Serikali ya CCM isivyo na utu, huruma wala aibu

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,867
35,875
Kwa mara nyingine serikali ya CCM imechanwa laivu. Haina aibu, huruma wala utu. Ajabu na kweli yenyewe inaona sawa tu.

Inamwakilisha nani kwenye minajili hii? Labda walamba asali, wahuni au wale vijana wa hovyo?

Yamejiri laivu kwenye mkutano wa wafanya biashara Kariakoo na Waziri Majaliwa. Kwamba polisi, TRA, wizara ya fedha ni majizi, dhulumati, wanyanyasaji nk?

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameongoza kikao baina yake na vigogo wa wizara wa Fedha na Mipango, Viwanda, Biashara na Uwekezaji pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).


Mawaziri, Dk Mwigulu Nchemba wa fedha na mipango, Dk Ashatu Kijaji wa viwanda, biashara na uwekezaji, Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kidata pamoja na watendaji wao wameshiriki kikao hicho. Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka.


Kikao hicho kimefanyika leo Alhamisi, Mei 17 Ikulu ya Dar es Salaaam ikiwa ni siku moja kupita tangu Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuumaliza mgomo wa wafanyabiashara wa Kariakoo uliokuwa umedumu kwa siku tatu kuanzia Jumatatu ya Mei 15 hadi 17, 2023.


Katika kikao hicho, mawaziri wa fedha, Dk Mwigulu Nchemba, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dk Ashatu Kijaji, Kamishna Mkuu wa TRA, Alphayo Kijaji waliokuwapo walishtumiwa kwa na wafanyabiashara hao kushindwa kuwawekea mazingira mazuri ya biashara.


Vitendo vya rushwa, manyanyaso kutoka kwa watumishi wa TRA, Jeshi la Polisi pamoja na kodi ya stoo vilikuwa miongoni mwa shtuma zilizotolewa huku Waziri Mkuu akivitaka vyombo, TRA na Jeshi la Polisi kujitafakari kutokana na kile kilichoelezwa na wafanyabiashara.


Mbali na Dk Mwigulu, Dk Kijaji, wengine waliokuwapo kwenye kikao hicho cha Majaliwa kilichofanyikiwa Viwanja vya Mnazi Mmoja ni mawaziri, Angellah Kairuki wa Tamisemi, Hamad Masauni wa Mambo ya Ndani pamoja na Katibu Mkuu-Ikulu, Mululi Majula Mahendeka.


Majaliwa aliunda kamati ya watu 14 ukijumuisha maofisa wa Serikali na wale miongoni mwa wafanyabiashara kwenda kupitia changamoto mbalimbali zilizoibuliwa na kuona jinsi ya kuishughulikia.

"Kwamba vitendo vya rushwa, manyanyaso kutoka kwa watumishi wa TRA, Jeshi la Polisi pamoja na kodi ya stoo vilikuwa miongoni mwa shtuma zilizotolewa huku Waziri Mkuu akivitaka vyombo, TRA na Jeshi la Polisi kujitafakari kutokana na kile kilichoelezwa na wafanyabiashara."

Kwamba uchafu huu ukiendelea serikali ipo na imekuwa imetulia tu? Sana sana ikiwataka watuhumiwa kujitafakari tu?

Serikali ya walamba asali au wahuni inapojiitisha kujitafakari ndani ya uponzani ulio usingizini, labda tusubirie maajabu ya Mussa.
 
Sasa umeandika nini cha maana hapo ambacho watu hatukijui kutokana na yote yaliyosemwa na kutokea tangu Sakata hilo lilipoanza?

Mnatujazia sever za JF na kutumalizia bando zetu kwa porojo zisizokuwa na maana yoyote.
 
Tumeshazoea kuburuzwa, hao wafanyabiashara ndio wamekuja kutuamsha kutukumbusha kumbe tukiamua tunaweza, jambo naloliona la msingi lililofanikisha ule mgomo ni udogo wa kundi la watu waliohusika.

