Anaandika Godbless J Lema
TAARIFA ZA UONGO NA MATESO NA MAUAJI YA RAIA.
Mwaka 2011, jijini Arusha, kulitokea sakata zito la mauaji yaliyosababishwa na Polisi kufuatia maandamano ya wananchi waliopinga uchaguzi Meya feki wa Arusha Mjini. Tukio hilo liliacha majeraha makubwa katika mioyo ya wananchi na maswali mazito kuhusu matumizi ya nguvu za dola dhidi ya raia wasio na hatia.
Katika mazingira hayo, Waziri Mkuu wa wakati huo, Mizengo Pinda, aliwasilisha taarifa Bungeni ambayo haikuwakilisha ukweli kamili wa kilichotokea Arusha. Nilihisi dhamira yangu ya uongozi na uwakilishi wa wananchi inanitaka nisikae kimya. Nilisimama hadharani na kusema wazi kuwa taarifa hiyo ilikuwa ya uongo.
Nilimwambia Waziri Mkuu kuwa alidanganya Bunge, na kwamba uongo aliousema angeweza hata kumfundisha shetani mbinu za uongo. Nilisisitiza kuwa nilikuwa na ushahidi wa kuthibitisha nilichokisema. Spika wa Bunge, alinipa siku saba kuwasilisha ushahidi huo, la sivyo ningechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge.
Nilimjibu Spika kuwa sikuhitaji siku saba. Nilihitaji muda mfupi tu kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, kwenda hotelini na kuleta ushahidi mara moja. Ilikuwa hali ngumu na yenye mvutano mkubwa wa kisiasa, lakini nilikuwa tayari kubeba gharama ya kusimama upande wa ukweli.
Baada ya Bunge kuahirishwa mchana, Waziri Mkuu alituma wasaidizi wake wanitafute, akitaka nionane naye ofisini kwake. Niliitikia wito huo. Tulipobaki wawili, aliniambia kwa sauti ya utulivu lakini yenye uzito, “ Lema, umeniita muongo hadharani kwa sauti kali sana. Unadhani uongo wangu ulikuwa upi? Tafadhali nieleze.”
Nilimweleza kwa kina kila nilichokijua kuhusu sakata la Arusha, alisikiliza kwa makini, akashika kichwa kwa mshangao, kisha akasema kwa unyenyekevu mkubwa
“Sasa nimekuelewa. Hatuhitaji kuendelea kulumbana ndani ya Bunge. Wewe potezea, nami nitamjulisha Spika asikufuatilie suala la ushahidi. Nitakuja Arusha kushughulikia jambo hili kwa kina zaidi. Kisha akatoa kauli ambayo hadi leo naona ina uzito mkubwa kwa mustakabali wa nchi yetu:
Lema, alisema , tatizo letu kubwa sasa liko kwenye recruitment ya vijana wanaoingia kwenye vyombo vya usalama. Kazi ya intelijensia ni kusema ukweli ulivyo, ili viongozi wapate mwelekeo sahihi wa kutawala. Kwa sasa tuna changamoto kubwa ya aina ya watu tunaowaajiri. Kuna kazi kubwa sana ya kufanya.”
Maneno haya yanaeleza kiini cha tatizo kubwa linalolikabili taifa letu kwa sasa. Watu wengi wameuawa, wameteswa au kupotezwa si kwa sababu walikuwa na hatia, bali kwa sababu ya taarifa za uongo, majungu na uzembe wa kitaaluma ndani ya mifumo ya usalama. Wapo wanaoandika au kuwasilisha taarifa nzito na uongo za kiintelijensia bila uchunguzi wa kina, wakati mwingine katika mazingira yasiyoheshimu hata thamani ya uhai wa binadamu.
Mwaka 2020, nilipokuwa natoroka nchini, nilikamatwa nchini Kenya. Niliwasikia baadhi ya maafisa wa vikosi maalum Kenya, wakisema kuwa mimi na wenzangu tulikuwa tunapanga kupindua nchi. Mke wangu Neema
alisikia maneno haya ya uongo ktk masikio yake, kwa huzuni na hofu, aliniuliza !
“Godbless, ni kweli ulikuwa unataka kupindua nchi?”
Nilimtazama na kumjibu kwa utani “Labda kama nchi hiyo ni wewe, mimi naweza naweza kukupindua pindua wewe tu mpenzi. Huu ni uongo mtupu.” Usiogope uongo huu , tutashinda tena.
Andiko hili si kwa ajili ya kulalamika, bali ni wito wa kutafakari. Taifa lolote linalojengwa juu ya taarifa za uongo hujenga msingi wa damu na machozi. Ukweli, hata unapoumiza, ndiyo pekee unaoweza kuokoa maisha na kulinda heshima ya nchi.
Taarifa za majungu , uongo , umbeya na ulevi zimeumiza watu wengi sana kibiashara, kijamii , makazini na wengine wamefungwa na hata kuuwawa bila hatia yoyote.
TAARIFA ZA UONGO NA MATESO NA MAUAJI YA RAIA.
Mwaka 2011, jijini Arusha, kulitokea sakata zito la mauaji yaliyosababishwa na Polisi kufuatia maandamano ya wananchi waliopinga uchaguzi Meya feki wa Arusha Mjini. Tukio hilo liliacha majeraha makubwa katika mioyo ya wananchi na maswali mazito kuhusu matumizi ya nguvu za dola dhidi ya raia wasio na hatia.
Katika mazingira hayo, Waziri Mkuu wa wakati huo, Mizengo Pinda, aliwasilisha taarifa Bungeni ambayo haikuwakilisha ukweli kamili wa kilichotokea Arusha. Nilihisi dhamira yangu ya uongozi na uwakilishi wa wananchi inanitaka nisikae kimya. Nilisimama hadharani na kusema wazi kuwa taarifa hiyo ilikuwa ya uongo.
Nilimwambia Waziri Mkuu kuwa alidanganya Bunge, na kwamba uongo aliousema angeweza hata kumfundisha shetani mbinu za uongo. Nilisisitiza kuwa nilikuwa na ushahidi wa kuthibitisha nilichokisema. Spika wa Bunge, alinipa siku saba kuwasilisha ushahidi huo, la sivyo ningechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge.
Nilimjibu Spika kuwa sikuhitaji siku saba. Nilihitaji muda mfupi tu kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, kwenda hotelini na kuleta ushahidi mara moja. Ilikuwa hali ngumu na yenye mvutano mkubwa wa kisiasa, lakini nilikuwa tayari kubeba gharama ya kusimama upande wa ukweli.
Baada ya Bunge kuahirishwa mchana, Waziri Mkuu alituma wasaidizi wake wanitafute, akitaka nionane naye ofisini kwake. Niliitikia wito huo. Tulipobaki wawili, aliniambia kwa sauti ya utulivu lakini yenye uzito, “ Lema, umeniita muongo hadharani kwa sauti kali sana. Unadhani uongo wangu ulikuwa upi? Tafadhali nieleze.”
Nilimweleza kwa kina kila nilichokijua kuhusu sakata la Arusha, alisikiliza kwa makini, akashika kichwa kwa mshangao, kisha akasema kwa unyenyekevu mkubwa
“Sasa nimekuelewa. Hatuhitaji kuendelea kulumbana ndani ya Bunge. Wewe potezea, nami nitamjulisha Spika asikufuatilie suala la ushahidi. Nitakuja Arusha kushughulikia jambo hili kwa kina zaidi. Kisha akatoa kauli ambayo hadi leo naona ina uzito mkubwa kwa mustakabali wa nchi yetu:
Lema, alisema , tatizo letu kubwa sasa liko kwenye recruitment ya vijana wanaoingia kwenye vyombo vya usalama. Kazi ya intelijensia ni kusema ukweli ulivyo, ili viongozi wapate mwelekeo sahihi wa kutawala. Kwa sasa tuna changamoto kubwa ya aina ya watu tunaowaajiri. Kuna kazi kubwa sana ya kufanya.”
Maneno haya yanaeleza kiini cha tatizo kubwa linalolikabili taifa letu kwa sasa. Watu wengi wameuawa, wameteswa au kupotezwa si kwa sababu walikuwa na hatia, bali kwa sababu ya taarifa za uongo, majungu na uzembe wa kitaaluma ndani ya mifumo ya usalama. Wapo wanaoandika au kuwasilisha taarifa nzito na uongo za kiintelijensia bila uchunguzi wa kina, wakati mwingine katika mazingira yasiyoheshimu hata thamani ya uhai wa binadamu.
Mwaka 2020, nilipokuwa natoroka nchini, nilikamatwa nchini Kenya. Niliwasikia baadhi ya maafisa wa vikosi maalum Kenya, wakisema kuwa mimi na wenzangu tulikuwa tunapanga kupindua nchi. Mke wangu Neema
alisikia maneno haya ya uongo ktk masikio yake, kwa huzuni na hofu, aliniuliza !
“Godbless, ni kweli ulikuwa unataka kupindua nchi?”
Nilimtazama na kumjibu kwa utani “Labda kama nchi hiyo ni wewe, mimi naweza naweza kukupindua pindua wewe tu mpenzi. Huu ni uongo mtupu.” Usiogope uongo huu , tutashinda tena.
Andiko hili si kwa ajili ya kulalamika, bali ni wito wa kutafakari. Taifa lolote linalojengwa juu ya taarifa za uongo hujenga msingi wa damu na machozi. Ukweli, hata unapoumiza, ndiyo pekee unaoweza kuokoa maisha na kulinda heshima ya nchi.
Taarifa za majungu , uongo , umbeya na ulevi zimeumiza watu wengi sana kibiashara, kijamii , makazini na wengine wamefungwa na hata kuuwawa bila hatia yoyote.