kantalambazi
JF-Expert Member
- Oct 19, 2012
- 2,010
- 650
Huu si wakati wa kulialia na kulaumu kila kinachofanywa na Serikali,jiulize kwanza wewe umeifanyia nini Serikali,hili swala la upungufu wa dawa baadhi ya watu wanaliongezea chumvi sana kana kwamba kuna wagonjwa wamekufa kwa kukosa dawa.Hivi nchi hii ni moja kama tunavyoaminishwa au vipo vinchi vingine vidogovidogo ninavyiviona sasa? Juzi kuhusu tukio la walimu tarajali kule mbeya vinchi vilijionyesha dhahiri. Jana na juzi navina tena vinchi vingine. Hali hii inaniaminisha kutokuwepo kwa collectiveness katika uongozi wa nchi.
Wanoitwa viongozi hawana mawasiliano chanya hata kidogo.
Haiwezekani makamu wa rais aseme uongo na waziri wa afya ndio awe mkweli.
Kuna haja ya kuwasiliana kwa viongozi wetu juu ya mambo yenye shida ili ikitokea umealikwa uwe na angalau la kuficha au kuanika kama sio kutetea.
Mama Suluhu, ukweli utakuweka huru. Kama kuna tatizo liweke bayana ili tujue namna ya kujibadilisha. Nikuombe umfukuze kazi huyo dadake Ally chemical wa enzi za Saddam kule Iraq kwa kuudanganya umma na kusababisha vifo vilivyowza kuepukika.