Serikali iwe macho: Tunapoelekea vyama vya upinzani huenda vikajeruhi, kuharibu mali na hata kusababisha mauaji ili kuhalalisha ''malalamiko'' yao

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

Kumekuwa na juhudi kubwa kwa vyama vya upinzani kupitia mitandao ya kijamii kupotosha yanayoendelea kuanzia kipindi cha uandikishaji, uteuzi wagombea na hatimaye uchukuaji na urejeshaji wa fomu.

Kipindi cha kujiandikisha walikuja na kampeni susia susia huku wakitoa picha za kuonesha kuwa zoezi la kujiandikisha wapiga kura litakwama, wakafeli wao. Baadaye wamejikuta wakitunga uongo kupitia mitandao ya kijamii kuwa wagombea wa upinzani wanadhulumiwa huku katika kipindi cha kujiandikisha uongozi wa Chadema hususani mkoa wa Kilimanjaro ulikiri kukosa fedha za kuweka mawakala tafsiri pana ni kuwa hata kupata wagombea wa uhakika ni shida.

Baada ya uongo unaosambazwa kupitia mitandao ya kijamii ikiongozwa na Zitto,Lema na ''vikaragosi'' kuonekana kushindwa serikali iwe macho kwani baada ya wao kukosa uhalali kwa wananchi hawatakuwa na ''option'' nyingine zaidi ya kuetengeza mauji, kujeruhi, kufanya vitendo vya kuharibu mali na wizi kwa kuvizia ili tu kuonesha ulimwengu Watanzania ''hawajaridhika''.

Ukizunguka mitaani,vitongojini na vijijini wananchi wanaendelea na shughuli zao kujiletea maendeleo lakini baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani wamejikita kwenye mitandao ya kijamii huku wakitoa vijineno kama vile, ''nchi itawaka moto'', ''wananchi wamechoka'' ili wakija kufanya uhuni wao iwe rahisi kuhalalisha.

Nimalize kwa kusema navishauri vyombo vya ulinzi na usalama viimarishe intelijensia ili kuhakikisha waovu wote wanamulikwa na kuumbuliwa mipango yao.

Nawasilisha kwa mjadala wenye afya.
 
Sio wapinzani tu, mi sio mfuasi wa chama chochote bali ni mtanzania ninayependa haki.watendaji wote waliokwamisha uchaguzi kwangu sina Huruma nao hata wakiuliwa.Sisi wengine tunaipenda zaidi Tanzania kuliko vikundi vya kiharamia viitwavyo vyama vya siasa.
 
Tanzania ni yetu sote.

Inawezekana anae lalamika akawa na nia njema kuliko unae amini anatenda haki. Na inawezekana ni ile hali ya binadamu kuhisi mawazo yake ni sahihi hasa wapinzani huamini wao ni lazima wasikilzwe hata kama jambo halina umuhimu.

Tuweke uwanja sawa wa kufanya siasa ile kila mmoja ashinde kwa sera zake na sio kwa kuwa ni wa chama fulani.
 
Kuna wapinzani walikuwa wanahamasisha watu wasijiandikishe kwenye daftari la wapiga kura
Leo hii wanachukua fomu za kugombea uongozi

Wapinzani msitufanye sisi mandondocha
Hiyo haihalalishi hujuma kwenye mchakato wa uchaguzi, walipaswa kupewa fomu ili washindwe kwenye sanduku la kura, Tanzania sio mali ya kikundi kimoja kinachojiita CCM.
 
Ni hivi, uzoefu unaonyesha kukiwa hamna haki njia pekee ni kushikana kidogo ili nidhamu irejee. Hapo wapinzani walipofikishwa bila kufanya jino kwa jino hawatakaa wapate haki. Huu uchafu unaoendelea kwenye box la kura ni lazima plan B itumike.
 
Ni hivi, uzoefu unaonyesha kukiwa hamna haki njia pekee ni kushikana kidogo ili nidhamu irejee. Hapo wapinzani walipofikishwa bila kufanya jino kwa jino hawatakaa wapate haki. Huu uchafu unaoendelea kwenye box la kura ni lazima plan B itumike
kwahiyo uzushi wa Zitto na Lema ndio unakutia hasira?njoo rodi basi,utapigwa na utachakaa.
 
kwahiyo uzushi wa Zitto na Lema ndio unakutia hasira?njoo rodi basi,utapigwa na utachakaa.

Ni kweli, hakuna uzushi bali ni mambo tanayaona kwa macho yetu, tena hayo yanasemwa ni machache. Hamna muda lazima tutawafurahisha. Mnaharibu uchaguzi kisa mnategemea vyombo vya dola.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Huyu mtoa maada hata simuelewi binafsi, haya majina ya wagombea wa upinzani yanaondolewa kwa sababu zipi? Kama kuna mambo mazuri yanafanywa c waache wananchi wachague mtu wanaemtaka? Usidanganye umma watanzania c wajinga.
 
Huyu mtoa maada hata simuelewi binafsi, haya majina ya wagombea wa upinzani yanaondolewa kwa sababu zipi? Kama kuna mambo mazuri yanafanywa c waache wananchi wachague mtu wanaemtaka? Usidanganye umma watanzania c wajinga.
Hivyo ni ''vilio'' ili kuhalalisha wanayotaka kuyafanya baada ya kukosa uhalali kwa wananchi.
 
Endeleeni kuchochea kuni mlianzia chaguzi ndogo baadae moto utawaka tu ngoja tuome mwisho wake wote tutakuwa mashaidi tunaeleka kubaya huku tunajuwa lakini tunaona hakuna shida.
 
Wala sisi hatutafika huko. Watanzania wataamua wenyewe siku zikifika.
 
Wewe ndio unayawaza hayo nauenda unataka kuyafanya.

Sisi wengine kutwa tunaombea Amani yanchi yetu alafu wewe unawaza ujingaujinga. Hali ni shwariii labda kama wewe nagenge lako ndio mnataka muigeuze kinyume chake
 
Hiki chama ukijiunga nacho tu unapoteza uwezo wa kufikiri hapohapo unakua unaona kila kitu ni sahihi.
 
Back
Top Bottom