Hii ilisababisha pawepo na organisation ya maana iliyofanya mgomo uwe mzito mpaka kumlazimu waziri mkuu kuweka kambi Kariakoo ili kutatua hiyo kero, kwa siku karibia tatu alikuwa akiumiza kichwa nini chakusema ili kuwatuliza wale wafanyabiashara.

Binafsi napenda nione mgomo ukitokea utakaohusisha kundi kubwa zaidi, mfano walimu nchi nzima, huu kama ukiwezekana kutokea naamini ndio utakuwa na impact kubwa zaidi.

Kwasababu walimu ni wengi wenye uwezo wa kubadilisha hali ya mambo kwa wakati mmoja, kwani mgomo wao utawasukuma mpaka wazazi nao kuikaba koo serikali, hapa naona ndio tutachangamka zaidi kama nchi, kwa haki zetu kuheshimiwa na kulindwa.
 
Kwa mara nyingine serikali ya CCM imechanwa laivu. Haina aibu, huruma wala utu. Ajabu na kweli yenyewe inaona sawa tu.

Inamwakilisha nani kwenye minajili hii? Labda walamba asali, wahuni au wale vijana wa hovyo...
Kawwita kuwsylizia kamba zao zilikatikia wapi hadi wakawa wanatafuna nje ya urefu wa kamba zao?

Ukiondoa kauli kali kali lakini uthubutu wa kuchukua hatua alikuwa nao yule bwana wanayemsimanga hadi ndotoni mwao
 
018100094042.JPG
 
Sasa umeandika nini cha maana hapo ambacho watu hatukijui kutokana na yote yaliyosemwa na kutokea tangu Sakata hilo lilipoanza?
Mnatujazia sever za jf na kutumalizia bando zetu kwa porojo zisizokuwa na maana yoyote.
Mods, unganisha huu upuuzi na nyuzi nyingine zilizokwisha wekwa hapa, please.

Mlamba asali, mhuni au kijana wa hovyo bandiko kama hili lazima likutoe nyongo. Serikali ya watu wasio na huruma, majizi, dhulumati, yasiyo na aibu na vya namma hiyo hamtufai!

Habari ndiyo hiyo.
 
Hivi wakuu nyie chadema zile hela mlizokuwa mnapewa na SABODO ilikuwa rukuzu? Au Mkopo? Mlizifanyia nini? Na hizi hela za join the chain zpo wapi Nani amezitunza kwanin hamtupi mrejesho....huu syo utapeli kweli
 
Kwa mara nyingine serikali ya CCM imechanwa laivu. Haina aibu, huruma wala utu. Ajabu na kweli yenyewe inaona sawa tu...
TRA ni CCM, task force ni CCM , vijana wote hao CCM, kiongozi wa wamachinga ni CCM na alitokea Moshi na ni KADA, wanajifanya kuwa hawana uhusiano na CCM.:

SHERIA YA TRA imepitishwa na WABUNGE WA CCM na COVID 19, wote ni CCM , mnachezewa tu na AMOS MAKALLA ameonewa na TRA wameonewa kwa kwakuwa wote hawa wanatekeleza sheria, hawana kosa, adui ni CCM na WABUNGE WAKE
 
TRA ni CCM, task force ni CCM , vijana wote hao CCM, kiongozi wa wamachinga ni CCM na alitokea Moshi na ni KADA, wanajifanya kuwa hawana uhusiano na CCM....
Wakati mwingine tufikiri zaidi ya tunachoona, ccm inaendeshwa na tiss, hata zitto alishasema jambo hili kuwalaumu ccm ni kupoteza muda, ccm hawana maamuzi ni kama kivuli tu..km ccm wana maamuzi wangekubali vipi mtu aliyeondolewa TRA, akawa katibu mkuu akashindwa, akawa balozi akafukuzwa halafu anarudishwa tena TRA maana yake kuna hila ccm kazi yao ni kupitisha yote yanayoletwa kwao, ccm hawana nguvu yoyote! Tuelewe.
 
