Serikali tusaidieni Fastjet wamezidisha uhuni

Serikali tusaidieni Fastjet wamezidisha uhuni

Mliolipa mipesa yenu ili mpande ndege kwa ubwete kuweni makini, hili shirika la ndege litayeyuka punde!
 
Hawa fastjet n shida n matapeli kuna vku nilibadilia tarehe y return wakanicharge laki 136000 sawasawa nimekata ticket upya.nw wameona wana wateja ndio wanavimba vichwa bei ziko juu hamna tofauti n precision

acha kupotosha umma hiyo ni policy ya budget airline zozote dunianai hata nyuma ya tiketi yako imeandikwa kwa nn usisome kua hakuna kubadili tar ya safari kama masharti magumu si usipande kakate shirika lingine??? low cost pia ina masharti yake!!
 
Punguza munkali wewe, hivi wewe ungekuwa unapanda ndege wakati wa ATC si ungejiua kabisa? uliza tatizi ni nini kabla ya kukurupuka.......safari za ndege sio kama mabasi, unafada zake na una kero zake........Ngoja tukusaidi, inasemekana ndege moja ilipata hitirafu ikiwa angani , hivyo ilirudi Dar kwa matengenezo

Serikali tunaomba msaada wa hizi ndege zimeanza leta matatizo makubwa sana toka asubuhi atujaondoka toka KIA ukiuliza mnaambiwa ndege inatatizo.

Hili limekuwa ni tatizo ambalo alijapatiwa ufumbuzi na hawa watu wa fastjet wanashindwa toa taarifa kuwa ndege aitakuwepo matokeo yake unafika kama hapa KIA ndo wanakuambia ndege akuna.

Kwa mfano hapa saizi KIA abiria wamekasirika na kumchukua mfanyakazi wa fastjet na kumpeleka polisi kwa sababu abiria wamechukia sana.

Tunaiomba serikali ichunguze hizi ndege kama zina usalama wa abiria kuzipanda
 
Hivi tatizo la siku moja tu ndio lihusishe na ufisadi.
​Nina wasiwasi kuwa huna uzoefu wa kusafiri na shirika hili! Kuna kero nyingi kuhusu huduma zinazotolewa na shirika hili ikiwa na kutoa matangazo feki ya bei za nauli zao!
 
Shukuruni Mungu tatizo limegundulika mapema kabla hamja paa angani.

Je, wangewapa taarifa kwamba ndege ina tatizo dakika 10 toka mpae je??
 
Hii ndiyo shida ya bei rahisi. Hata wale ambao walikuwa hawategemei kupanda ndege sasa wamepanda. Ni nzuri sana. Ila tatizo linakuja ni kwenye ushamba. Kana huyu mlalamikaji. Yeye anafikiri ndege ni kama basi, linatembea tu hata kama kuna hitilafu! Tulia, soma mazingira na utazoea tu
 
bora niendlee na ngorika zangu hawa kila mara tunaski malalamiko,potelea mbal hata nikipakizwa kwenye costa pale mzan wa kibaha mosh natoboa
 
Huyu anataka tujue tu kama anapanda ndege leo...have a safe journey.
 
Muda umefika sasa Watanzania tuelewe, fastjet daima wanajitahidi kutoa huduma bora tatizo lililotokea jana la kupata ufa kioo ni la kiusalama sana sasa ulitaka ndege iende hivyohivyo? Tuelimike jamaniii na tuanze kuapreciate na kuisupport fastjet sababu wameleta mapinduzi makubwa sana katika usafiri wa anga.
 
Muda umefika sasa Watanzania tuelewe, fastjet daima wanajitahidi kutoa huduma bora tatizo lililotokea jana la kupata ufa kioo ni la kiusalama sana sasa ulitaka ndege iende hivyohivyo? Tuelimike jamaniii na tuanze kuapreciate na kuisupport fastjet sababu wameleta mapinduzi makubwa sana katika usafiri wa anga.

Kweli we have to appreciate,ukienda na Basi Tabora unafika saa 4 usiku kuanzia saa 12 asubuhi kutoka Dar,with Fastjet sasa nafika Tabora saa 9 mchana via Mwanza then napanda Basi.
 
Back
Top Bottom