Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Status
Not open for further replies.
Tatizo lako hutaki kuelewa! Kwahiyo unataka kusema efficiency ya bandari ya Dar ikifikia 100% ndo cargo storage haitakuwa tatizo?

Narudia, Bandari ya Dar hata ikiongeza efficiency kwa 100000000000% not mentioning hiyo 100%, watakachofanikiwa ni improvement ya logistics. Kwamba, meli ikifunga nanga, mzigo utapakuliwa na kuwa cleared on time na kwa outward cargo, nayo itakuwa hivyo hivyo! Kwamba, kazi waliyokuwa wanafanya kwa siku 5, kukiwa na efficiency itafanyika kwa dakika 5!!

Hoja hapa ni kwamba bandari ya Dar es salaam haina uwezo wa ku-handle mzigo mkubwa. Kwamba, sawa una supersonic efficiency; inward na outward cargo imeongezeka; sasa na hiyo supersonic efficiency yako itakusaidia nini wakati hauna facilities za kutosha za kuhifadhi mzigo? Ingawaje kuna ICD za watu binafsi, lakini mzigo unapofika mteja ana haki ya kuhifadhiwa mzigo wake kwa siku 7 bila kulipa chochote... kwahiyo, hata kukiwa na ICDs za watu binagsi kila mtaa, bado bandari wana wajibu wa kuhifadhi mzigo wa mteja at least kwa siku 7... kama ndani ya hizo cku 7 itabidi kupelekwa privately owned ICDs, basi wapeleke wenyewe bandari kwa gharama zao!!
Hii yote ni kwa sababu kule bandarini hakuna maghala ya kutosha ya kuhifadhia mizigo! Kwahiyo, efficiency ita-speed up logistics lakini tatizo la msingi litabaki pale pale!

Bandari ya Tanga, nimewahi kupita pale siku moja... sina hakika kama nilichokuwa nimekiona ndicho kilichopo au ile siku maji yalikupwa! Kwa macho yangu nilishuhudia tishari zinatoa mzigo melini na kuleta gatini! Kama hivyo ndo hali yenyewe, basi maanake ni kwamba kuna shallow water.... kama kuna mtu wa Tanga humu anisaidie. But all in all, hivi pale Tanga kuna bandari ya kuboresha pale kama sio kujenga upya!!

Kwamba Kenya kutaka kujenga bandari nyingine haimanishi ndo wapo sawa... hebu jiulize kidogo! Kenya ina raslimali watu na raslimali fedha! Imetumia raslimali zote mbili kufanya feasibility study na wakaona umuhimu wa kujenga bandari kubwa zaidi kutokana na projections zao!! Yaani bado unaamini wewe usiyefahamu hata wanapokea containers ngapi kwa mwezi unaweza kuwa sawa kuliko wao? Sasa wakati nyie mnadhani ndo wataalamu zaidi wa kuzifahamu white elephant projects, Wakenya na Wamarekani kwa kuwa hawana akili hawa hapa:Kwahiyo hapa Wachina hawana akili, Kenya hawana akili, US Companies nao maboya tu lakini nyinyi tena ambao hata shipping business yenyewe hamuifahamu lakini ndo mna uwezo mkubwa wa kufahamu viable and white elephant project kwenye ports investments!!!! Sasa ikiwa $ 10 Billion mnaona ni li-project likubwa kwelikweli; what abaout hao ambao target yao ni $26 Billion?

Wengine wakati wanelezea strategy za China kujitanua, wanaandika:
China’s strategy is to have key points on the Silk Road space such as Bagamoyo become the key sites for the transcontinental exchange of manufactured goods and commodities between the Asian and African economies along the Maritime Silk Road. Chinese policy-makers are convinced that the benefits of China’s infrastructure-driven development model can also be transferred to Africa. Pamoja na yote hayo, bado mnaona Wachina ni wapumbavu wa kutaka kuwekeza Bagamoyo?!

Tatizo la Watanzania, hata vitu ambavyo hatuna utaalamu navyo tunataka kuvitolea maoni na ku-criticize na tunafanya hivyo bila ku-research wala kuuliza wenye utalaamu na suala husika!!! Yaani unakuta mtu anaibuka from nowhere na kuongea bila woga kwamba pale kina kifupi... muulize kifupi futi ngapi hana jibu... kumbe alikariri Jiografia ya shule ya msingi kwamba Mtwara ndo bandari yenye kina kirefu basi ndo tayari anajiona mtalaamu wa kufahamu wapi panafaa kujengwa bandari na wapi hapafai!!!! Muulize ili kujenga bandari kina kinatakiwa kuwa futi ngapi, hana jibu lakini bado anataka kuwa-criticize watalaamu ambao wameshafanya study!


