Serikali imeiuza Kariakoo kwa Wachina

Serikali imeiuza Kariakoo kwa Wachina

Wafanya biashara wa kibongo ni wahuni bidhaa ya 12k unauziwa 35k. Risiti hawatoi na hata wakitoa ni za magumashi Acha wachina watupe unafuu ya maisha. Tumechoka na mawinga wa kariakoo
Kama hujui wachina ndiyo mabingwa wa kutolipa ushuru ndugu, wamenunua Mahoteli kibao na kujaza shehena zao huko na wanauza kimaghumashi.
 
Wachina wako kwenye Cartels😁 yani ukimtingisha ana Godfather wake ambaye ana connection ubalozini.

Kesi ikifika ubalozini kama sio ya msingi inazimwa chap. Mtu anatoka kidogo akirudi anaendelea na mambo yake. Wachina wako smart sana na flexible kwenye ku adopt mazingira halafu pia ni wepesi wa kuhonga kuliko kufata sheria. Hapo ndipo wanapoenda sawa na mamlaka zenu za kimchongo.
Sahihi mjumbe.
 
Mleta mada umeandika kishabiki na kibaguzi tu, lakini ulichoandika sio kweli.
Uhalisia ni huu.
1. Hakuna mchina anayeweza kuishi na kufanya biashara au kazi hapa Tanzania bila kibali. Wale jamaa ni smart kwa hilo maana wanajua msingi wa kuishi na kufanya chochote hapa Tz ni kuwa na hivyo vitu.

2. Hakuna mchina asiyelipa kodi TRA ambaye yuko hapo Kariakoo. Kulipa kodi kihalali ndio kinga ya hao wachina.

3. Kwa sababu ya kuongezeka idadi yao huku wakiwa makini, ujanja na uharaka wa kufanya biashara kumewatisha na kuwanyima fursa watanzania hapo Kariakoo hivyo kutaka upendeleo au udhibiti, jambo ambalo sio sahihi kisheria.

Ushauri.
Watanzania tuache kulalamika, tupambane.
si kweli kwamba wanalipa 100% ni janja janja sana kwenye kodi sometimes anaweza hata asikuuzie mzigo ukidai full risiti ila kwenye bei wanaacha mbali sana wabongo.

note: ninanunua mzigo kariakoo na kitumbini kwa hiyo nina uzoefu kwenye hili.
 
Okay na hapa paangaliwe ila kule kwenye mikataba mibovu ya madini, kule kwenye Bandari kwamba hatuwezi mnaona Kosher..., Yaani ni Divide and Rule kila mtu anavutia kwake huyu Mlanguzi Kariakoo wakibanwa hawa Wachina anageuka kuwa Chawa na kuona kila kitu poa..., Kule waalimu wakiongezewa mshahara wanaona madaktari wakigoma wanataka kuua watu...

Wastaafu wakiongezewa pensheni wanaona hawa wabangaizaji ambao watakuwa hawana pensheni walalamishi..., Walioajiriwa kwa kusomeshwa kwa grant wakiona vijana wanalalamika hawana ajira wanaawaambia waache uvivu waende wakauze uji...

The whole system is rotten tungekuwa vizuri huenda badala ya sisi kulalamika wanachukua kazi zetu za uchuuzi tungefurahia tunaagiza wachuuzi wakati sisi tunafanya kazi za administration / unyampara (ila ndio hivyo sisi ndio vijakazi in our own country)...
 
Wachina wako kwenye Cartels😁 yani ukimtingisha ana Godfather wake ambaye ana connection ubalozini.

Kesi ikifika ubalozini kama sio ya msingi inazimwa chap. Mtu anatoka kidogo akirudi anaendelea na mambo yake. Wachina wako smart sana na flexible kwenye ku adopt mazingira halafu pia ni wepesi wa kuhonga kuliko kufata sheria. Hapo ndipo wanapoenda sawa na mamlaka zenu za kimchongo.
Jamaa ni wazuri wa kuhonga balaaa
Kukupa 50mil ni kawaida
 
Jay one muelekeze bila matusi atakuelewa vizuri tu mkuu wangu..

Sometimes kwa mtu with Low IQ ili akuelewa anza kwa kumkera sana if possible kipigo hapo ataelewa, maana hivi nani hajui wachina machinga hawa wamejaa Tanzania ni hatari sana kwa nchi yetu na wananchi wetu, na wengi wao sio investors, tena wananchi wetu wengi wanakosa biashara sbb ya hao wachina kibao

Lile jengo jipya pale Ubungo litaua kabisa Kkoo sbb wao wanaleta bidhaa za Lowest Quality alafu wanauzia wananchi bei chee, tena wafanya biasha wazawa hawezi kufanya biashara sbb pale Ubungo tuliambiwa itakuwa center ya kusafirisha bidhaa nje ya nchi hasa za mazao na kupokea bidhaa toka nje ya nchi, ila sasa limekuwa Godown la wachina, ni hatari sana biashara za wazawa zitakufa Kkoo

Wachina walio Kkoo wamepanga flats magorofani Kkoo, halipi kodi wanauzia bidhaa huko huko maghorofani na kwa bei chee, kwa siri siri, Serikali inapoteza mapato mengi na wananchi wanakosa kufanya biashara sbb hawa wachina wanauza cheaper bila kodi na kwa uhuni uhuni, uchumi wetu wataumiza hawa wachina

Immigration pitieni huko Kkoo na nchi nzima, why Wachina wawe machina hapa kwetu?
 
Mleta mada umeandika kishabiki na kibaguzi tu, lakini ulichoandika sio kweli.
Uhalisia ni huu.
1. Hakuna mchina anayeweza kuishi na kufanya biashara au kazi hapa Tanzania bila kibali. Wale jamaa ni smart kwa hilo maana wanajua msingi wa kuishi na kufanya chochote hapa Tz ni kuwa na hivyo vitu.

2. Hakuna mchina asiyelipa kodi TRA ambaye yuko hapo Kariakoo. Kulipa kodi kihalali ndio kinga ya hao wachina.

3. Kwa sababu ya kuongezeka idadi yao huku wakiwa makini, ujanja na uharaka wa kufanya biashara kumewatisha na kuwanyima fursa watanzania hapo Kariakoo hivyo kutaka upendeleo au udhibiti, jambo ambalo sio sahihi kisheria.

Ushauri.
Watanzania tuache kulalamika, tupambane.
Namba tatu nikusahihishe kidogo kila taifa lina utaratibuwa furda kwa ajili ya wazawa ,sio sawa mchina kufungua duka kariako .
 
Winga haumii chochote mkuu .wanaoumia ni wafanyabiashara wenye mitaji mkubwa

Maana mchina kakuuzia vitu toka kiwandani kwake ili uje uuze nchini.na yeye anakuja nchini tena anakuja kuuza kwa bei ya chini tena Hadi mikoani kwa wateja wadogo.wewe utauza wapi?
😂😂😂😂😂😂😂 Wanaolalamika zaidi mawinga
 
Back
Top Bottom