Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 3,119
- 1,428
SERIKALI KUJA NA MPANGO WA KUWALIPA POSHO WAZEE
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi amesema Serikali inaangalia uwezekano wa kuwanusuru wazee na lindi la umasikini kwa kuanza kuwalipa posho kila mwezi endapo hali ya uchumi itaruhusu.
Naibu Waziri Katambi ametoa kauli hiyo bungeni Jijini Dodoma leo Aprili 29, 2025, wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu, Christina Mnzava aliyetaka kufahamu mpango wa Serikali kuja na sera ya kuwapatia posho wazee wote nchini kama inavyofanyika Visiwani Zanzibar.
"Ni kweli kwa upande wa Tanzania Visiwani wameanza utaratibu huo (wa kuwalipa posho wazee) na sera hii ya mwaka 2003 moja ya maeneo ambayo yamewekewa mkazo ni pamoja na hili la kuangalia hali za kiuchumi na kuwanusuru wazee katika lindi la umasikini na changamoto za kiuchumi...Kwa hiyo tutaendelea kulifanyia kazi kupitia ofisi ya Waziri Mkuu na wizara husika kuona kama hali itaruhusu hilo litatekelezwa". amesema Naibu Waziri Katambi