Mimi nimekwambia siwezi kuongelea mambo ya Kenya kwa maana sina uelewa sana ila kwa hapa kwetu Bandari ya Bagamoyo ni white elephant project yaani kupoteza tu fedha, fedha ambazo tungeweza kuzitumia kuboresha kwanza hizi zilizopo kabla ya kujenga Bandari mpya yaani kwanza Reli ijengwe upya ya kuunganisha Dar na Kigoma/Mwanza; Tanga- Moshi -Arusha mpaka Musoma na Mtwara corridor ambapo reli ya kutoka MT mpaka Ziwa Nyasa hivyo vifanyike kwanza, Maziwa yetu yote yapate Bandari kwanza, tayari zipo ni kukarabati tu kama vile Kigoma, Mwanza, Musoma, Bukoba na Nyasa na kama tukitumia hiyo bilioni 10 tutafanya mengi sana kwenye hilo baada ya hapo sasa baada ya kila kitu kuwa exhausted ndiyo kama kuna haja ya kujenga Bandari nyingine from scratch basi tufanye hivyo lkn siyo kinyume chake, huko ni kupoteza fedha!
 
Last edited:
Labda ni mgeni kidogo. Kuhusu Bandari tumejadili sana wakati mradi huo ukianza

Kama utakumbuka mradi ulikuwa kujibu mradi wa CoW katika EAC.
Tulisema hivi, kuna hatari ya kuchukua maamuzi ya jazba

Ni lazima kwanza ifanyike study ya kuona faida na hasara za muda mrefu na si kuhamaki.

Katika rekodi, nipo nikisema hivi, bandari ya Dar es Slaam inafanya kazi chini ya kiwango.

Tatizo ni ukosefu wa vifaa na mbinu ikiwemo wizi kutamalaki na kodi zisizovutia wasafiri.

Tukaeleza kwanini eneo muhimu kama bandari liendeshwe na makampuni binafsi yasiyowekeza bali kuleta mitambo ya kukusanya mapato?

Nilisema, yale magati yaliyokuwa yajengwe iligundulika ufisadi kwa kutumia kampuni ile ya China. Hilo ni tatizo kubwa

Tuliendelea, kuna mradi wa bandari ya Mwambani Tanga ambayo ina link na reli ya kaskazini na ya kati.

Bado inaweza kutumika kama bandari ya mizigo ya ndani na ile ya Dar es Slaam ikawa kwa mizigo ya mataifa.
Katika maelezo hayo tulishauri ijengwe bandari kavu ambayo kwasasa ipo kahama.

Msongamano katika bandari ya Dar unaweza kupunguzwa ikiwa wafanyabiashara kutoka Rwanda, Burundi, Uganda au Kongo wataweza kuchukua mizigo yao kutoka bandari kavu katika gharama zinazowavutia.

Hivyo hoja kubwa ilikuwa kuimarisha bandari ya Dar /Tanga /Mtwara zifanye kazi kwa asilimia 100 kwasababu tatizo si ukubwa bali ufanisi.

Ukiende Dubai eneo lao si kubwa kihvyo bali efficiency yake ni superb. Mradi wa Bagamoyo tukashauri uangaliwe kwanza

Kuhusu Magufuli, inawezekana alikataa, hata hivyo alitoka nje katika kampeni na kupigia upatu.
Pitia video zilizowekwa hapa usikie mwenyewe akisema.

Sasa inakuwaje leo anasema mradi huo usitishwe? Alikuwemo na akatumia kama kauli mbiu ya kampeni, miezi michache anageuza kibao.

Hapa ndipo tunahoji kulikoni? Tunajua tunapokwenda au tunaunga tela kwasababu tu !!!!

Hivyo katika mradi huu, Magufuli anaujua kutoka katika Cabinet, na alizungumzia katika kampeni.
Kitu gani unachoona kina kosa kuzungumzia hilo. Hatuwezi kumtwisha JK mzigo mzima ikiwa washirika wake wapo.

Kuhusu sababu za kuahirisha na faida zake au la, hilo halina mashiko kwasasa.

Wameamua kusimamisha! period! Hatuwezi kuwageuza maana hakuna mission wala vision.

Tunachotaka nI watu wajifunze kuelewa kuwa matatizo yetu hayatoki nje, ni yale yale ya miaka 50 na wale waliotufikisha hapa ndio wanatengeneza vision inayosemwa mpya! Vision ya flip flop kucheza na muda kwa matokeo sifuri kama mradi huu unavyoonyesha.

