Serikali kujenga kampasi za vyuo 6 katika mikoa 14 nchini

Jamal Akbar

JF-Expert Member
Oct 9, 2014
413
471
Wakati wa mkutano wa Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali za Wanafunzi wa Vyuo Vikuu (TAHLISO) uliofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma jana, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,

Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeanza kujenga kampasi za vyuo vikuu katika mikoa mbalimbali ukiwemo Kigoma, Tabora, Singida, Tanga, Ruvuma, Kagera ili kutoa fursa kwa watoto wa Kitanzania kupata elimu ya juu.

Pia alisema serikali itajenga jumla ya vyuo vya ufundi stadi (VETA) 65 ambapo vyuo 64 vitajengwa katika wilaya 64 ambazo hazina VETA na kimoja cha mkoa kitajengwa mkoani Songwe.

Ameeleza kuwa Serikali imeamua kujenga kampasi hizo katika maeneo hayo 14 ambayo hayana kampasi ili kuwawezesha watoto wa kitanzania kupata elimu bora.

Vilevile Profesa Mkenda alisema serikali pia imetenga fedha kwa ajili ya kuwasomesha wahadhiri wa vyuo vikuu vya serikali na binafsi ambapo dola milioni moja imetengwa kwa ajili ya kuwaendeleza kilimo wahadhiri katika vyuo binafsi.

16 (1).jpg
 
Mavyuo mengi yote ya nini badala ya kuboresha kwanza hiyo elimu inayotaka kutolewa.Tengeneza mpango madhubuti wa kuifanya elimu iheshimiwe na wala si vinginevyo
 
Mi nikajua tunaongeza technical school kila kona kumbe tunaongeza degree
 
Yatafanyika kwa muda wa miaka mingapi?
5, 20 au 50??
 
Mavyuo mengi yote ya nini baadala ya kuboresha kwanza hiyo elimu inayotaka kutolewa.Tengeneza mpango madhubuti wa kuifanya elimu iheshimiwe na wala sivingnevyo

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
Well said.

Ni kweli tunauhitaji wa vyuo, lakini kuboresha hiyo elimu yenyewe ni muhimu zaidi, ili tusiwe tunaongeza wahitimu wangi ambao hawawezi kuzitumia elimu zao.
 
Pia alisema serikali itajenga jumla ya vyuo vya ufundi stadi (VETA) 65 ambapo vyuo 64 vitajengwa katika wilaya 64 ambazo hazina VETA na kimoja cha mkoa kitajengwa mkoani Songwe.

Ameeleza kuwa serikali imeamua kujenga kampasi hizo katika maeneo hayo 14 ambayo hayana kampasi ili kuwawezesha watoto wa kitanzania kupata elimu bora.
Hongera Rais

Nashauri nguvu zielekezwe kuwekeza kwenye fani zenye kujiajiri
 
Back
Top Bottom