Serikali impe angalizo Jerry Silaa, namuona anaiingiza Serikali katika mgogoro mkubwa wa kulipa fidia!

Ni waziri wa ardhi.
Alichofanya ni sahihi.
Mkuu najua wewe ni mtu wa details. Hebu tupe snapshot ya kilichotokea. Kwangu mimi waziri kama kiongozi mkubwa wa serikaki ni muhimu kufuata sheria. Inawezekana mahakama zetu zina mapungufu mengi. Lakini ndo chombo tulichonacho.
Tukiamua kuignore maamuzi ya mahakama, it will be anarchy.
 
Leo katika taarifa ya habari ya ITV nimemuona Jerry Silaa akisimamia kubomoa ghorofa, na bila shaka kwa kujifanya yeye ni hakimu au Jaji mwenye uamuzi wa mwisho, kwa nini asishauri watu wafuate mlolongo wa mahakama ambao unasikiliza pande zote na kutoa haki ya rufaa ya ngazi tofauti? Kwa nini asiache tafsiri ya mwisho ya haki ifanywe na mahakama kabla ya mtu yoyote kuingizwa kwenye hasara?

Hofu kubwa ni kwamba haya mambo anayafanya Dar es salaam kwa kusaidia watu ambao mi marafiki zake, au marafiki wa familia yake. Ukikutana na family friend wa Silaa, na kimsingi wanamzonga sana pale ofisini watumie fursa kabla hajatenguliwa, ujue lazima atavuruga kila kitu ili kwemye vikao vya ukoo au harusi akasifiwe. Imagine Waziri mzima anatembea mpaka kwako na mmoja wa watu waliolalamika, yule anayelalamikiwa yuko na nani? Na ameshamumini anayekulalamikia, kamkodia mpaka greda, sijui kwa hela za serikali au kamshawishi akodi! utamwambia nini akuelewe?

Ajiepusha kuiweka serikali mbele katika kila tukio, aache sheria ichukue mkondo, akiwa waziri wa ardhi, miaka kumi serikali italipa fidia za trilioni na zaidi.

Nina imani haya mambo ya hovyo anayafanya bila kuhusisha ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, angewahusisha wangemkatalia maana wao ndio wanajua vita ya mahakamani ikoje, yeye atafanya upuuzi wake, atatenguliwa, na anatuachia hasara kubwa ya kulipa fidia.


Mawaziri wapya watoto watoto wasipewe wizara nzito kama ardhi. Waziri badala ya kushughulikia sera za kitaifa, anazurura mitaani ambako tayari ana maafisa ardhi. Mchi hii ina mitaa mingapi? Kama sera ina shida kutatua migogoro ya ngazi hizo, yeye kama waziri kaliambia nini Bunge limtungie sheria kutengeneza mfumo imara wa watu wa ardhi kuwa na mawasiliano na wateja wao? Atafika lini Chankende kutatua mgogoro?

Wazara yake inatoa hati, baadae inaikataa hati moja,inaikubali nyingine, halafu yuleyule waliyempa hati na kibali cha ujenzi, wao wenyewe wanaenda kumvujia walichomruhusu ajenge!
Halafu hizi taratibu za kuvunja, si ustaarabu na ni kinyume cha ubinadamu. Pakiwa na mgogoro, thamani ya uwekezaji/uendelezaji haionekani bali pande la ardhi tu! Na kitendo cha Waziri kusimamia zoezi, kimeshusha kiwango chake cha uwajibikaji..!!!
 
Kama issue ni hivyo si wanaweza kukutengenezea hati wakabackdate documents zote ili uonekane ni wa kwanza?

Haiwezekani.

Hati na offer letter huwa zinabadilika badilika kutokana na teknolojia.

Mfano hati na ofa za miaka ya 80 na 90 zimeandikwa kwa type writer na karatasi zake za kizamani sio rangi nyeupe. Na mafaili yake yapo wizara ya ardhi. Siku hizi mafaili yanakaa manispaa. Leo hii unatoa wapi type writer ama karatasi kama zile.

Pili waliokuwa wanasaini wote wameshastaafu na wengi kufariki. Unazitoa wapi sahihi zao. Maana ukirudisha siku nyuma back date lazima uwafufue na wafanyakazi waliokuwepo hizo tarehe za nyuma

Utajulikana tu umefoji
 
Anajitahidi kutenda kwa haki.

Vibaya kumuonea mtu lakini tabia ya kuvamia maeneo ya watu na janja janja kisha kujenga Halafu utake huruma wakati umedhurumu haki ya mtu mwingine haikubaliki.
Wengi wanaopiga makelele ni madalali wa hao wa matapeli waliokubuhu wanaotesa watu kwa kupora maeneo yao.

Yule Mzee Mushi anaambiwa aweke document angalau moja tu ya halali anajiumauma, watu mfano wake ni wa kushughulikiwa mara moja.
 
Tuache ushaabiki maandazi, mimi siyo muumini wa kuonewa au kuona mtu anamuonea mwenzie. Huyu Slaa sidhani km ni kichaa hadi asimamie zoezi Hilo bila kibali cha mahakama. Tangu wanaanza kubomoa ni nani alimskia yule mama akisema alishinda kesi mahakamani.