Sina tatizo na ulichoandika kwa kiasi kikubwa, shida ni pale unapojenga hoja ya uwepo wa Magufuli kwenye cabinet ya Kikwete katika 'contetx' inayoashiria angeweza kukataa wakati mradi wa Bagamoyo unapitishwa! Nadhani hapa utakuwa unamuonea Magufuli kwa sababu kwanza hatujui kama huo mradi ulijadiliwa kwa kiwango gani kwenye cabinet wakati wa JK, pili, hatujui kama Magufuli alisema ndio au hapana na kama jibu lolote alilotoa (kama alitoa) lilikuwa na nguvu ya kubadili uamuzi wa utawala wa wakati huo, na tatu Bandari ilikuwa chini ya wizara nyingine ambayo Magufuli alikuwa hausiki nayo, unadhani ni wapi Magufuli alikosea?

Baada ya kusema hayo, sasa narudi tena kwenye maelezo yako hapo juu, ni hatua gani sahihi ulitaka RAIS Magufuli achukue dhidi ya Bandari ya Bagamoyo kwa kuzingatia uwepo wa Bandari zingine kama Dar, Tanga etc?

Kwenye red: Kama nimekuelewa vizuri ni kwamba unasema wakati wa Kampeni Magufuli alitumia Bandari ya Bagamoyo kama kauli mbiu ya kampeni. Bado unasimamia hii hoja?

Na pengine ningekuuliza jambo moja (na hii ni kutokana na threads zako nyingi hapa jamvini hasa wakati na baada ya kampeni, 2015) unadhani nani alifaa kuwa rais kati ya Magufuli na Lowassa? Uwe mkweli.
 
Kujengwa banadari mpya na ya kisasa kupisha bandari ya dar ambayo haina nafasi ni uharibifu?

Hakika shule mlienda kusomea ujinga.
Kama walienda kusomea ujinga basi wew ndo uliye kuwa mwalim wao. Maana naona unashindwa kuelewa kuwa ghalama za kuijenga hyo bandari ni kubwa kuzidi hata bajeti yetu ya taifa. $10bill=22Tilion kwa pesa zetu za madafu. Dahh sijui alie propose hii project alidhani wote wanakili za madafuo_O
 
Nadhani wengi hawajapa picha kubwa juu ya hii bandari , hii bandari ni pamoja free zone inakayo kuwa na mabohari na viwanda na vyote hivi vinategemewa kuhudimia zaidi ya nchi 10 na idadi ya watu zaidi ya 200 million, badala ya watu kuenda Dubai na Guanzouw watakuwa chukua bidhaa zao toka Bagamoyo na Tanzania inapata mapato na ajira ! pia bandari itakuwa ni transhipment hub - yaani itakuwa ni kituo ambacho makontena yaendayo nchi mbali mbali yana badili meli.
Bandari za Dar, Mtwara na Tanga ni kama stendi za dala dala hazina mfumo wa business ya karne ya 21 ndio maana wizi na ufisadi umeshamiri.
Bandari ya Bagamoyo itakuwa ni most efficient port in Africa na geared to put Tanzania on key mariner / logistic hubs


Na yote hayo Uchina waje kuwafanyia WatanZania buuureeee kwa lipi hasa? Au kwa sababu mnaongea kwa kubana pua?
 
Kama Ni kweli basi tunasema Inalilah waina ilahi rajiun.....
Laiti serikali imetenga fedha zake wenyewe kujenga mradi huu basi hii point ya hapa kazi tu ingekua na maana . Lakini mrfadi wa Bagamoyo unajengwa kwa pamoja kati ya Mfuko wa Hifadhi Wa Oman na Serikali ya China..Tanzania haitoi kitu kwa sasa.
sasa unapo simamisha hizi fedha za wachina na Wa Oman ndio watakupa kuendeleza Dar ?
Serikali inatakiwa kuendelea na mradi huu na vile vile kufanya juhudi za kuendeleza bandari ya Dar.

Bqagamoyo imechaguliwa kwa sababu ina kina kirefu zaid na uwanda mkuu ambao utfanya meli kubwa zaidi kufika Tanzania, Na lengo jengine ni kupunguza foleni na kuzidiwa kwa bandari ya Dar es salaam ambayo kutokana na kuwa ndogo kwa eneo ndio sababu kubwa ya kuanzisha hizi ICD Ambazo zimeleta tafrani katika kukusanya kodi.
bandari ya bagamoyo ni kubwa hakutakua na sababu za kuanzisha ICD.
 
