- Thread starter
- #61
nyiue watu nyie TBC iko DSTV free of charge tena serekali ndio ili walazimisha kwamba TV ya taifa ni sharti iwe bure haya ni maelezo kwa mujibu wa TCRA wenyewe,swala la private TV station kama itv,channel 10 star tv ni ziwepo DSTV sio swala la TCRA hilo ni swala la kibiashara kati ya wamiliki wa vyombo hvi na DSTV ingekuwa itv ni tv ya taifa nayo unge iona DSTV,so kama mtu una taka itv DSTV nenda kaonge na mzee Mengi wafanye makubaliano na dstv wajuane watakatana shilling ngapi kujumlisha itv katika list zao.pia ikumbukwe DSTV ime pewa leseni ya kibiashara hawawezi tu amua kuweka channel za mfanya biashara mwingine kwa bure kwenye channel zao.swala la dollar nadhni ndilo la kulipigia kelele
Mkuu maelezo yako nimeyapata vizuri. Nadhani uneeleza Ukweli na hali halisi on the ground.
Kwa upande wa malipo makubwa yanayotozwa na multichoice pamoja na kwamba ni hiari kupata service Multichoice wanalo jukumu la kupunguza hii gharama lakini TCRA pia wana jukumu la kulinda haki za watumiaji kama wanavyofanya kwenye mitandao ya Simu.
Vile vile TCRA au serikali kupitia wizara husika wana jukumu la kuhakikisha ushindani wa haki kati ya makampuni yanayotoa huduma za tv kwa kuondoa vipengele vinavyoifanya Multichoice kuwa na monopoly Au exclusive right ya Chanel za kimataifa inazozirusha. Pamoja na ubora wa matangazo yao nadhani hili nalo linawafanya wawe na bei za kiburi.
Kwa upande wa Chanel za kitaifa (ingawa si chanel za taifa) nakubaliana na wewe kwamba ili kuingizwa DSTV itategemea sana negotiation ya makambuni husika na Multichoice. Lakini vile vile naamini itakuwa ni faida kwa Multichoice wakiingiza hizi Chanel Na kufanya bei yao iwe reasonable. Kwa kufanya hivi watanzania wengi wataweza kujiunga na watapata faida zaidi.