Serikali yaajiri walimu hewa(?) Ushahidi huu hapa...

Serikali yaajiri walimu hewa(?) Ushahidi huu hapa...

Katika ajira 4549 zilizotangazwa wiki iliyopita, baadhi ya majina yameajiriwa mara mbili katika vituo viwili tofauti. Ukifatilia katika matokeo yao ya NECTA kwa mwaka husika, unagundua kuwa namba hazikujirudia.

1.Hawa hapa walimaliza F4 mwaka 2010
View attachment 1085322
Matokeo ya NECTA ni namba moja tu
View attachment 1085323

2. Hawa walimaliza F4 2012
View attachment 1085324
Matokeo ya NECTA ni namba moja tu
View attachment 1085325
3. Hawa hapa mmoja alimaliza F4 2011 na mwingine 2015
View attachment 1085328
lakini jambo la kushangaza ni kwamba mwaka 2015 jumla ya idadi ya watahiniwa iliishia 0126 wakati huyu akionekana kuwa na namba 0131.
2011;
View attachment 1085329

2015;View attachment 1085330

4. Cheki hawa hapa, mmoja kaongezewa SURNAME halafu mwingine namba yake ya F4 imeandikwa kwa irabu 'O' ilihali matokeo yanaonesha aliyefanya mtihani ni mtu mmoja tu.
View attachment 1086167
View attachment 1086170

5. Hawa hapa hawakusoma AGRICULTURE F4. Huyo aliyemaliza F4 2016 alipata 'DIV ZERO'. Je, aliendaje advance? Hata kama angeenda, kuna F4 wa 2016 wa 'School candidate' aliyekwisha maliza SHAHADA?
View attachment 1086203
View attachment 1086214
View attachment 1086215


The Beautyful Ones Are Not Yet Born!
HAPPY MAY DAY!

Hii kali. Kumbe mtu ukichunguza sana utagundua madudu mengi hivi? Mkuu wa nchi anajua hili kweli au wamemficha?
 
Waziri asipochukua hatua kwa madudu haya tutajua ni dili lake tutamuwajibisha
 
Hapo hakuna atakaeingiabkwenye ajira na majina mawili mawili kwanmfumo wa sasa wa usajili maana hawa bado hawajathibitishwa kwenye Halmashauri sasa vyeti vikionekana sehemu mbili lazima atoke mtu. Kwa mfumo wa sasa ni kazi sana kuiba na hata akiiba aliyeingiza jina hata chukua muda mrefu mfumo automatic utamtema. Labda kama wameweka majina ili kujaza idadi ionekane kubwa sawa na watu wenyewe waliojirudia hawazidi watano (5) ko nahisi kutakuwa na makosa ya kiuandishi na uandaa data za hao wahitajika. Ila mwisho wa siku hakuna atakayelamba pesa marambili hafiki mbali atadakwa tuu, huu mfumo mpya aliouleta JPM wa kusaka watumishi hewa umeondoka sana na watu ko kuukwepa ni kazi sana labda iwe inside job ambayo ninauhakika hiyo hela mtagawana watu wengi ili kuficha uchafu na haitakuwa haitoshi kugawana mishahara yenyewe haifiki hata 1M kwa wanaoanza.
 
Mkuu kwa hyo unataka kwenye tufikirie kuwa wamefanya sawa tu, au positive way ipi unazungumzia.??
Sio kwamba wako sawa no, yaani kwamba ni makosa ya kibinadamu yaliojitokeza. Na c kwamba wamefanya makusudi ili wafaidi.
 
Hii kali. Kumbe mtu ukichunguza sana utagundua madudu mengi hivi? Mkuu wa nchi anajua hili kweli au wamemficha?
Watafidia vipi hela walizokwiba kama hawataajiri wafanya kazi feki? Hii ndiyo sababu CAG anapigwa vita. CCM ni ile ile, huwezi kupanda mchicha ukavuna nyanya! CCM kutoa kiongozi mwadilifu ni sawa na nguruwe kuzaa mbuzi au nyang'au kuzaa swala, wapi na wapi! Masikini Tanzania...
 
Watafidia vipi hela walizokwiba kama hawataajiri wafanya kazi feki? Hii ndiyo sababu CAG anapigwa vita. CCM ni ile ile, huwezi kupanda mchicha ukavuna nyanya! CCM kutoa kiongozi mwadilifu ni sawa na nguruwe kuzaa mbuzi au nyang'au kuzaa swala, wapi na wapi! Masikini Tanzania...

Wataumbuana tu, na ukweli utakuwa wazi siku si nyingi, nijambo la muda tu.
 
Sio kwamba wako sawa no, yaani kwamba ni makosa ya kibinadamu yaliojitokeza. Na c kwamba wamefanya makusudi ili wafaidi.

Mkuu kama kauli yako ungekuwa valid basi Mahakama zingekuwepo kwa ajili gani.????
Error huwa zinakuwa mbili au tatu coz kabla hawajaweka hewani kunakuwa na uhakiki kwanza wa data.

Hii ishu ya majina ukisoma kwa makiiiini unaweza kuwa majina hata 200 yamejirudia na wamepangiwa vituo tofauti, mengine wanarudia ya ajira zilizokwisha tolewa.
 
Pointi ya MUHIMU ilofuatwa ni UANACHAMA wa CCM! Kutengeneza WALIMU WATIIFU kwa Sirkali..
 
Mkuu umetumia 'software' gani kubaini ulichobain..

Maana kwa akili ya kawaida, majina zaidi ya buku, AF ugundue ktu km hiki, sio kazi nyepesii..
Mkuu Mimi mwenyewe niligundua hili. Ukiwa mfuatiliaji au mhusika wa hivi vitu utajua tu.
 
Katika ajira 4549 zilizotangazwa wiki iliyopita, baadhi ya majina yameajiriwa mara mbili katika vituo viwili tofauti. Ukifatilia katika matokeo yao ya NECTA kwa mwaka husika, unagundua kuwa namba hazikujirudia.

1.Hawa hapa walimaliza F4 mwaka 2010
View attachment 1085322
Matokeo ya NECTA ni namba moja tu
View attachment 1085323

2. Hawa walimaliza F4 2012
View attachment 1085324
Matokeo ya NECTA ni namba moja tu
View attachment 1085325
3. Hawa hapa mmoja alimaliza F4 2011 na mwingine 2015
View attachment 1085328
lakini jambo la kushangaza ni kwamba mwaka 2015 jumla ya idadi ya watahiniwa iliishia 0126 wakati huyu akionekana kuwa na namba 0131.
2011;
View attachment 1085329

2015;View attachment 1085330

4. Cheki hawa hapa, mmoja kaongezewa SURNAME halafu mwingine namba yake ya F4 imeandikwa kwa irabu 'O' ilihali matokeo yanaonesha aliyefanya mtihani ni mtu mmoja tu.
View attachment 1086167
View attachment 1086170

5. Hawa hapa hawakusoma AGRICULTURE F4. Huyo aliyemaliza F4 2016 alipata 'DIV ZERO'. Je, aliendaje advance? Hata kama angeenda, kuna F4 wa 2016 wa 'School candidate' aliyekwisha maliza SHAHADA?
View attachment 1086203
View attachment 1086214
View attachment 1086215


The Beautyful Ones Are Not Yet Born!
HAPPY MAY DAY!

Kama jina lako lilivyo! you real trust none/ you trust nobody. Nimeipenda hii.
 
Back
Top Bottom