#COVID19 Serikali iongeze elimu dhidi ya chanjo ya COVID-19, imuombe Askofu Gwajima asiongelee chanjo

Liability

Member
Oct 20, 2019
75
100
Jana nilimskiliza tena askofu Gwajima! Matamshi yake yanaungwa mkono na watu wengi sana kuliko hata watu waliopewa ubalozi wa Corona. Nashauri yafuatayo:

1. Serikali iongeze elimu juu ya chanjo
2. SerikaLi imuombe Gwajima abaki na msimamo wake lakini asiongelee chanjo
3. Itangaze chanjo kuwa lazima
4. Vyama vya upinzani vishirikishe hatua kwa hatua ilikuleta umoja katika kupambana na hili janga.

ÑB: Clip za Gwajima zinauzwa na warusha movie tsh 300 na unaambiwa mauzo ni makubwa. Jana kwenye kijiwe cha chai tuliwekewa hiyo video mpaka watu wakasahau kuangalia movie.
 
Mama samia amethibitisha bayana kwamba mwanamke hawezi kuongoza hii nchi, taifa linapiga kampeni ya chanjo, halafu anasimama mtu mmoja kwa dharau na kiburi cha kupitiliza nae anapiga kampeni ya kupinga chanjo tena anatamka hadharani kwamba viongozi wanaopigia debe chanjo akili wameziweka likizo.

yeye Rais na Amiri jeahi mkuu ametulia tu sijui ni uoga sijui ni kutokujitambua, yani simuelewi kabisa
 
Mama samia amethibitisha bayana kwamba mwanamke hawezi kuongoza hii nchi, taifa linapiga kampeni ya chanjo, halafu anasimama mtu mmoja kwa dharau na kiburi cha kupitiliza nae anapiga kampeni ya kupinga chanjo tena anatamka hadharani kwamba viongozi wanaopigia debe chanjo akili wameziweka likizo,

yeye Rais na Amiri jeahi mkuu ametulia tu sijui ni uoga sijui ni kutokujitambua , yani simuelewi kabisa
We jamaa ungekuwa hata tu Waziri mkuu ungekuwa dikteta zaidi ya Hitler au Mussolini.

Mama Samia yuko sahihi kuwaacha watu waongelee mambo haya ikiwemo chanjo. Amiri Jeshi mkuu anapaswa kuwa na ngozi ngumu maana maamuzi yake yanaweza leta madhara makubwa. Kiufupi hufai hata kuongoza kijiji, sijui hata ubavu wa kumshauri mtu mzito kama CiC unaupata wapi?

Rais sio muoga wala sio kwamba hajitambui. Watu wasiojitambua kama wewe ndio mnamuona hivyo.

By the way kama wanaokataa chanjo wana sababu za kijinga na zisizo na mashiko, mbona sasa unataka kuwanyamazisha? Si uwaache watu wachambue mchele na pumba? Au una maana Watanzania ni vilaza plus na hawana akili hata chembe ya kujua mpaka wapate handlers kama wewe?

Shame on you dictator!
 
Mama samia amethibitisha bayana kwamba mwanamke hawezi kuongoza hii nchi, taifa linapiga kampeni ya chanjo, halafu anasimama mtu mmoja kwa dharau na kiburi cha kupitiliza nae anapiga kampeni ya kupinga chanjo tena anatamka hadharani kwamba viongozi wanaopigia debe chanjo akili wameziweka likizo,

yeye Rais na Amiri jeahi mkuu ametulia tu sijui ni uoga sijui ni kutokujitambua , yani simuelewi kabisa
Msimlaumu Mh. Rais, wapambe ndiyo mlioharibu kwa ushabiki wenu badala ya kutumia weledi. Mambo ya maisha ya mtu na ahasa kama kuna imani ndani yake ni vigumu mno kuyalazimisha. Na hii haitokei hapa tu kusema eti kwakua ni mwananmke labda kama mna agenda ya siri. Vipi kuhusu huko kwingine wanakokataa kuchanjwa viongozi ni wanawake?

Acheni hujuma, tuisaidie nchi yetu kusimama!
 
2. SerikaLi imuombe Gwajima abaki na msimamo wake lakini asiongelee chanjo
3. Itangaze chanjo kuwa lazima
1. Badala ya kumwomba asiongelee chanjo, serikali inatakiwa ijibu hoja zake (mf. Madhara ya muda mrefu ya hizo chanjo ni nini?) Kisayansi. Kumfumba mtu mdomo kwa vitisho siyo solution nzuri ya tatizo.

2. Nchi zote zinazotambua uhuru na haki za binadamu hakuna hata moja ambayo imefanya chanjo kuwa ya lazima.
 
We jamaa ungekuwa hata tu Waziri mkuu ungekuwa dikteta zaidi ya Hitler au Mussolini.
Mama Samia yuko sahihi kuwaacha watu waongelee mambo haya ikiwemo chanjo. Amiri Jeshi mkuu anapaswa kuwa na ngozi ngumu maana maamuzi yake yanaweza leta madhara makubwa. Kiufupi hufai hata kuongoza kijiji, sijui hata ubavu wa kumshauri mtu mzito kama CiC unaupata wapi?

Rais sio muoga wala sio kwamba hajitambui. Watu wasiojitambua kama wewe ndio mnamuona hivyo.

By the way kama wanaokataa chanjo wana sababu za kijinga na zisizo na mashiko, mbona sasa unataka kuwanyamazisha? Si uwaache watu wachambue mchele na pumba? Au una maana Watanzania ni vilaza plus na hawana akili hata chembe ya kujua mpaka wapate handlers kama wewe?

Shame on you dictator!
vipi kuhusu Magufuli alikua dikteta au sio dikteta?
 
Mama samia amethibitisha bayana kwamba mwanamke hawezi kuongoza hii nchi, taifa linapiga kampeni ya chanjo, halafu anasimama mtu mmoja kwa dharau na kiburi cha kupitiliza nae anapiga kampeni ya kupinga chanjo tena anatamka hadharani kwamba viongozi wanaopigia debe chanjo akili wameziweka likizo,

yeye Rais na Amiri jeahi mkuu ametulia tu sijui ni uoga sijui ni kutokujitambua , yani simuelewi kabisa
mara nyingi tu wewe jamaa una Ngebe
hivi hujawahi kukutana na sauti za mbwa wakibweka hata kunapopambazuka?
ukisikiliza milio ya mijibwa wala hutafika kazini kwa muda utaliwao
na ukianza kuwajibu hata kwa kushika kiboko ndio sauti zitazidi
huyo Gwajima mnamjua wenyewe kwanini hakumuombea mwendazake asife na Corona, mpaka Masheikh wakamfuata wodini yeye alikuwa wapi mpaka leo ndio apinge?
Kumjibu Gwajima ni kumuongezea misifa acha abaki na walokole wenzake, wakati wameonyeshwa blue print wanamtetea leo COVID 19 wanamtetea hata KIBWETERE alifanikiwa vivi hivi
 
Jana nilimskiliza tena askofu Gwajima! Matamshi yake yanaungwa mkono na watu wengi sana kuliko hata watu waliopewa ubalozi wa Corona. Nashauri yafuatayo:

1. Serikali iongeze elimu juu ya chanjo
2. SerikaLi imuombe Gwajima abaki na msimamo wake lakini asiongelee chanjo
3. Itangaze chanjo kuwa lazima
4. Vyama vya upinzani vishirikishe hatua kwa hatua ilikuleta umoja katika kupambana na hili janga.

