Watu wenyewe wa Dar ya tangu enzi za Shomvi anatoka Barawa, tangu enzi za Sayyidina Said Majid, tangu enzi za Dr. Seward na Pazi Mazungera, tangu enzi za Jumbe Tambaza huwezi kutusikia tunaongea maneno mbofumbofu.
Ni hawa wa kuja juzi na mbio za Mwenge hata ukiwauliza Odeon iko wapi, City Drive imeanzia wapi na kuishia wapi na kwa nini imebadilishwa jina? Kitchwele ni wapi? Mwembetogwa pako wapi? Mchafukoge inaanzia wapi na kuishia wapi?
Mtu hajui Aga Khan kauziwa na nani uwanja wa kujenga shule, au kwa nini Salender Bridge linaitwa Salender Bridge.
Mtu hajui Tangi Bovu liko wapi, na kwa nini kwa Sykes kunaitwa kwa Sykes.
Hamjui Mwanamboka alianzia wapi, Mengi alijaza wino kwenye peni nyumbani kwake wapi, wala kiosk cha kwanza cha Bakhressa kilikuwa wapi.
Mtu hajui Saigoni iko wapi, na chapati kwa mchuzi inaliwaje.
Hamjui Sykes wala Mwinyijuma, Chamgui wala Rupia.
Hana historia ya familia Misheni kota wala Gerezani.
Watoto hawajui hata historia ya Jumbe Tambaza alivyomtilia ngumu Carl Peters kuuza vijiji vya Mzi Mzima kwa rupia 15 kila kijiji.
Leo wanataka kukuambia Dar es salaam kwao wanakataza wengine wasije.
By Tambaza na mimi nikirudi naweza kuitwa mgeni wakati babu wa Bibi yangu kajenga Azania Front mpaka kulimaliza 1903 !
Sasa kama.wenye mji wenyewe hatuwezi kukataza wagenu, mshihiri gani wa kutoka wapu anaweza kujipakazia yeye Dar ndio kwao?