Serikali Sasa Irekebishe Ushuru Wa Magari

Serikali Sasa Irekebishe Ushuru Wa Magari

Nilishangaa sana bilionea Laizer alipopata zile bilioni 7 serikali ilichukua kodi ndogo mno,kitu kama milioni mia mbili au tatu ...tu.....
Nikasema kama Laizer angeleta gari la thamani ya bilioni saba basi angetakiwa alipie ushuru bilioni 12 !
Hapo ndio unapoona hii kodi kwa magari ni kukomoana tu



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
sahihi kabisa kaka nimeagiza 4m kodi 6m point kwakwel nimekua mdogo sana loh
 
Hahaha wewe jamaa bhana, kwa hiyo wanapitisha gari zao hapa kwa sababu kwao ushuru ni mdogo? Kwani kwao huko import duty ni asilimia ngapi na uchakavu ni asilimia ngapi ya FOB?

Fanyeni tafiti ya haya mambo kabla ya kukurupuka tu. Kwa hapa E. A ni Tanzania ndio kuna kodi nzuri ya magari. Haswa haya mtumba. Kama ni kubishana njoo na facts hapa sio siasa
bange mbaya sana anaetengeneza anauza 4m kod 6m et kod ndogo ea yote mfyuuu
 
Sasa mkuu kweli kwa hiyo exposure yako ndio unataka ufananishe huku na Japan au Ulaya kwa wingi wa magari? Hivi miundombinu inafanana kweli? Purchasing power inalingana kwa raia wake? Hizo gari wenye vipato wakiongezeka sana na miundombinu ikiwa bora na usafiri wa umma ukiborekaa ndio utaona gari zitashuka bei na zitakosa thamani automatically.

Yani kama mnavyopishana na kukatiza kkoo ndio magari nayo yapite hivyo hivyo! Kuwa serious chief. Lazima miundombinu ijengwa sasa labda mshauri kodi ya magari ipunguzwe ila makusanyo yaelekezwe kwenye kitu kingine. Bila kodi mambo hayawezi kwenda
kumbe ulikua ata huelew watt wanabisha nn ?ndio kod ipunguzwe ndo tunachotaka gar ya mwaka 2004 ama 2002 ushuru 6m bei ya kununua japan 3m loh
 
Uko na chick vision chief, samahani kwa hilo. Unaona usawa wa pua yako tu. Huko vijijini kwenu kuna barabara nzuri za kufanya hayo magari yaweze kupita huko kwa muda wote wa mwaka? Kuna uhakika wa huduma nyinginezo jumuishi za kusaidia huo usafiri kuwa madhubuti na kupunguza mzigo badala ya kuongeza mzigo?

Nguvu kubwa ya manunuzi iko vijijini au mjini? Hizo IST unataka zishuke bei ili zikafanyie nini huko vijijini? Gari zikishuka bei automatically mjini kutajaa misongamano maana ndio kwenye purchasing power kubwa than vijijini. Halafu hizo fuso, pick ups, tractors zina utaratibu wake na kodi rafiki tu.. Usafiri binafsi bado kwa nchi yetu ni anasa. Na ni kwasababu usafiri wa umma haujakaa vizuri namiundombinu nayo sio rafiki sana haijaendelea kiwango chakuridhisha. Ili tupate miundombinu bora na usafiri bora, salama na wa uhakika ni lazima watu walipe kodi tu hakuna namna nyingine. Ndio nashangaa jamaa anakuja na hoja nyepesi hapa eti kodi za magari zishuke ili vijijini wanunue magari. Vijiji gani hivyo ambavyo hata maji ya bomba ni shida, vituo vya afya, barabara na madaraja hakuna.. Umeme etc sasa hao ndio anatetea washushiwe kodi ili wanunue magari.. Kula yenyewe tabu hayo magari wataweka maji humo? Kujua vipaumbele vya nchi ni muhimu. Sio matakwa binafsi ya mtu yanachukuliwa kama ndio mahitaji ya jamii nzima.
Kwa akili hizi we jamaa utakuwa ni mbunge aise. Maana wabunge ndo wanaongoza kuwa akili finyu kama hizi.
 
Nadhani watu waliopewa mamlaka ya kukusanya kodi hawana ueledi wa kazi yao
Tukisema tunapanua wigo wa ukusanyaji kodi ni kwamba watu wengi walipe kodi tena bila ya shinikizo wafurahi kulipa kodi ukishusha kodi za magari kitakachotokea watu wengi wataagiza magari kodi nyingi itakusanywa,the same watalipa bima watanunua petrol kwa wingi wataagiza vipuri kwa wingi mapato yataongezeka maradufu sijui kwanini hawalioni hili.

Mfano tangu kodi ya magari iongezeke kwa mwaka huu uagizaji wa magari umepungua hivo ukusanyaji wa kodi unapungua serikali inapoteza mapato.
Akili kama hii waziri mwenye dhamana hana, mkurugenzi TRA hana.

Halafu utakuta mwenye hii akili hata ajira hana (mfano tu), waliojaa ujinga ndio wamejazana kwenye nafasi.
 
bange mbaya sana anaetengeneza anauza 4m kod 6m et kod ndogo ea yote mfyuuu
kumbe ulikua ata huelew watt wanabisha nn ?ndio kod ipunguzwe ndo tunachotaka gar ya mwaka 2004 ama 2002 ushuru 6m bei ya kununua japan 3m loh
Kwa akili hizi you don't deserve a civil and matured conversation. Nenda bishana na wavaa madera.

Fananisha Tanzania magari ni bei ghali zaidi kuliko nchi gani hapa E. A.. just as simple as that. Sasa ukitaka uanze kunijadili mimi ni kupotoka.
 
Kwa akili hizi we jamaa utakuwa ni mbunge aise. Maana wabunge ndo wanaongoza kuwa akili finyu kama hizi.
Ilikuwaje nyie wenye akili nyingi mkakubali kuruhusu wenye akili finyu wawaongoze katika chombo cha hadhi ya juu ktika nchi. Yanimkawapa dhamana wenye akili finyu wapitishe na watunge sheria za kuwaongoza nyie wenye akili nyingi!?

Sasa hizo akili zenu nyingi zimewasaidia nini? Acha biashara ya kurusha matope utajichafua mwenyewe. Kodi ya magari kuwa kubwa hapa bongo unaipimaje? Ni kubwa kuliko nchi gani hapa E. A? Tutafute kipimo ili tujisahihishe bhas.. Njoo na data sio maneno karibu.
 
Back
Top Bottom