Kuna hoja ya msingi, ingawa najua itapingwa hapa kwa hoja nyepesi. Hakuna sababu ya mtu kuja Dar halafu analala kwenye vibaraza vya maduka kwa kutandika na kujifunika mabox, halafu mtu anasema tutabanana hapa hapa!
![]()
17.-(1) Every citizen of the United Republic has the right to freedom of movement in the United Republic and the right to live in any part of the United Republic, to leave and enter the country, and the right not to be forced to leave or be expelled from the United Republic.
(2) Any lawful act or any law which is intended to -
(a) curtail a person's freedom of movement and to restrain or imprison him; or
(b) limit a person from exercising his freedom of movement so as to -
(i) execute a judgment or court order; or
(ii) compel a person first to comply with any obligations arising under another law; or
(iii) protect public interest in general or preserve certain special interest or interests of a certain section of the
public,
such act or law shall not be construed or be held to be repugnant to or inconsistent with the provisions of this Article.
![]()
Wewe masai! Una work permit ya kulinda usiku na kusuka nywele mchana?
Nafikiri wakati umefika sasa kwa Serikali ianze kuzuia watu kutoka Mikoani kuja Dar, tumetosha sasa! ikiwezekana Waruhusiwe wale tu ambao wamepata kazi au walioitwa kwenye usahili... Hali inatisha sana ukienda Ubungo Mabasi yanakuja yamejaa na yanaondoka tupu, kwa nini hamkai huko Mikoani mbona mnatutambia kuna kuna Hali ya Hewa nzuri, sasa ni nini kinawaleta Dar?
Kiranga salute sana mkuu,
Unanikumbusha enzi za kula ice cream kwa bakhresa hapa livingstone au kwa chalinze lumumba nikitaka pamba kijiti nashuka malapa inn!!!!!
Fete fair ya wagiriki (mabembea) mnazi mmoja!!!!
Kulaboda Mchikichi,gerezani to keko! !!!!!
Mix kwa Kenge!!!!!!
Nakimbia na pila (used tyre) Livingstone yote!!!!!
Ukonga ndo kwa babu ukiambiwa safari ya huko maembe yanatetemeka,na narudi na pepeta za kutosha!!!!!!
Dar was Dar kaka sasa mtu kama huyu ukimuuliza pepeta ni nini atatoa macho hapa!!!!!
Wapumzike kwa amani wazee wenye mji wao!!!!!!
Duh, umenikumbusha pepeta mwana.
Kwa Bakhressa watu tumeenda kuangalia "Commando John" huku unapata world class chocolate ice cream.
Baadaye Kidogo unaenda kumuangalia Jabali la Muziki Marijani Rajab au Gurumo na madaktari, bure, courtesy of Prof. Sarungi and crew.
Watu wamekuja mjini baada ya side streets kuwekwa lami halafu leo wanataka kujifanya mji wao?
Aaaargh kama mpaka pepeta umepiga basi kaka siongezi tena Kiranga!!!!
Kuna mtu hapo kaongelea kulala kibarzani ndo kaonesha ugeni wake dhahir shahir wenyewe nyumba zetu za udongo na miti joto sana mpaka zipoe hiyo saa tano muda wote tulale wapi sasa!!!!????
Ndiyo mimi nikamwambia watunge sheria kuwazuia mamwinyi wasilale vibarazani tuone.
Hizo pepeta alikuwapo bibi mpenzi, shamba lake likiwa hapa Tangi Bovu, ukikaa shambani unaliona tangi hili, liko upande wa pili tu wa barabara, lina kutu kichizi.
Basi kabla ya kuvuna mpunga lazima upatiwe pepeta kwanza.
Leo wanakuja Wakavirondo hata Tangi Bovu hawajawahi kuliona, wanataka kusema Dar mji wao.
Nikirudi mimi nikiyeona Sozigwa anachukia imla kutoka kwa mchonga live nisemeje?
Acha babu umenikumbusha bibi zangu walale pema waliko!!!!!!!!
Ha ha ha haaaaa umemtaja mzee Sozigwa umenikumbusha mtemi mmoja marehemu Sykes Alli huyu alinunua Land Rover 110 mpyaaaaa by then wanazo serikalini tu akatua airport afuatwe na hiyo mashine then mtundu mmoja pale katoka nayo.........anyways!!!!!!!
Watu wanawasikia watu redioni leo wanataka kufukuza wengine ati wao wamekuwa wenyeji!!!!!!
Mkuu Kiranga hope huyo nani sijui mtoa mada atakuwa kajitafakari sasa na kajua kama Dar ni dambwe tu kama mengine kila uchao channel zinaamka na kufa in a Darwinian fashion!!!!!
Kuna hoja ya msingi, ingawa najua itapingwa hapa kwa hoja nyepesi. Hakuna sababu ya mtu kuja Dar halafu analala kwenye vibaraza vya maduka kwa kutandika na kujifunika mabox, halafu mtu anasema tutabanana hapa hapa!
![]()
hahahahahaaa ...unaogopa watachukua ajira yako? tulia waje. mi nimeingia jana na ndo kwanza natafuta kazi..
wakuja utawaona tu,, kukaa dar miaka 4-5 wanajiona ndo wenyeji...wenyemji tupo kimyaa na hadi tumehamia pembezoni mwa mji kwa jinsi karaha za mji zilivyotuchosha.Wewe na hiyo Dar yako unalalamika hivyo je wenzetu wa New York ambapo biashara ya kimataifa inafanyikia pale nao wasemeje?