Sasa Ultra High Tension Line si ingetumika kusafirishia umeme na co gas?! Au kuna UHT Line zinazotumika kusafirisha gas?! Kama unacholenga ni kusafirisha umeme basi ulazima wa bomba la gesi ungebaki pale na sooner or later tungejenga tu wakati tumeshagharamika kwenye UHT Line. Nasema lazima tungeingia gharama nyingine za bomba la gesi coz" suala la kusafirisha raw gas toka Kusini hadI Dar es salaam haliepukiki unless kama tunge-opt gas yote iwe exported.
Lakini kwa upande mwingine; kwa hapa tulipofikia; kukiwa na additional supply ya gas kutoka Mtwara; hatutaingia gharama nyingine kv miundombinu ya usafiri shati (bomba) tayari ipo. Umeme bado majanga coz' gas inayotoka Mtwara hivi ni kidogo kwa kuwa uchimbaji wa deep sea kwenye gas nyingi haujaanza
Soma vizuri ndugu-Nmeanza na neno "Zile gharama ZINGETUMIKA kujenga hiyo UHT, kwa maana hiyo hazikutumika kujenga hiyo UHT line!
 
Sina tatizo na ulichoandika kwa kiasi kikubwa, shida ni pale unapojenga hoja ya uwepo wa Magufuli kwenye cabinet ya Kikwete katika 'contetx' inayoashiria angeweza kukataa wakati mradi wa Bagamoyo unapitishwa! Nadhani hapa utakuwa unamuonea Magufuli kwa sababu kwanza hatujui kama huo mradi ulijadiliwa kwa kiwango gani kwenye cabinet wakati wa JK, pili, hatujui kama Magufuli alisema ndio au hapana na kama jibu lolote alilotoa (kama alitoa) lilikuwa na nguvu ya kubadili uamuzi wa utawala wa wakati huo, na tatu Bandari ilikuwa chini ya wizara nyingine ambayo Magufuli alikuwa hausiki nayo, unadhani ni wapi Magufuli alikosea?

Baada ya kusema hayo, sasa narudi tena kwenye maelezo yako hapo juu, ni hatua gani sahihi ulitaka RAIS Magufuli achukue dhidi ya Bandari ya Bagamoyo kwa kuzingatia uwepo wa Bandari zingine kama Dar, Tanga etc?

Kwenye red: Kama nimekuelewa vizuri ni kwamba unasema wakati wa Kampeni Magufuli alitumia Bandari ya Bagamoyo kama kauli mbiu ya kampeni. Bado unasimamia hii hoja?

Na pengine ningekuuliza jambo moja (na hii ni kutokana na threads zako nyingi hapa jamvini hasa wakati na baada ya kampeni, 2015) unadhani nani alifaa kuwa rais kati ya Magufuli na Lowassa? Uwe mkweli.

Mkuu kula tano.

Magufuli hakuwa na jinsi maana Kikwete alikwishaamua bandari ijengwe Bagamoyo ingawa hata washauri walipendekeza kuboreshwa kwa bandari za Dar, Mtwara na Tanga.

Lakini pia wazo la kusitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo hata Edward Lowasa alikuwa nalo na hata kwenye kampeni alisema kwamba angesitisha ujenzi huo na kuelekeza fedha kwenye bandari hizo tatu ili kuziboresha.

Hivyo pia si mbaya kutumia uzoefu wa Edo kwenye baadhi ya mambo muhimu kwenye maslahi ya taifa.

Hivyo utaona kwamba tulikuwa na kiongozi aliekuwa amezungukwa na washauri wabovu.
 
Hapa tunaimba nyimbo tu wenzetu wanachanja mbuga. JK ana la kusema kuwa mradi huo ulikuwa na faida

Magufuli alikuwemo, sasa anasema hapana. Huyu ndiye wa kutueleza nini kimebadilika alichokuwa hakioni wakati huo?

Kila siku tunalishwa 'kashata' mpya, tunaimba tu hatufikirii. Hatuna maono na nchi yetu

Tusubiri tangazo siku moja, mtu ataamka asubuhi na kusema akina baba wahasiwe, population imekuwa kubwa!

Mungu pishilia mbali , twaweza fyekwa tu.
Huchoki na kampeni au ndiyo yale ya mvumilivu hula mbivu!

Uchaguzi umeisha au hufahamu kama kampeni za uchaguzi zimeisha!

Kwa kukusaidia hii ni serikali ya awamu ya tano inayojaribu kurekebisha pale ambapo serikali za awamu zilizopita hazikufanya suala lililotakiwa lifanywe au zilifanya kimakosa kutokana na mchanganuo wa priority kulingana na pato la taifa.

Kwani Rais Magufuli kuwepo kwenye kabineti ndiyo inamzuia kuchukua maamuzi ambayo ni tofauti na awamu zilizopita kulingana na mwelekeo wa serikali yake.

Kama katiba inaruhusu Rais kushitakiwa na Rais Magufuli akaamua kumkamata na kumshitaki Rais Kikwete, utakuja hapa na kuanza kusema mbona anamkamata Rais ambaye maamuzi yake aliyoyafanya hata Rais Magufuli alikuwa waziri? Au ndiyo macho ya makengeza kihoja katika kampeni zako?

