Angeweza kama angekuwa nje wa mfumo wa kifisadi wa CCM.
Ni kweli tuna vijana wazuri kama kina January Makamba lakini wanaharibiwa na mfumo.
Hivi WAKUU mna matumaini gani na huyu January Makamba? Hivi lini Shetani akazaa Malaika? Huyu ni zao la Kifisadi na atadumu hivyo!!! Si tuliletewa nakala kivuli hapa jamvini ya dada yake kuomba pesa kwenye makampuni ya madini ili ndugu yake atumie kupata ubunge? Mbona mnasahau wkuu? Sasa katika hali hiyo unategemea atapata wapi ujasiri wa kuwatetea WaTanganyika mbele ya waliyo mwezesha kupata ubunge? Yeye atakuwa mtumwa wao milele.
Tumefika hapa tulipo, na tutaendelea kuumizwa na wanao itwa wawekezaji hadi pale tutakapo amka na kujua haki zetu. Tufike mahala tukatae kunyonywa na hao wanao itwa WAKWAPUAJI. Tuna viongozi wasio na uwezo. Wamepewa uongozi kama fadhila, hivyo wanaogopa kupingana na masilahi ya walio weka madarakani.
Hakuna cha mfumo wala nini. Kilichopo mbele yetu ni Uongozi wa maslahi binafsi. Mbona kina Mwakyembe wanachanja mbuga ki ukweli, si wapo kwenye mfumo wa CCM?
Tuamke waDanganyika saa ya ukombozi ni sasa, na tuache kulalama bila kuchukua hatua.
Mimi sio kwamba sina uwezo wa ku-join DsTv (ninao). Lakini kwa kutambua unyonyaji huu, nimeamua kuwa mmoja kaiti ya walio amua kukataa unyonyaji wa hali ya juu wa aina hii: Amua sasa na ikatae DsTv kama una uchungu na pesa yako. Vinginevyo endelea kuliwa.