Tunaambiwa kesi imedumu mahakani kwa miaka 20, unadhani ni kitu gani kilichelewesha hukumu hadi ije iwe leo. Watu wenye vijisent wawe na tabia ya kuheshimu watu masikini kwani "haki ya mtu huwa haipotei bali hucheleweshwa tu". Zoezi liliosimamiwa na askari police tena wengine wa vyeo vya juuu mtu anakuja kusema ni mambo ya family friends eti kwamba huyo mama kaonewa. Guys "kitanda usichokilalia huwezi kujua kunguni wake", vipi huyo mama mjane aliekuwa amedhulumiwa kiwanja ndo angekuwa MAMA yako huku mkiishi upangajini kwa tabu.

Mimi ninaamini kilichofanyika ni matokeo ya maamuzi ya mahakama na siyo blaa blaa za mleta mada, km kaonewa bado nafasi anayo ya kwenda mahakamani.

Said: BANDOKITITA
 
Halafu hizi taratibu za kuvunja, si ustaarabu na ni kinyume cha ubinadamu. Pakiwa na mgogoro, thamani ya uwekezaji/uendelezaji haionekani bali pande la ardhi tu! Na kitendo cha Waziri kusimamia zoezi, kimeshusha kiwango chake cha uwajibikaji..!!!
Uwekezaji wa wizi na dhulma! Shithole!
 
Rushwa, Rushwa, Rushwa
Ikiwezekana waziri aamuru takukuru wapitie Hilo sakata from the beginning na wote waliohusika wawajibishwe
 
Halafu hizi taratibu za kuvunja, si ustaarabu na ni kinyume cha ubinadamu. Pakiwa na mgogoro, thamani ya uwekezaji/uendelezaji haionekani bali pande la ardhi tu! Na kitendo cha Waziri kusimamia zoezi, kimeshusha kiwango chake cha uwajibikaji..!!!
Hujawahi kuvamiwa wewe na usiombe. Matapeli yanavamia ardhi halafu yanaweka hapo uwekezaji mkubwa sana Ili tu mwenye uhalali wa kiwanja asiweze kurudi kabisa... Kuna kesi Moja huko kariakoo judge alimkomesha S.H.Amon aliamuru ardhi na kilichopo juu yake ni Mali ya mwenye ardhi halali... Sijui waliishia wapi lakini S.H.Amon alipoteza jengo
Usiangalie tu thamani ya uwekezaji uliofanywa na mvamizi, angalia usumbufu naufa na fedheha alizosababbishiwa mmiliki halali
 
Nimemuonesha hapo KESI TATU zinazomhusu huyo kiumbe anayemtetea na zote ni za ardhi, na hizo ni zile zilizo kwenye public domain tu. Sasa by total sijui atakuwa na kesi ngapi.
Kibaka akiiba mnamvisha taili anamwagiwa mafuta mnamuua. Je vipi mtu kama Mahururu ambaye ameumiza familia mbili ( mwenye kiwanja halisi na mwenye ghorofa)? Mahururu anapaswa kushughulikiwa. Tunaomba serikali ishughulikie Mahururu yeye ni sehemu ya mizizi ya tatizo.
 
Tuache ushaabiki maandazi, mimi siyo muumini wa kuonewa au kuona mtu anamuonea mwenzie. Huyu Slaa sidhani km ni kichaa hadi asimamie zoezi Hilo bila kibali cha mahakama. Tangu wanaanza kubomoa ni nani alimskia yule mama akisema alishinda kesi mahakamani.

Tunaambiwa kesi imedumu mahakani kwa miaka 20, unadhani ni kitu gani kilichelewesha hukumu hadi ije iwe leo. Watu wenye vijisent wawe na tabia ya kuheshimu watu masikini kwani "haki ya mtu huwa haipotei bali hucheleweshwa tu". Zoezi liliosimamiwa na askari police tena wengine wa vyeo vya juuu mtu anakuja kusema ni mambo ya family friends eti kwamba huyo mama kaonewa. Guys "kitanda usichokilalia huwezi kujua kunguni wake", vipi huyo mama mjane aliekuwa amedhulumiwa kiwanja ndo angekuwa MAMA yako huku mkiishi upangajini kwa tabu.

Mimi ninaamini kilichofanyika ni matokeo ya maamuzi ya mahakama na siyo blaa blaa za mleta mada, km kaonewa bado nafasi anayo ya kwenda mahakamani.

Said: BANDOKITITA
Kama sikosei, hii kesi huyo aliyevunjiwa alishinda kesi na eneo lipo kilonga wima Mbezi Beach.
Jambo la busara ni serikali kukataa rufaa na sio kutumia mabavu.
 
Kiwanda Cha bakhresa kilitaka kubomolewa watu na mashine vikiwa ndani na hajashitaki, sembuse hao wavamizi. Labda walipewa muda wa kubomoa wenyewe wakaghairi
 
Back
Top Bottom