Kwa nini hupigi kelele kuhusu kukamatwa au kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi waliokuwa chini ya utawala wa Rais Kikwete kama wale wa TAKUKURU,TRA na TPA ambao walifanya madudu lakini serikali ya Rais Kikwete haikuwafanya lolote. Kwa nini husemi Rais Magufuli awaache tu kwa vile hata yeye alikuwepo kwenye serikali ambayo ilichukua maamuzi ya kutowafanya chochote.

Mbona US Secretary of Defense, Robert Gates alifanya kazi katika awamu ya Bush na Obama ambao walikuwa na malengo/sera tofauti katika masuala ya ulinzi hasa kuhusu combat mission nchini Afghanistan. Baada ya kuingia Obama, Sera kuhusu ulinzi ilibadilika na Gates akaendelea kuwa secretary of defense, kwa maana nyingine alichokuwa akikifanya wakati wa Bush Administration akaachana nacho.

Wake up man, hii ni awamu nyingine ya uongozi wa nchi na uchaguzi imamalizika siku ambayo Rais Magufuli aliapishwa kuwa Rais wa Tanzania.
 
Last edited:
Ningependa kuona andiko la mpango wa biashara wa bandari ya Bagamoyo, hata executive summary tu- au hizo ni siri?
 
...ndio mana bado tunasema serikali iliyoondoka ilijaa unafiki mtupu kwenye mipango yake...na JPM anazidi kujidhihirisha kuwa more realistic kwenye mipango yake...maana haingii akilini blah blah kibao zilizopigwa na serikali ya mkwere kuhusu ujenzi wa bandari ya bagamoyo....not knowing kumbe hawakuwa na funds kwa ujenzi ule!!....yaani waliingia mikataba bila uhakika wa funding!....this is amazing....na zile bla blah sijui za oman funds??wakishirikiana sijui na wachina (exim banks or whatever!!)....yaani wabongo kweli wamedanganywa awamu iliyopita....Mi najiuliza bado kwanini watambe na jenzi hizi wakati pesa hawakuwa nazo????.

......ndio maana hata ma meli na mibehewa walinunua mafeki (used)...na hata ujenzi wa ile standard gauge railway nao lazima watakua walituzuga tu....Hivi jamani tusemezane...ni mipango gani ilipangwa na serikali ya mkwere ikatekelezeka????i mean lets be realistic....je mtu humu sasa atuambie mpango mmoja tu wa utawala wa mkwere uliotekelezeka....maana hata kwenye elimu yale madaraja ya viwango vya chini sasa Prof. Ndalichakom anataka kufumua.....hata yale ma mipango ya BRN nayo yamefia baharini...hujasema bado kilimo kwanza...sijui operation tokomeza....ujenzi wa magati ya bandari hakuna.....sasa nini kilipangwa kikatekelezeka kwa asilimia 100???....maana hata ujenzi wa udom ni mipango ya Mkapa....daraja lam kigamboni halijaisha.....na hata huo mradi wa DART wa mabasi ya kasi ndio hivyo wamekula sijui hela na mabasi hawajalipia bandarini......sasa tusemeje wajameni???...maana hata wezi waliokwiba escrow hawajashughulikiwa.....
Mkuu, kwa kifupi nchi yetu imepoteza miaka 10 kusikiliza masimulizi ya mkwere badala ya kuendelea na safari ya maendeleo.
 
Kama Ni kweli basi tunasema Inalilah waina ilahi rajiun.....
Laiti serikali imetenga fedha zake wenyewe kujenga mradi huu basi hii point ya hapa kazi tu ingekua na maana . Lakini mrfadi wa Bagamoyo unajengwa kwa pamoja kati ya Mfuko wa Hifadhi Wa Oman na Serikali ya China..Tanzania haitoi kitu kwa sasa.
sasa unapo simamisha hizi fedha za wachina na Wa Oman ndio watakupa kuendeleza Dar ?
Serikali inatakiwa kuendelea na mradi huu na vile vile kufanya juhudi za kuendeleza bandari ya Dar.

Bqagamoyo imechaguliwa kwa sababu ina kina kirefu zaid na uwanda mkuu ambao utfanya meli kubwa zaidi kufika Tanzania, Na lengo jengine ni kupunguza foleni na kuzidiwa kwa bandari ya Dar es salaam ambayo kutokana na kuwa ndogo kwa eneo ndio sababu kubwa ya kuanzisha hizi ICD Ambazo zimeleta tafrani katika kukusanya kodi.
bandari ya bagamoyo ni kubwa hakutakua na sababu za kuanzisha ICD.

Mkuu serikali haijakurupuka kusitisha mradi huu.

Mradi haujafutwa bali umesitishwa.

Pia fedha za mradi huo bado hajitatolewa zote na ni wachina ndio walianza kutoa kiasi kwa ajili ya hatua za mwanzo, ila hao wa Oman bado hawajatoa hata senti.

