Serikali imeiuza Kariakoo kwa Wachina

Serikali imeiuza Kariakoo kwa Wachina

Na hii ndio legacy ya ujamaa, kitu pekee mtanzania anaweza ni propaganda. Kwasasa ni muache ulanguzi au mkubali kufa kifo cha mende

Nyuzi nyingi sana humu Jf zipo tangu kitambo mkionywa upumbavu wa kutaka mpaka faida zaidi ya 100% mkapofusha macho na kuziba masikio.

Wakati umewadia kushare kile kikombe mlichokuwa mnatunywesha nacho maji, serikali wasikilizie hata miaka mitano ijayo then wawapige ban wachina maana mpaka wakati huo vichwa vyenu vitakuwa vimerudi kwenye default settings
Mwafrika anafurahia anguko la mwafrika wenzake
 
Nenda kwa wenzetu, hakuna ujinga huu
Kwa yanayotokea kwa Mzee Trump...binadamu wote ni Sawa Tu! Watu wanakula pesa za marehemu, Watu wanapewa pesa kuandamana kama CCM wanavyotoa tisheti na kofia tupige Kura, Watumishi hewa nao wamo kama kwetu Tu,

Neno "wenzetu" nimelifuta rasmi...wajinga wanaopatikana hapa hapa na Ulaya, Marekani, wapo
 
Haiwezekani Kariakoo wachina wanaishi kama kwao.

Mbaya zaidi hawalipi kodi ipasavyo. TRA haina kanuni za asiye raia kulipa kodi kama mzawa

Hii ni sawa tu na kusema Kariakoo imeuzwa
Wazawa tuache ghubu. Wachina ni msaada Sana kwetu
 
Mawinga wamefikiwa, bado madalali wa magari na nyumba, wachina waonyeshwe hiyo fursa.
Unahangaika na mawinga ambao ni wabangaizaji unashindwa kuumia watu wanavuna mabilion ila mwafrika kifikra anasafari ndefu sana

Hao unaowaita madalali, na mawinga wengi e ni ndugu zetu, majirani, na ukipata shida ndo watakaokusaidia na sio mchina ebu tupendane waafrika
 
Unahangaika na mawinga ambao ni wabangaizaji unashindwa kuumia watu wanavuna mabilion ila mwafrika kifikra anasafari ndefu sana

Hao unaowaita madalali, na mawinga wengi e ni ndugu zetu, majirani, na ukipata shida ndo watakaokusaidia na sio mchina ebu tupendane waafrika
Mpaka uuziwe gari ya wizi, upangishiwe nyumba iliyokwishalipiwa na mwingine au yenye mwenye nyumba feki, uuziwe kiwanja cha manispaa au uuziwe simu feki kariakoo kwa bei kubwa ndo utaelewa kwanini madalali na mawinga watanzania wenzao wanaona bora wachina. Unless wewe ni dalali au winga ndo hutoelewa hichi kilio cha watanzania wenzako.
 
Mpaka uuziwe gari ya wizi, upangishiwe nyumba iliyokwishalipiwa na mwingine au yenye mwenye nyumba feki, uuziwe kiwanja cha manispaa au uuziwe simu feki kariakoo kwa bei kubwa ndo utaelewa kwanini madalali na mawinga watanzania wenzao wanaona bora wachina. Unless wewe ni dalali au winga ndo hutoelewa hichi kilio cha watanzania wenzako.
Mwafrika anaombea mabaya kwa mwafrika mwenzake alafu unajiona unaakili kwa akili hizi tunasafari ndefu sana

Sio kweli eti madalali wote ni wabaya wako wazuri alafu sio kila mtu anamda wa kwenda kuzurura kariakoo wengine mda hawana kwa hiyo wanatumia mawinga

Ukishaona unalalamikia mawinga fahamu kipato chako ni kidogo pambana uongoze kipato
 
Mwafrika anaombea mabaya kwa mwafrika mwenzake alafu unajiona unaakili kwa akili hizi tunasafari ndefu sana

Sio kweli eti madalali wote ni wabaya wako wazuri alafu sio kila mtu anamda wa kwenda kuzurura kariakoo wengine mda hawana kwa hiyo wanatumia mawinga

Ukishaona unalalamikia mawinga fahamu kipato chako ni kidogo pambana uongoze kipato
Fikiri kabla ya kuandika boss, huwezi halalisha malalamiko kwa mawinga kwa hoja ya kipato. Watanzania wengi ni wenye kipato kidogo na cha chini.

Swali la kujiuliza kwanini Watanzania wakanunue kwa wachina badala ya mawinga?
 
Hao wabishi achana nao, na wanadhani hawatofikiwa.

Aya sasa Mchina ananunua ardhi yenye madini uko Chunya na maeneo mengine, Mchina ana makarasha na miundombinu ya kuchimba anabeba dhahabu ya wazawa ambayo ina soko regulated duniani na bei ni soko la dunia. Napo utaambiwa wachimbaji wa Kitanzania wanataka faida kubwa.