Wakati mwingine tufikiri zaidi ya tunachoona, ccm inaendeshwa na tiss, hata zitto alishasema jambo hili kuwalaumu ccm ni kupoteza muda, ccm hawana maamuzi ni kama kivuli tu..km ccm wana maamuzi wangekubali vipi mtu aliyeondolewa TRA, akawa katibu mkuu akashindwa, akawa balozi akafukuzwa halafu anarudishwa tena TRA maana yake kuna hila ccm kazi yao ni kupitisha yote yanayoletwa kwao, ccm hawana nguvu yoyote! Tuelewe.
Kaka kosa lako umemaliza mjadala mapema, haya madini umetema vijana wengi hawajui.

Kinachofanyika ni kuhamishwa hapa kupelekwa pale, kesho na keshokutwa watanzania wamenyimwa elimu watabaki kuongozwa na genge flani dogo maisha yao yote.
 
Wakati mwingine tufikiri zaidi ya tunachoona, ccm inaendeshwa na tiss, hata zitto alishasema jambo hili kuwalaumu ccm ni kupoteza muda, ccm hawana maamuzi ni kama kivuli tu..km ccm wana maamuzi wangekubali vipi mtu aliyeondolewa TRA, akawa katibu mkuu akashindwa, akawa balozi akafukuzwa halafu anarudishwa tena TRA maana yake kuna hila ccm kazi yao ni kupitisha yote yanayoletwa kwao, ccm hawana nguvu yoyote! Tuelewe.

Palikuwa na uzi humu mkuu. ya Zitto si mageni:

Kama CCM siyo adui, mchawi wetu ni nani?

IMG_20230519_085416.jpg
 
Tumeshazoea kuburuzwa, hao wafanyabiashara ndio wamekuja kutuamsha kutukumbusha kumbe tukiamua tunaweza, jambo naloliona la msingi lililofanikisha ule mgomo ni udogo wa kundi la watu waliohusika.

Hii ilisababisha pawepo na organisation ya maana iliyofanya mgomo uwe mzito mpaka kumlazimu waziri mkuu kuweka kambi Kariakoo ili kutatua hiyo kero, kwa siku karibia tatu alikuwa akiumiza kichwa nini chakusema ili kuwatuliza wale wafanyabiashara.

Binafsi napenda nione mgomo ukitokea utakaohusisha kundi kubwa zaidi, mfano walimu nchi nzima, huu kama ukiwezekana kutokea naamini ndio utakuwa na impact kubwa zaidi.

Kwasababu walimu ni wengi wenye uwezo wa kubadilisha hali ya mambo kwa wakati mmoja, kwani mgomo wao utawasukuma mpaka wazazi nao kuikaba koo serikali, hapa naona ndio tutachangamka zaidi kama nchi, kwa haki zetu kuheshimiwa na kulindwa.
Umeongea jambo la maana hasa hapo kwenye mgomo wa walimu. Lakini bahati mbaya kabisa kwa sasa hilo haliwezekani. Sababu kubwa ni kwamba, organiser mkubwa anayetarajiwa kusimamia hili, CWT, hana nguvu wala nia ya kuitisha mgomo. Na sababu zipo nyingi tu: mazingira magumu ya kazi, mshahara mdogo, kutolipwa teaching allowance kama kada zingine wanavyolipwa mfano madaktari wanalipwa consultation fee, n.k. CWT hawana nguvu wala nia kwakuwa wao ni sehemu ya CCM, chama tawala. Na mimi nasema nyie CWT, mnakula pesa za michango kutoka kwa walimu lakini hamuwezi kutimiza jukumu lenu la msingi ambalo ni kupigania maslahi bora kwa wanachama wenu, MLAANIWE. Mwisho wa siku chama chenu kife, kwakuwa dalili tumeishaanza kuziona.
 
Kaka kosa lako umemaliza mjadala mapema, haya madini umetema vijana wengi hawajui.
Kinachofanyika ni kuhamishwa hapa kupelekwa pale, kesho na keshokutwa watanzania wamenyimwa elimu watabaki kuongozwa na genge flani dogo maisha yao yote.