Hivyo paper zote zimepitiwa na pameonekana inawezekana kusitisha kisheria.

Msidhani hii serikali ya sasa ni kuchekeanachekeana, hayo yalikwisha siku raisi wa awamu ya tano JJPM alipoapishwa.
 
Mkuu, kwa kifupi nchi yetu imepoteza miaka 10 kusikiliza masimulizi ya mkwere badala ya kuendelea na safari ya maendeleo.

Na hata wenzetu wazungu waloendelea wanaamini kwamba mtoto akifika miaka 10 na ukaona kuna kasoro, yaani hasikii, basi ndio ataendelea kuwa hivyo hadi anakuwa mtu mzima.

Ndio maana akifika miaka 16 anahesabiwa anaweza kujitegemea na mzazi kama ulikuwa unamtunzia akaunti yake benki, basi ni benki haohao ndio wanamtumia kadi mpya ya benki na si ile ya kawaida wa saving account ambayo wewe ndie uliekuwa ukiitunza.

Sasa miaka 10 imepita na tumekuja kugundua aina ya mtoto atakaekuja kuwa mtu mzima ni lazima tujitahidi kumtengeneza mapema kabla hajafika miaka 20.
 
Last edited:
Tatizo lako hutaki kuelewa! Kwahiyo unataka kusema efficiency ya bandari ya Dar ikifikia 100% ndo cargo storage haitakuwa tatizo?

Narudia, Bandari ya Dar hata ikiongeza efficiency kwa 100000000000% not mentioning hiyo 100%, watakachofanikiwa ni improvement ya logistics. Kwamba, meli ikifunga nanga, mzigo utapakuliwa na kuwa cleared on time na kwa outward cargo, nayo itakuwa hivyo hivyo! Kwamba, kazi waliyokuwa wanafanya kwa siku 5, kukiwa na efficiency itafanyika kwa dakika 5!!

Hoja hapa ni kwamba bandari ya Dar es salaam haina uwezo wa ku-handle mzigo mkubwa. Kwamba, sawa una supersonic efficiency; inward na outward cargo imeongezeka; sasa na hiyo supersonic efficiency yako itakusaidia nini wakati hauna facilities za kutosha za kuhifadhi mzigo? Ingawaje kuna ICD za watu binafsi, lakini mzigo unapofika mteja ana haki ya kuhifadhiwa mzigo wake kwa siku 7 bila kulipa chochote... kwahiyo, hata kukiwa na ICDs za watu binagsi kila mtaa, bado bandari wana wajibu wa kuhifadhi mzigo wa mteja at least kwa siku 7... kama ndani ya hizo cku 7 itabidi kupelekwa privately owned ICDs, basi wapeleke wenyewe bandari kwa gharama zao!!
Hii yote ni kwa sababu kule bandarini hakuna maghala ya kutosha ya kuhifadhia mizigo! Kwahiyo, efficiency ita-speed up logistics lakini tatizo la msingi litabaki pale pale!

Bandari ya Tanga, nimewahi kupita pale siku moja... sina hakika kama nilichokuwa nimekiona ndicho kilichopo au ile siku maji yalikupwa! Kwa macho yangu nilishuhudia tishari zinatoa mzigo melini na kuleta gatini! Kama hivyo ndo hali yenyewe, basi maanake ni kwamba kuna shallow water.... kama kuna mtu wa Tanga humu anisaidie. But all in all, hivi pale Tanga kuna bandari ya kuboresha pale kama sio kujenga upya!!

Kwamba Kenya kutaka kujenga bandari nyingine haimanishi ndo wapo sawa... hebu jiulize kidogo! Kenya ina raslimali watu na raslimali fedha! Imetumia raslimali zote mbili kufanya feasibility study na wakaona umuhimu wa kujenga bandari kubwa zaidi kutokana na projections zao!! Yaani bado unaamini wewe usiyefahamu hata wanapokea containers ngapi kwa mwezi unaweza kuwa sawa kuliko wao? Sasa wakati nyie mnadhani ndo wataalamu zaidi wa kuzifahamu white elephant projects, Wakenya na Wamarekani kwa kuwa hawana akili hawa hapa:Kwahiyo hapa Wachina hawana akili, Kenya hawana akili, US Companies nao maboya tu lakini nyinyi tena ambao hata shipping business yenyewe hamuifahamu lakini ndo mna uwezo mkubwa wa kufahamu viable and white elephant project kwenye ports investments!!!! Sasa ikiwa $ 10 Billion mnaona ni li-project likubwa kwelikweli; what abaout hao ambao target yao ni $26 Billion?

