Salaam wanabodi,
Ndiyo, kumekuwako ukosefu wa mafuta katika baadhi ya vituo vya kuuzia mafuta nchini, ukifika hapo unaambiwa petrol imekwisha.
Mtazamo wangu ni kuwa hawa wafanya biashara aidha wanakuwa wakisubiri bei kupanda au wanatengeneza uhitaji wa ziada kwa sababu wanazuia usambazaji na hivo kupelekea bei kupanda.
Wakati wa Mwendazake sikusikia hata siku moja matatizo ya namna hii. Ingawaje nakumbuka wakati wa Mzee Kikwete kuna wafanya biashara walitikisa kiberiti kwa kugoma kuuza mafuta eti mpaka walichokitaka kitekelezwe.
Namshauri Mama yetu hawa jamaa asiwachekee kabisa watatusumbua sana. Maghala yao ya kuhifadhi mafuta yanafahamika yalipo ni kupeleka askari tu na kusimamia uuzaji wa mafuta mpaka yaishe na ataegundulika kuhujumu juhudi za usambazaji unaotambulika rasmi akamatwe na kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi, hawa wapuuzi ndio watanyooka!
Asietaka kufanya biashara nchi hii aondoke aende kule anakoona atafanya vile anavotaka yeye.
Mama yangu, hivi kweli hawa akina sijui .....OIL, OIL ....... , OIL ........ wanaichezea serekali kweli?
Namalizia kwa kuishauri serikali isiwachekee hawa watu hata kidogo
Ndiyo, kumekuwako ukosefu wa mafuta katika baadhi ya vituo vya kuuzia mafuta nchini, ukifika hapo unaambiwa petrol imekwisha.
Mtazamo wangu ni kuwa hawa wafanya biashara aidha wanakuwa wakisubiri bei kupanda au wanatengeneza uhitaji wa ziada kwa sababu wanazuia usambazaji na hivo kupelekea bei kupanda.
Wakati wa Mwendazake sikusikia hata siku moja matatizo ya namna hii. Ingawaje nakumbuka wakati wa Mzee Kikwete kuna wafanya biashara walitikisa kiberiti kwa kugoma kuuza mafuta eti mpaka walichokitaka kitekelezwe.
Namshauri Mama yetu hawa jamaa asiwachekee kabisa watatusumbua sana. Maghala yao ya kuhifadhi mafuta yanafahamika yalipo ni kupeleka askari tu na kusimamia uuzaji wa mafuta mpaka yaishe na ataegundulika kuhujumu juhudi za usambazaji unaotambulika rasmi akamatwe na kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi, hawa wapuuzi ndio watanyooka!
Asietaka kufanya biashara nchi hii aondoke aende kule anakoona atafanya vile anavotaka yeye.
Mama yangu, hivi kweli hawa akina sijui .....OIL, OIL ....... , OIL ........ wanaichezea serekali kweli?
Namalizia kwa kuishauri serikali isiwachekee hawa watu hata kidogo