ÑB: Clip za Gwajima zinauzwa na warusha movie tsh 300 na unaambiwa mauzo ni makubwa. Jana kwenye kijiwe cha chai tuliwekewa hiyo video mpaka watu wakasahau kuangalia movie.
Shida kubwa kwenye hii issue ilianzia kwa serikali hiyo hiyo na viongozi hao hao kuwaaminisha wananchi kwamba chanjo hazifai kabisa na ni mbinu za wazungu kuwadhuru wamatumbi. Pia wanaenda mbali kuwaaminisha wananchi kwamba ufumbuzi na tiba pekee ya korona ni maombi na kujifukiza (rejea mpaka kujengwa mtambo wa kujifukiza pale Muhimbili na mawaziri kujifukiza na kupost picha), matokeo yake wananchi wakawaamini. Sasa ghafla bin vuu wamepiga U turn hapo unatarajia nini??
 
Serikali haina haki ya kumlazimisha mtu kuchanjwa. Huwezi lazimisha kumtibu mtu. It's unethical bhana.
Hulazimishwi, lakini hiyo hiari yako usiitumie vibaya kuwaambukiza wengine. Ukiwa kwenye public places au transport vaa barakoa, hutaki unashushwa, kwenye mikusanyiko yote vaa barakoa na tahadhari nyingine. Sasa haiwezekani kuchanjwa hutaki na pia kuchukua tahadhari hutaki.
 
Jana nilimskiliza tena askofu Gwajima! Matamshi yake yanaungwa mkono na watu wengi sana kuliko hata watu waliopewa ubalozi wa Corona. Nashauri yafuatayo:

1. Serikali iongeze elimu juu ya chanjo
2. SerikaLi imuombe Gwajima abaki na msimamo wake lakini asiongelee chanjo
3. Itangaze chanjo kuwa lazima
4. Vyama vya upinzani vishirikishe hatua kwa hatua ilikuleta umoja katika kupambana na hili janga.

ÑB: Clip za Gwajima zinauzwa na warusha movie tsh 300 na unaambiwa mauzo ni makubwa. Jana kwenye kijiwe cha chai tuliwekewa hiyo video mpaka watu wakasahau kuangalia movie.
Serikali ingetoa tamko moja tu,kuwa Kama hujachanja na ikatokea ukaumwa Corona Basi hakuna hospitali itakayokupokea.Watu wangechagua wenyewe.Sema Gwajima Kuna sehemu anaisitiri serikali chanjo milioni moja Ni kidogo mno
 
Serikali ingetoa tamko moja tu,kuwa Kama hujachanja na ikatokea ukaumwa Corona Basi hakuna hospitali itakayokupokea.Watu wangechagua wenyewe.Sema Gwajima Kuna sehemu anaisitiri serikali chanjo milioni moja Ni kidogo mno
Dikteta mwingine huyu hapa. Yaani nyie jamaa mnacheckesha sana. Huu udikteta wenu unawatia shaka hata wenye nia ya kuchanja. Wanajiuliza sana mbona mnalazimisha sana?

Ishauri na serikali iache kukusanya kodi kwa wale ambao hawajachanja. Hizo hospitali unazosema wazuiliwe ni kodi zao. Mbona mnawaza kama kuku aliyekatwa kichwa? Yaani mpaka watu wenye akili timamu kwenye hili wamekosa utashi kabisa.

Inasikitisha!
 
Kwa ufupi Gwajima is winning na mbaya zaidi hakuna anaye challenge hoja zake.

No need. Chanjo ni hiari: anayetaka anachanja; asiyetaka anapuuza (ignore). Hakuna cha kujadiliana. It’s a non-issue.

Hakuna challenge kwa watu wanaolumbana toka sakafu tofauti (different premises). Scientific analysis na conspiracy theorizing ni dunia tofauti kabisa.
 
1. Badala ya kumwomba asiongelee chanjo, serikali inatakiwa ijibu hoja zake (mf. Madhara ya muda mrefu ya hizo chanjo ni nini?) Kisayansi. Kumfumba mtu mdomo kwa vitisho siyo solution nzuri ya tatizo.
2. Nchi zote zinazotambua uhuru na haki za binadamu hakuna hata moja ambayo imefanya chanjo kuwa ya lazima.
Namba 2 serikali imeanza kuifanyia kazi kupitia naibu waziri
 
Back
Top Bottom