio.
Wakili: Unafahamu hilo sio shitaka lilipo hapa mahakakamani.
Shahidi: Sifahamu.

Wakili: Ulipotoa maelezo hapa mahakamani ulikiwa unaelezea shitaka la kutishwa
Shahidi: Ndio
Wakili: Utajisikiaje ukiambiwa hilo shitaka halipo mahakamani.
Shahidi: Nitajisikia vibaya.
 
Watu wanapotosha. Yeye alivyomuona mume wake alikuwa tayari keshapigwa na kunyang'anywa simu. Angemuonaje? Alipokutana na mume wake tayari alikuwa keshafanyiwa hivyo vitu. Mawakili wanajaribu kupindisha ukweli kwa kuuliza maswali ya kuchanganya shahidi.
 
Huna 'mandate' yeyote ya kunipangia cha kuandika as long as sivunji sheria za JF.

Nitaendelea kuandika chochote nitakachojisikia.

Una haki zote za kuandika hapa jukwaani, ila hukuwa na ulazima wa kujiunga hapa jukwaani mwezi uliopita ili uje uandike huu utoto humu. Huu utoto ungeweza kuufanyia huko huko kwenye shule yenu ya msingi.
 
Katika muendelezo wa kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili, Shahidi wa nane wa Jamhuri dhidi ya Sabaya ameieleza mahakama kuwa hakumshuhudia mumewe akipigwa kama alivyoeleza...

Mimi naona kama vile kuna watu wanajaribu kulipiza kisasi kwa kutumia mahakama zetu. That’s wrong!
 
Sio jambo la kushangaza kwa huyo shahidi kutoa ushahidi wa aina hiyo.
Ikumbukwe ushahidi ni muunganiko wa facts nyingi, sasa ktk kesi kama hii nadhan lengo la kumwita shahidi huyu ilikua sio kuthibitisha kuona mlalamikaji akitendewa uhalifu. Ila ushahidi muhimu kutoka kwa shahidi kama huyu ni kuthibitisha tu mazingira ya utendekaji wa uhalifu.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom