'Serikali ya Wanyonge' ndiyo adui namba moja wa maendeleo. Eti simu/video kupitia wavuti marufuku kupitia 'Bando'!

funluverx

JF-Expert Member
Jun 2, 2014
480
342
Hata salamu sitoi.:(

Leo nina hasira kupitiliza

Ninaweza kumzaba kibao yeyete ambae naweza kukutana naye barabarani nikihisi tu kuwa kwa namna moja ama nyingine amehusika na 'Utopolo' huu, bila ya kujali yeye ni nani ama ana nini.

Ni hivi; kwenye uchambuzi wa magazeti asubuhi hii ya leo, kupitia CLOUDS FM-Radio. Wanasema kwa kifupi kuwa 'Serikali yenu ya Wanyonge' inao mpango mkakati wa kuzuia matumizi ya kupiga na kupokea 'Simu na Video' kupitia Wavuti yaani mfano. WhatsApp, FB na huduma nyingine za aina hiyo.

Sababu kubwa eti, 'Serikali hiyo ya Wanyonge' inakosa mapato kwakuwa huduma hizo ni za gharama ya chini.

Iwapo hii ni kweli.

Huduma kupiga video na simu kwa wapendwa wetu italazimu kutumia gharama tofauti na 'mabando ya Intanet' ambayo kwa kawaida tunaweka yaani 'vifurushi vya intaneti'.

Kwa maneno mengine, ni kuwa gharama itakuwa mara dufu iwapo utahitaji kutumia huduma hizo.

Nikuulize, je, umewahi kutumia Mtandao kwa kutumia salio lako la kawaida?

Mlioko maeneo yanapopatikana Magazeti tafadhalini tafuteni mjiridhishe kwa Undani maana kilichofanywa na Clouds ni ule wanaita 'udanduzi' wa Magazeti leo tar.10/3.

Itakuwa ni Habari iliyopamba magazeti ya leo, hivyo usiniulize ni gazeti gani.

Jamani, mawasiliano si anasa na hii ni Karne ya 21. Hawa watu hawalijui hili?

Argrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr.
 
Mitano tena in Kiswahili!
Five again in English!
Panch in Hindi!
Eeh mnyonge anyongwe!
Apigike mpaka achakae!

Tumejipanga sote wote tutaisoma...ewaah

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Ni hivi; kwenye uchambuzi wa magazeti asubuhi hii ya leo, kupitia CLOUDS FM-Radio. Wanasema kwa kifupi kuwa 'Serikali yenu ya Wanyonge' inao mpango mkakati wa kuzuia matumizi ya kupiga na kupokea 'Simu na Video' kupitia Wavuti yaani mfano. WhatsApp, FB na huduma nyingine za aina hiyo.

Sababu kubwa eti, 'Serikali hiyo ya Wanyonge' inakosa mapato kwakuwa huduma hizo ni za gharama ya chini.
Kwahiyo mwananchi kupata huduma kwa gharama nafuu wao wanaumia, furaha yao ni kumchagulia mwananchi njia ya mawasiliano alimradi tu aumie, nionavyo muda si mrefu tutaanza kulipia hewa tunayovuta
 
WTF.
Yaani serikali ipo tayari kumkamua mwananchi ili yenyewe ipate faida tu?

Serikali ipo kwa ajili ya wananchi na sio wananchi wapo kwa ajili ya serikali.

Sasa badala ya kurahisisha huduma za mawasiliano kwa wananchi kitu ambacho ni muhimu zaidi katika maisha ya kila siku ya wananchi wa leo.
Wao wanachojali ni faida tu yaani hawaoni consequences ni nyingi kuliko faida?

Kama hii ni kweli basi huu ni ujinga uliopitiliza.
 
Hata salamu sitoi.:(

Leo nina hasira kupitiliza

Ninaweza kumzaba kibao yeyete ambae naweza kukutana naye barabarani nikihisi tu kuwa kwa namna moja ama nyingine amehusika na 'Utopolo' huu, bila ya kujali yeye ni nani ama ana nini.

Ni hivi; kwenye uchambuzi wa magazeti asubuhi hii ya leo, kupitia CLOUDS FM-Radio. Wanasema kwa kifupi kuwa 'Serikali yenu ya Wanyonge' inao mpango mkakati wa kuzuia matumizi ya kupiga na kupokea 'Simu na Video' kupitia Wavuti yaani mfano. WhatsApp, FB na huduma nyingine za aina hiyo.

Sababu kubwa eti, 'Serikali hiyo ya Wanyonge' inakosa mapato kwakuwa huduma hizo ni za gharama ya chini.

Iwapo hii ni kweli.

Huduma kupiga video na simu kwa wapendwa wetu italazimu kutumia gharama tofauti na 'mabando ya Intanet' ambayo kwa kawaida tunaweka yaani 'vifurushi vya intaneti'.

Kwa maneno mengine, ni kuwa gharama itakuwa mara dufu iwapo utahitaji kutumia huduma hizo.

Nikuulize, je, umewahi kutumia Mtandao kwa kutumia salio lako la kawaida?

Mlioko maeneo yanapopatikana Magazeti tafadhalini tafuteni mjiridhishe kwa Undani maana kilichofanywa na Clouds ni ule wanaita 'udanduzi' wa Magazeti leo tar.10/3.

Itakuwa ni Habari iliyopamba magazeti ya leo, hivyo usiniulize ni gazeti gani.

Jamani, mawasiliano si anasa na hii ni Karne ya 21. Hawa watu hawalijui hili?

Argrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr.
Tuna miwazuri ya ajabu kweli kipindi hiki !! Utafikiri hayakwenda shule !!!!
 
Ndugulile Amelewa madaraka.
Matokeo ya anachokifanya atakuja kuyapata muda ukifika.
 
Nchi ya ajabu sana wao pekee wanataka ndio waishi maisha bora sisi wengine tuwasindikize kisa hatupo kwenye kundi la kutoa maamuzi ya hovyo hovyo...
 
Back
Top Bottom