Wengine wanaohangaika kutafuta mikopo kwa ajili ya bandari hawa hapa:

In what appears to be a possible clash with Brazilian mining giant Vale, the government of Mozambique plans to secure funding from China to build a deepwater port in Nacala, in the Nampula province. Vale has announced plans to invest US$5 billion in the construction of a deepwater port in Nacala

Wengine wakati wanelezea strategy za China kujitanua, wanaandika:
China’s strategy is to have key points on the Silk Road space such as Bagamoyo become the key sites for the transcontinental exchange of manufactured goods and commodities between the Asian and African economies along the Maritime Silk Road. Chinese policy-makers are convinced that the benefits of China’s infrastructure-driven development model can also be transferred to Africa. Pamoja na yote hayo, bado mnaona Wachina ni wapumbavu wa kutaka kuwekeza Bagamoyo?! Yaani kv Kikwete hatumpendi, ndo basi tena tunaona huu mradi ni kwa manufaa ya Kikwete... yaani Mchina akatafute mkopo wa $ 10 Billion kwa ajili ya kumnufaisha Kikwete!!!

Tatizo la Watanzania, hata vitu ambavyo hatuna utaalamu navyo tunataka kuvitolea maoni na ku-criticize na tunafanya hivyo bila ku-research wala kuuliza wenye utalaamu na suala husika!!! Yaani unakuta mtu anaibuka from nowhere na kuongea bila woga kwamba pale kina kifupi... muulize kifupi futi ngapi hana jibu... kumbe alikariri Jiografia ya shule ya msingi kwamba Mtwara ndo bandari yenye kina kirefu basi ndo tayari anajiona mtalaamu wa kufahamu wapi panafaa kujengwa bandari na wapi hapafai!!!! Muulize ili kujenga bandari kina kinatakiwa kuwa futi ngapi, hana
jibu lakini bado anataka kuwa-criticize watalaamu ambao wameshafanya study!

Nakubaliana na wewe kiasi kuhusu bandari ya Tanga, ilivyo inatofauti kubwa na hii ya Dar au ile ya Mtwara. Kwamba meli inakua mbali na baadae mzigo unabebwa hadi nchi kavu, happ kuna shida kidogo!

Ama kuhusu Mtwara, iko vizuri sana tena sana. Kwa ufupi eneo kubwa la maji ya bahari kule Mtwara ni kina kirefu, achilia pale bandarini, ndiyo maana Mtwara siyo rafiki sana kuogelea. Hivyo kistratrjia, bandari ya Mtwara,Dar na Tanga kwa uchumi tulio nao, tungeanza kuziboresha kwanza. Na ndiyo ile ya Bagamoyo imesitishwa kwanza!
 
Soma vizuri ndugu-Nmeanza na neno "Zile gharama ZINGETUMIKA kujenga hiyo UHT, kwa maana hiyo hazikutumika kujenga hiyo UHT line!
Mimi nilishakuelewa na ndio maana nikasema kama zingetumika kwa UHT bado mahitataji ya ujenzi wa bomba la gas yangebaki pale pale... tungekwepa tu kwa muda lakini ungefika wakati lazima gas kama gas isafirishwe to commercial cities.
 
...ktk ushindani wa biashara ya bandari, tutakabiliana vp na bandari za lamu, mombasa, durban, na hata djibout? Hizi bandari zetu zina uwezo wa kuhudumia 3G, na 4G sea vessel, ambazo lamu port inaandaliwa kuziuhudumia? Tutahimili ushindani wa biashara ya bandari unakuwa? Tunatembea wakati wenzetu wanakimbia!

Ni kama vile rais wa awamu ya 4 allikua kwenye mashindano ya kimataifa ya kutafuta rahisi mbovu kuliko wote duniani, Wote tulijua hapa bagamoyo hakukuwa na sababu nyingine zaidi ya kuonekana mtoto wa mjini kafanya miracle, ndugu yetu katuletea, aibu sana sana sana na haya ni machache tu nasikia kama tungeyajua nusu ya hayo anayoyajua JPM na timu yake, tungetembea uchi barabarani kwa maandamano yasiyo na mwisho. Halafu kale katoto kake kashenzi kanathubutu kuita press conference eti kusema familia yao wanaandamwa, anadhani familia yao ni ya celebrity au mstaafu wakati ni ya mwizi mkuu na baba yake, Nisingeamini kama kuna mtu angeweza kulibetua jambo hili, huu ni mwanzo tuendeleeni kupeleka vijimambo vyote kama kawaida yetu, with detailed evidence, na zile roho za wote walioangamia kwa mateso yako, zikapige kelele mbele ya bwana
 
kukuonyesha jinsi gani watanzania wote isipokua wale walioko kwenye timu yako ya ufisadi iliyopigwa knock out na Rizwana na Ghalib Said Mohamed aliyebadili jina la Home Shopping Center kuwa GSM na Alosco ambapo serikali imekataa kwanza kabla ya kujitangaza mufilisi ngoja kwanza kunaendelea kupanga documents zetu za evidence, the whole country is overwhelmed with the Bagamoyo scandal, Msoga dance is now over,
 