Palikuwa na uzi humu miaka 2 iliyopita:

Kama CCM siyo adui, mchawi wetu ni nani?

Of interest alikuwa mtu nyuma ya mtu:

IMG_20230519_085416.jpg
 
Tumeshazoea kuburuzwa, hao wafanyabiashara ndio wamekuja kutuamsha kutukumbusha kumbe tukiamua tunaweza, jambo naloliona la msingi lililofanikisha ule mgomo ni udogo wa kundi la watu waliohusika.

Hii ilisababisha pawepo na organisation ya maana iliyofanya mgomo uwe mzito mpaka kumlazimu waziri mkuu kuweka kambi Kariakoo ili kutatua hiyo kero, kwa siku karibia tatu alikuwa akiumiza kichwa nini chakusema ili kuwatuliza wale wafanyabiashara.

Binafsi napenda nione mgomo ukitokea utakaohusisha kundi kubwa zaidi, mfano walimu nchi nzima, huu kama ukiwezekana kutokea naamini ndio utakuwa na impact kubwa zaidi.

Kwasababu walimu ni wengi wenye uwezo wa kubadilisha hali ya mambo kwa wakati mmoja, kwani mgomo wao utawasukuma mpaka wazazi nao kuikaba koo serikali, hapa naona ndio tutachangamka zaidi kama nchi, kwa haki zetu kuheshimiwa na kulindwa.

Kwenye maelezo yako ninakusoma wewe ukiwa nje. Raha ya ngoma nawe uwemo kuicheza. Mgomo wa maana ulikuwa kama ule wa baba, Mzee Raila. Kuwategemea wafanyakazi hawa wenye kuhofia kufukuzwa kazi ili kuleta mabadiliko ni kuchagua kutokuwatendea haki.

Tunayo madai mengi ya msingi ambapo bila kujua tunafanikiwa vipi kupata majibu tunayoyataka itakuwa ni shughuli kubwa zaidi.

Hatuna tulichojifunza kwa wafanya biashara hawa walioyapata yao kwa kukutana Tahrir? Au tunamsubiri nani kutupatia sisi suluhu zetu bila jasho?

Tunataka haki? Hatutaki tozo? Tukutane Tahrir
 
Kwenye maelezo yako ninakusoma wewe ukiwa nje. Raha ya ngoma nawe uwemo kuicheza. Mgomo wa maana ulikuwa kama ule wa baba, Mzee Raila. Kuwategemea wafanyakazi hawa wenye kuhofia kufukuzwa kazi ili kuleta mabadiliko ni kuchagua kutokuwatendea haki.

Tunayo madai mengi ya msingi ambapo bila kujua tunafanikiwa vipi kupata majibu tunayoyataka itakuwa ni shughuli kubwa zaidi.

Hatuna tulichojifunza kwa wafanya biashara hawa walioyapata yao kwa kutana Tahrir? Au tunamsubiri nani kutupatia sisi suluhu zetu bila jasho?

Tunataka haki? Hatutaki tozo? Tukutane Tahrir
Hao jamaa nimewaona ndio kundi kubwa linaloweza leta impact kubwa na ya haraka kwa muda mfupi zaidi.

Tofauti na individuals kama sisi, ambao mpaka tumpate wa kutu organise, tusiojulikana tutaanzia wapi tuishie wapi, hata kama madai ya msingi tunayo, kutuleta sawa watu wa sampuli yetu nchi nzima haitakuwa kazi ndogo, japo inawezekana.

Watu ambao wakati mwingine tunatofautiana itikadi hivyo kuamua kupingana kwenye madai yetu ya msingi ili kukomoana tu, tena hata kama matatizo yetu yanafanana, naamini walimu ni kundi kubwa la wanaojitambua linaloweza kutuletea mabadiliko ya haraka kama likiamua.
 
Back
Top Bottom