Ukienda mikoa kama Katavi unakuta Wachina wanamiliki ardhi ya kilimo, wamepataje hujui. Wanavijiji wanambulia kuwa watumwa kwenye ardhi zao.

Nina jamaa yangu aliajiriwa nao mradi fulani, wakampeleka short course, sasahivi wamesajili kampuni kupitia wabongo wawili na terms ngumu wamewapa. Yupo front kama geresha operations ni wao wanashusha makontena.

Ubaya wa Wachina wanakomba hela kwenye mzunguko na hawana settlement ya kudumu hapa. Bora hata Wahindi na Waarabu kwa kiasi fulani tunao makumi elfu mitaani, Wachina wakipata hela yote wanatuma kwao na miaka kadhaa wanarudi kwahiyo hatupati re-investment ya ile faida yao.
Wachina wako sahihi sana! Ni lazima wasake fursa kokote duniani Kwa ajili kulijenga taifa lao la china ili liwe super power, na kurithisha vizazi vyao uchumi wa uhakika! Watanzania mnapoambiwa chagueni visionary leaders na wenye wivu na taifa lao mmekalia uchawa na mapambio, ktk zama hizi ambazo vita ya kiuchumi inapiganwa Kwa ustadi na werevu wa hali ya juu tunapaswa tuwe na viongozi smart sana! Wenye upeo wa juu, maono na wivu Kwa taifa! Madhara ndio haya sasa watu kubaki kulia lia na hata viongozi wenu hawana namna ya kuwafukuza maana hao wanaabudiwa kama wawekezaji. Kimewaramba!
 
Fikiri kabla ya kuandika boss, huwezi halalisha malalamiko kwa mawinga kwa hoja ya kipato. Watanzania wengi ni wenye kipato kidogo na cha chini.

Swali la kujiuliza kwanini Watanzania wakanunue kwa wachina badala ya mawinga?
We unaona tatizo ni mawinga mtu ambaye anabangaiza na kukaa hata week hajauza hata Mia mtu ambaye akiumwa hangizi hata Mia

Mawinga wengi wanamaisha magumu kuwatupia lawama ni kuwaonea wale ni wabangaizaji
 
Wachina ni janga kubwa sana Serikali inabidi ichukue hatua haraka sana hasa kokote kule kwenye wachina Kariakoo, pale Ubungo jengo kubwa jipya, hawa wachina ni watu hatari sana na wataua uchumi wa nchi yetu na wananchi kupoteza biashara zao..!! Kuna wachina pia walitoka Mombasa wako Dar, wanajenga majengo, ni hatari sana, pia TIC waangalie wawekezaji wa kichina ni wahuni kwani anakuja mmoja ana dollar say $100,000 anajisajili mmoja kama investor kumbe wako wachina 100 ndio wamejichangisha..

Wachina wachukuliwe ni hatari kubwa kama Corona kwa uchumi wa nchi yetu, wachina wote Serikali iwafuatilie, iwe kama janga la Taifa, hasa Kkoo itapotea kabisa na wananchi wetu watapoteza biashara zote.
Mkuu Serikali ya awamu ya sita na ile ya awamu ya 4 zote zimeungana zimekua awamu moja zinashirikiana na Wachina kuibomoa nchi, Serikali ya awamu ya 4 ilikua inawashtaki wa China kwa kuhujumu uchumi leo hii serikali inashrikiana nao,we nenda uko Mikoani Maeneo yote ya Migodi midogo midogo wamepewa Wachina, Mara mia Uchumi wetu ushikwe na Mabepali kuliko awa Masikini wenzetu.
 
We unaona tatizo ni mawinga mtu ambaye anabangaiza na kukaa hata week hajauza hata Mia mtu ambaye akiumwa hangizi hata Mia

Mawinga wengi wanamaisha magumu kuwatupia lawama ni kuwaonea wale ni wabangaizaji
Huwezi halalisha tatizo kwa hoja ya ubangaizaji, vibaka na wakabaji ni wabangaizaji pia.

Mawinga wengi wanajichafua wenyewe sababu ya tamaa ya kuwaibia wanaoitwa washamba. Kariakoo si salama kwa wateja wasiopaelewa sababu ya mawinga, vibaka na wezi.
 
Mnaolialia ni wachache ni nyie wafanyabiashara msiotaka ushindani sisi wateja tunafurahi sana maana bidhaa ni nyingi bei cheeee wachina wangeruhusiwa wawe wengi zaidi ikiwezekana asiwepo hata mbongo mmoja kariakoo badala ya kushindana mnataka serikali iwalinde na utapeli wenu sina hamu na nyie wafanyabiara wa kariakoo
 
Back
Top Bottom