#COVID19 Serikali yawaonya wanaojipatia vyeti feki vya chanjo ya Corona

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,209
42,071
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Bwana Abel Makubi amesema kumeanza kujitokeza vitendo vya kujipatia vyeti feki vya chanjo ya Covid-19 hivyo amewaomba wananchi kuwa wasijaribu kujiingiza kwenye mkenge wa kujipatia vyeti feki vya Covid-19.

Katibu Mkuu amesisitiza kuwa kuwa Wizara ya Afya ndio pekee inatoa vyeti vya chanjo ya Covid-19 na kwa sasa iko kwenye mchakato wa kuandaa vyeti vya wote waliopata chanjo hivyo wasidanganywe kupata vyeti feki

Na pia ameendelea kuwaonya watu wote ambao hawajachanjwa chanjo ya Corona wasiendelee na mipango ya kujipatia vyeti feki vya chanjo kwani wakibainika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Chanzo: Magazeti

My take:

Katika hili Wizara ya Afya inatakiwa kuwajibika kabisa kwenye huu uzembe unaopelekea watu kuanza udanganyifu kwani walitakiwa kujiandaa kabisa kabla ya kuletwa chanjo , inakuwaje watu wachanjwe halafu wasubiri vyeti?

Kwanini mfumo ule wa utoaji wa vitambulisho vya kupigia kura usingelitumika? Kwanini tusiseme hii ni hujuma? Kweli Waziri na Katibu wake wako makini kweli?
 
Ngoja ninywe malimao na matangawizi nyungu mpaka jionii
 
Kitu kama hakikubaliki shida yake ndio hiyo

Hiyo ni signal kuwa watu hawataki chanjo ila serikali ndio inataka chanjo!!!!! Ilitakiwa watu waitake ndio serikali iitake!!! Demand ilitakiwa kuanzia kwa wananchi sio serikalini!!!

Hii chanjo ya kwetu kituko serikali ndio ina high demand ya chanjo !!!! ha ha ha ha


Lakini kwenye hili la chanjo ni opposite serikali ndio inataka wakati wananchi hawataki!!!!
 
Udanganyifu na uongo ni kawaida na hao hao wanaopiga kelele ndio wa kwanza kutoa hivyo vyeti feki

Nchi masikini kama kuuwa unatoka itakuwa kacheti
Kama hawakujipanga mwanzo imekula kwao
 
Wizara ya Afya walikosea, hao wanaojipatia vyeti feki wanavitumia kwenye mambo yao muhimu ikiwemo kusafiria nje ya nchi kwa kazi zao kama kigezo cha kuruhusiwa kukaa waendako, sasa kuwachanja watu halafu hawapewi vyeti walitaka wakaoneshe makovu ya sindano ya chanjo ubalozini?
 
Are you sure??
Chanjo ilitakiwa kuwa kilio cha wananchi kuwa jamani tunaomba mtuletee chanjo ndipo serikali ingechukua hatua isingekuwa shida chanjo kukubalika

Lakini kwa sasa watungua kilio wakubwa ni viongozi wa serikali kuwa chanjo inahitajika chanjo chanjo chanjo!!! Demand ya chanjo kubwa serikalini kuliko mitaani na vijijini !!! hii ni paradox!!! ilitakiwa kuwa kinyume chake lakini Tanzania serikali ndio muhitaji mkuu wa chanjo!!
 
Vyeti vya nini? Yaani serikali iliyo na wataalamu wa IT imeshindwa kutengeneza data base inayoonyesha Name, ID/Paassport ukifanya scan kwa simu yako basi inaonyesha "Inoculated" very simple. Hivi tupo wajima kiasi gani hii nchi??
 
Wizara ya afya ni wazembe, watu wanataka vyeti ili waendelee na safari zao, wao wanapiga porojo tu hadi sasa vyeti bado, hizi ndio mambo ambazo Magu alikuwa lazima apige watu chini ili akili zije.
 
Kitu kama hakikubaliki shida yake ndio hiyo

Hiyo ni signal kuwa watu hawataki chanjo ila serikali ndio inataka chanjo!!!!! Ilitakiwa watu waitake ndio serikali iitake!!! Demand ilitakiwa kuanzia kwa wananchi sio serikalini!...
Leo umeipinga serikali.

Watu watachanjwa sababu ya huduma tu,na sio kwa ajiri ya corona.

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Serikali kupitia Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Bwana Abel Makubi amesema kumeanza kujitokeza vitendo vya kujipatia vyeti feki vya chanjo ya Covid-19 hivyo amewaomba wananchi kuwa wasijaribu kujiingiza kwenye mkenge wa kujipatia vyeti feki vya Covid-19...
Kabisa hili nimeliona Temeke hospital, eti unachanjwa unasubiri vyeti, hii si ni njia ya kuleta udanganyifu?
 
Wizara ya afya ni wazembe, watu wanataka vyeti ili waendelee na safari zao, wao wanapiga porojo tu hadi sasa vyeti bado, hizi ndio mambo ambazo Magu alikuwa lazima apige watu chini ili akili zije.
hiiii ndio tatizo yani mtu achanjwwe halafu akae tuu akisubiri likaratasi aisee
 
Back
Top Bottom