Serikali yaajiri walimu hewa(?) Ushahidi huu hapa...

Serikali yaajiri walimu hewa(?) Ushahidi huu hapa...

Uwezo wako wa kufikiri ni mkubwa sana, ni nini kolikuingia mpaka ukachunguza yote haya? With that brain you can be anything....
Amejitaidi kufuatilia lakini mpe Cheo huko tume ya ajira, anaweza piga pia.
 
Naomba nichangie kama ifuatavyo......
1.Katika mfumo wa uombaji wa hizi ajira hakukuwa na uwezekano wa kufuta akaunti ya kuombea ajira mara baada ya kuifungua.
2.hakukuwa na uwezekano wa kudelete attachment kama vyeti vya sekondari au taaluma iwapo mtumaji anahisi ametuma kwa makosa.
3.mtandao ulikuwa unasumbua sana sana tena zaidi ya sana wakati wa kuomba isipokuwa siku chache kabla ya deadline kutimu.
Hivyo basi waombaji wengi walifungua akaunti zaidi ya moja huku wakiambatanisha document zilezile kwa sababu ya kuweka maombi yao kwa usawa zaidi,kumbuka kuwa hawakuwa na uwezo wa kufuta akaunt wala kufuta uploaded document.
Kubwa zaidi documents zilisumbua saaaaaana tena sana kuzi upload.watu wakatangaziana kufungua akaunt nyingine na zitakubali kisha zikakubali.

Wizara nao hawakuwa makini kwa upande wao wakati wa uchambuzi.
Maybe kweli mtandao ulikuwa wasumbua.
Haya vipi na kuhusu jina hilo hilo kumaliza miaka miwili tofauti!???..
 
Kwa hili waziri Jafo na watu wake wahusika 100%. Haiwezekani ukae na data muda mrefu namna ile uje na huu upuuzi. Kuna mtoto/ndugu wa Gerson Msigwa kamaliza kidato cha nne 1994(miaka ishirini na tano iliyopita). Lakini kaajiriwa wameacha kijana aliyena umri wa miaka 24-30 kwa manufaa ya taifa. Wao wanafuata maelezo kutoka juu(vimemo). Aibu hii ni ya Jaffo!!!
kweli mkuu...big up
 
C=/si kama umesoma hesabu ya darasa la kwanza utajua kuwa watu wazima huandika ujinga.
Sio kwamba wako sawa no, yaani kwamba ni makosa ya kibinadamu yaliojitokeza. Na c kwamba wamefanya makusudi ili wafaidi.
 
Dah haya bhana. Huo ni mtazamo wangu. But kila mtu ana perception yake. Ndio maana inakuwa ngumu kuamini kile mwingine anaamini.
Kwamba scolastica yupo female na male halafu ni makosa ayo eeh!!
Ebu kayasome kwanza majina ndo ujue nini watu wanashangaa.
 
Naona kuna watu wanataka wanachoamini wao ndio wanataka wengine waamini hivyo hivyo, ukitofautiana nao basi unaambulia matusi. this is not fair.
1. Kwanza makosa ya kibinadamu yapo. Kwa hiyo kilichotokea kinaweza kuwa kwa kukusudia au kimakosa
2. Hili la jina kutokea mara mbili au tatu huwa lipo. Na tatizo hili huwa linatokea lakini mfumo wa kiajira hulifuta. Kwa mfano mtu amepangiwa vituo viwili, anapofika kituo ambacho ameamua kwenda basi hufanyiwa uhakiki upya na kama kuna makosa haajiriwi na taarifa hutolewa kunako husika. Katika kituo kingine atakuwa hakuripoti hivyo hutolewa.
3. Ni vigumu mishahara kupigwa kwani hata mhusika akifanya mbinu za kuripoti sehemu mbili waajiri wana utaratibu wa kuhakiki payroll kwa wale watoro kwa hiyo mtu wa hivyo hataonekana kazini upande mmoja kwa zaidi ya siku tatu na atatolewa ripoti ya utoro.
4. Kwa utawala uliopo mtu atakayefanya hila za kuchakachua mishahara atakuwa ameamua kujitoa mhanga kitakachomtokea sisemi. Hivi mtu anaweza kuhatarisha ajira yake kwa mishahara ya watu watatu?
5. Mwisho kichwa cha habari kinaweza kuwa sahihi kwa idadi ya waliopita lakini watakao ripoti, hata kama idadi iliyotolewa iko sahihi bila makosa watakao ripoti sio wote, kuna wengine kwa kipindi cha tangu watume maombi watakuwa wamepata shughuli nyingine, au ajira nyingine au hata kufariki. Hapo kwa idadi pungufu (imeitwa hewa) haitakosekana.

NASUBIRI MATUSI KWA WASIOKUBALI MAWAZO TOFAUTI NA YAO - TUMEWAZOEA.
 
hahahahh imebidi nicheke tuuu wazee wakufukunyua kama nawaona vileee
 
Back
Top Bottom