Nanyaro Ephata
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,221
- 1,788
Sakata la Mkurugenzi Jiji la Arusha, Halmashauri inapaswa kuvunjwa
Jana Mbunge wa Michongo wa Arusha mjini alisikika akilalamika mbele ya Waziri Mkuu kuhusu tuhuma kadhaa ambazo zinamkabili Mkurugenzi wa Jiji!
Mosi huyu Mbunge akumbuke kuwa hana uadilifu wa kukemea ufisadi wa aina yoyote maana yeye ni zao la ufisadi. Matendo ya Mkurugenzi ni matokeo ya uchafuzi wa 2020 ambako CCM ilimtumia Mkurugenzi huyu kupora haki za watu wa Arusha, matokeo yake imezaliwa baraza la madiwani la michongo na kibogoyo.
Ni wazi baada ya kumtumia sasa hawana kazi naye, hili liwe funzo kwa wengine wanaotumiwa kupora haki za watu
Kwa mujibu wa sheria za serikali za mitaa, Mbunge ni mjumbe wa baraza la madiwani na ni mjumbe wa kamati ya fedha na utawala ya Halmashauri. Moja ya majukumu ya kamati hii ambayo kisheria inakutana kila mwezi ni kusimamamia mapato na matumizi ya fedha na mali za Halmashauri.
Sasa iliwezekanaje kamati inayokutana kila mwezi na Mbunge akiwepo ishindwe kubaini ubadhirifu mkubwa kama huu?tafsiri yake ni rahisi tu Jiji la Arusha halina mbunge wa madiwani wenye uwezo na weledi. Kamati hii inakutana kwa gharama walipakodi lakini imeshindwa hata kujua kuwa shule yake yenyewe imepangishwa.
Halmashauri ambayo imeshindwa kuendesha shule ni Halmashauri iliyofeli na suluhisho la kudumu ni kuivunja na kuunda tume ya jiji kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Fikiria ujasiri wa mkurugezi kuagiza fedha ziwekwe kwenye akaunti binafsi ya mtumishi au ujasiri wa kukodisha shule,ujasiri huu unatupa picha tu kuwa kuna hitilafu kubwa kwa upande wa madiwani na mbunge wao! Madiwani michongo!
Mbunge michongo! Mkurugezi michongo!
Wakati wanapanga wamachinga niliandika kuhusu ufisadi huu,bajeti ya kupanga wamachinga ilikuwa zaid ya bilioni moja. Ni hatari kutumia mamilioni ya fedha kwa jambo shikizi ambalo sio la kudumu, maeneo ya Machame na Nyire ni open spaces passive, kwa mujibu wa sheria ya mipango miji open space passive haziruhusiwi kufanyiwa maendeleo yoyote, haya ndio baraza la madiwani la michongo liliona ni sehemu ya kuwekeza bilioni moja, sehemu ambazo kibiashara hazina tija na kisheria ni haramu. Hii ni hitilafu kubwa
Tangu hayo masoko shikizi yamejengwa ni zaidi ya miezi eti madiwani na mbunge hawaoni hata mabati kuwa ni geji 32 alafu wanataka waitwe Waheshimiwa, hii hitilafu kubwa.
Kimsingi tangu 2020 shughuli za maendeleo kwenye jiji la Arusha zimesimama kwa kuwa makusanyo ni hafifu na matobo ni mengi
Ni katika siku za karibuni gari la Mkurugenzi limekamatwa huko mkoa wa Kilimanjaro likiwa na mirungi, madiwani wapo kimya, mbunge yupo kimya, hata kama kuna hatua za kipolisi zinaendelea walipaswa kuchukua hatua za kimadili.
Wito wangu kwa mamlaka za Serikali zichukue hatua stahiki mapema na wavunje Halmashauri ili kunusuru mali ya umma.
Nanyaro EJ
Jana Mbunge wa Michongo wa Arusha mjini alisikika akilalamika mbele ya Waziri Mkuu kuhusu tuhuma kadhaa ambazo zinamkabili Mkurugenzi wa Jiji!
Mosi huyu Mbunge akumbuke kuwa hana uadilifu wa kukemea ufisadi wa aina yoyote maana yeye ni zao la ufisadi. Matendo ya Mkurugenzi ni matokeo ya uchafuzi wa 2020 ambako CCM ilimtumia Mkurugenzi huyu kupora haki za watu wa Arusha, matokeo yake imezaliwa baraza la madiwani la michongo na kibogoyo.
Ni wazi baada ya kumtumia sasa hawana kazi naye, hili liwe funzo kwa wengine wanaotumiwa kupora haki za watu
Kwa mujibu wa sheria za serikali za mitaa, Mbunge ni mjumbe wa baraza la madiwani na ni mjumbe wa kamati ya fedha na utawala ya Halmashauri. Moja ya majukumu ya kamati hii ambayo kisheria inakutana kila mwezi ni kusimamamia mapato na matumizi ya fedha na mali za Halmashauri.
Sasa iliwezekanaje kamati inayokutana kila mwezi na Mbunge akiwepo ishindwe kubaini ubadhirifu mkubwa kama huu?tafsiri yake ni rahisi tu Jiji la Arusha halina mbunge wa madiwani wenye uwezo na weledi. Kamati hii inakutana kwa gharama walipakodi lakini imeshindwa hata kujua kuwa shule yake yenyewe imepangishwa.
Halmashauri ambayo imeshindwa kuendesha shule ni Halmashauri iliyofeli na suluhisho la kudumu ni kuivunja na kuunda tume ya jiji kuelekea uchaguzi mkuu 2025.
Fikiria ujasiri wa mkurugezi kuagiza fedha ziwekwe kwenye akaunti binafsi ya mtumishi au ujasiri wa kukodisha shule,ujasiri huu unatupa picha tu kuwa kuna hitilafu kubwa kwa upande wa madiwani na mbunge wao! Madiwani michongo!
Mbunge michongo! Mkurugezi michongo!
Wakati wanapanga wamachinga niliandika kuhusu ufisadi huu,bajeti ya kupanga wamachinga ilikuwa zaid ya bilioni moja. Ni hatari kutumia mamilioni ya fedha kwa jambo shikizi ambalo sio la kudumu, maeneo ya Machame na Nyire ni open spaces passive, kwa mujibu wa sheria ya mipango miji open space passive haziruhusiwi kufanyiwa maendeleo yoyote, haya ndio baraza la madiwani la michongo liliona ni sehemu ya kuwekeza bilioni moja, sehemu ambazo kibiashara hazina tija na kisheria ni haramu. Hii ni hitilafu kubwa
Tangu hayo masoko shikizi yamejengwa ni zaidi ya miezi eti madiwani na mbunge hawaoni hata mabati kuwa ni geji 32 alafu wanataka waitwe Waheshimiwa, hii hitilafu kubwa.
Kimsingi tangu 2020 shughuli za maendeleo kwenye jiji la Arusha zimesimama kwa kuwa makusanyo ni hafifu na matobo ni mengi
Ni katika siku za karibuni gari la Mkurugenzi limekamatwa huko mkoa wa Kilimanjaro likiwa na mirungi, madiwani wapo kimya, mbunge yupo kimya, hata kama kuna hatua za kipolisi zinaendelea walipaswa kuchukua hatua za kimadili.
Wito wangu kwa mamlaka za Serikali zichukue hatua stahiki mapema na wavunje Halmashauri ili kunusuru mali ya umma.
Nanyaro EJ