mankachara
JF-Expert Member
- Sep 27, 2013
- 6,161
- 3,495
Kilichosababisha mkose mkopo ni necta, wamepasisha mpaka vilaza sasa saivi wote wanahitaji kuingia chuoni, haya sasa. Tanzania mfumo wa elimu ni mbovu
Sasa wewe hasira za kukosa mkopo tu....Hebu fikiria hasira za Watanzania milioni 45 kuhusiana na ufisadi, ujangili, ugaidi, utajiri wa nchi kuwanufaisha wachache, watoto wako kukosa mikopo/ajira huku wakiambiwa wajiajiri wakati hawana mitaji ya kuanzia biashara na wao wenye mitaji ya kuanzia biashara watoto wao wanawaingiza kinyemela katika taasisi mbali mbali nchini, hasira za kuona mikataba ya mbali mbali nchini haijali maslahi ya nchi hata kidogo. Warudishie kadi ya Mamndenyi.
Am serious my man. Bodi ya mikopo ina utani na watu. Wafute mashule yao ya serkali. Kwani watoto si watasoma tu.
huu uzi ulikuwa chukuchuku sana , asante kwa picha mkuu .
Me ndio nataman kufa sijapewa hata asilimia o
Salamu sana.
Hapa nakaribia kupasuka kwa uhuni niliofanyiwa na bodi ya mikopo.
Imekuwaje mtoto wa mimi mkulima asipewr mkopo hata senti moja.
Kasoma shule za kidumu na mfagio tokea msingi hadi a levo.
Mtoto wa kike kajitahidi kapata div moja. Jkt kwa mujibu kaende. Leo wanasema eti budget exhausted.
Bado sijaelewa somo.
Tena mi nalalamika kivyangu. Na wewe ulalamike yako.
Chanzo cha kuifilisi bajeti ya masomo ya juu kipo hapa.
Aiseee huu uandishi huu mbona hivi?
Kwani kuna namna ya uandishi ambao hauruhusiwi hapa mpaka uhoji?
Sorry mkuu Kama nimekukwaza lakini sikuwa na nia ya kuhoji nilikuwa nashangaa tu....
Kipi kilichokushangaza? Funguka Mkuu!
Maneno makali
Maneno makali lakini si uongo Mkuu. Sasa kama unashangazwa na maneno makali mauaji ya Mwangosi na hadi leo muuaji wake kupeta uraiani hushangai Mkuu? Waliotaka kumuua Dr Ulimboka hadi leo hii bado wapo mtaani hushangai mkuu, Nchi tajiri kama ya kwetu viongozi wanakuwa mabilionea hata kuficha pesa nyingine nchi za nje huku Watanzania walio wengi wakishindwa kujua hata mlo mmoja kwa siku hawajui utatoka wapi, hushangai Mkuu?
Kitabu cha TCU kinaonesha vigezo vingi sana! Kwanza kuna wenye 1& 2 kwa masomo ya art na hadi 3 masomo ya sayansi wana sifa ya kupata mikopo!
Pia kuna course priority kama Ualimu na Udaktari!
Pamoja na hayo kuna vigezo vya mtu kutokuwa na mzazi au wazazi lakini lazima awe amefaulu!
Mimi nakuomba Mamndenyi nenda TCU ufanye appeal kama nilivyo kwambia kuna mtoto wa ndugu yangu nae kakosa japo hana mzazi mmoja na alipata 2 na wamemwambia afanye appeal wata mzingatia kuna makosa yamefanyika!
Nakuomba uende bodi watakusikiliza!
Kilichosababisha mkose mkopo ni necta, wamepasisha mpaka vilaza sasa saivi wote wanahitaji kuingia chuoni, haya sasa. Tanzania mfumo wa elimu ni mbovu