Asante JPM unaona mbali sana bila kumuonea mtu yeyote aibu hata kama ni rais mstaafu kwa maamuzi yake mabovu.ilikuwa haiingii akilini hii hivi hakuwa na washauri au ni washauri wanafiki wa ndio mzee na kutomwambia ukweli bwana mkubwa aliyemaliza muda wake?haki ya Mungu wewe ni Rais bora utatuvusha na kutuondoa ktk aibu tuliyoanza kupata najuta kwanini sikukupa kura yangu.ushauri fanya kazi na wapinzani utajua mengi zaidi ya kuyafanyia kazi kurudisha heshima ya nchi hii.
 
Nakubaliana na wewe kiasi kuhusu bandari ya Tanga, ilivyo inatofauti kubwa na hii ya Dar au ile ya Mtwara. Kwamba meli inakua mbali na baadae mzigo unabebwa hadi nchi kavu, happ kuna shida kidogo!

Ama kuhusu Mtwara, iko vizuri sana tena sana. Kwa ufupi eneo kubwa la maji ya bahari kule Mtwara ni kina kirefu, achilia pale bandarini, ndiyo maana Mtwara siyo rafiki sana kuogelea. Hivyo kistratrjia, bandari ya Mtwara,Dar na Tanga kwa uchumi tulio nao, tungeanza kuziboresha kwanza. Na ndiyo ile ya Bagamoyo imesitishwa kwanza!
Nashukuru kwa kuniondolea mashaka yangu kuhusu Tanga manake ile siku nilivyofika tu nikahisi hapa kuna shallow water! Kuhusu Mtwara, YES, ni natural habor!!

Hofu yangu kuhusu Mtwara ni moja tu! Kama zile cubic feet trillion kadhaa za gas ni kweli zipo Lindi na Mtwara basi biashara ya gas export ikichanganya ile bandari itakuwa busy sana! Na tusisahau, mimeli ya kusafirisha gas inakuwa mikubwa sana... sasa inaweza kuleta delays kwa meli zingine za kibiashara na nadhani inawezekana ndio sababu iliyomfanya Dangote kutaka kujenga bandari yake kwa kukwepa hizo hizo meli za mafuta!! Sasa kwa Mchina ambae lengo lake ni ku-speed up biashara zake ukanda huu halafu anakuja na mmeli wake; anakuta mimeli ya mafuta ime-cover... hawezi ku-favor sehemu kama hiyo hata siku moja.
 
Nashukuru kwa kuniondolea mashaka yangu kuhusu Tanga manake ile siku nilivyofika tu nikahisi hapa kuna shallow water! Kuhusu Mtwara, YES, ni natural habor!!

Hofu yangu kuhusu Mtwara ni moja tu! Kama zile cubic feet trillion kadhaa za gas ni kweli zipo Lindi na Mtwara basi biashara ya gas export ikichanganya ile bandari itakuwa busy sana! Na tusisahau, mimeli ya kusafirisha gas inakuwa mikubwa sana... sasa inaweza kuleta delays kwa meli zingine za kibiashara na nadhani inawezekana ndio sababu iliyomfanya Dangote kutaka kujenga bandari yake kwa kukwepa hizo hizo meli za mafuta!! Sasa kwa Mchina ambae lengo lake ni ku-speed up biashara zake ukanda huu halafu anakuja na mmeli wake; anakuta mimeli ya mafuta ime-cover... hawezi ku-favor sehemu kama hiyo hata siku moja.

Hapana, Dangote uamuzi wake haukutokana na udogo wa Bandari ya Mtwara, hata pale ilipo kwa sasa inaweza kuaccomodate 95% ya meli ya ukubwa wowote duniani,ingawa vifaa vya kupakulia siyo kama hivi vya Dar, ila kwa size ya meli ondoa shaka, ile bandari achana nayo, ni kuongeza tu urefu wa gati lakini meli kubwa uzionazo Dar zikifika Mtwara zinatua bila shida. Maboresho yakifanyika, hakuna sababu ya Bandari ya Dar kuelemewa!
 
Mnajaribu kila njia ku attack character lakini ikija kwenye issues za ukweli hamumuwezi.

Kikwete anadunda na ana rikodi ambayo mpaka sasa hakuna wa kabla yake aliyeifikia. Na ikitokea wa sasa akiifikia basi hilo pia ni chaguo lake, au mmesahau?
Jeshi la mtu mmoja. Kweli sikio la kufa halisikii dawa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom