Serikali imefuta service charge za TANESCO (Kanusho)

Serikali imefuta service charge za TANESCO (Kanusho)

Hizo taarifa zitaanza kufanya kazi kuanzia mwezi wa ngapi maana utekelezaji kwa Serikali unakuwa chini sana.
 
Italuwa safi, ila wasifanye usanii wa kutoa service charge na kuongeza matumizi per second! Yaani wanatoa service charge ila wakaongeza ilawa unit moja badala itumike saa moja ikawa inatumika dk 40.
 
Bora ziwekwe kwenye unit cost mkuu!

Unajua kwa mfano ukisafiri miezi sita nyumba umezima umeme, siku ukirudi unatakiwa kulipa service charge za hiyo miezi 6?
Ndugu yangu alisafiri toka mwaka juzi, juzi jumanne amerudi kutaka kununua umeme akadaiwa service charge 138000 ya miaka 2. Hana hamu.
 
Taarifa nilionayo ya kuaminika ni kwamba serikali imeagiza watu wote kubadilishiwa taarif za tanesco na kusajiliwa taarifu 0 au D1 ambayo haina service charge za kila mwezi.

Mameneja wote wa tanesco wa wilaya wameagizwawahakikishe hili linafanikiwa .

Inaweza kuwa habari njema kwa watu wasiopenda service charges.


ACHA UONGO NA KUPOTOSHA WATU.

UKWELI NI HUU HAPA

KUBADILISHA TARIFF KWA WATEJA WANAOISHI VIJIJINI
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuwataarifu wateja wake wote wa maeneo ya vijijini kuwa kuanzia tarehe 20 Januari, 2016 wateja wote wa maeneo ya vijiji watakaounganishiwa umeme kwa kutumia njiamoja (single phase) wataingizwa kwenye ‘Tariff D1’ kuanzia mwanzo.
Wateja wa umeme wa njia moja wa maeneo ya vijijini ambao kwa sasa wapo kwenye ‘Tariff T1’ na ambao matumizi yao ya umeme hayazidi wastani wa uniti 75 kwa miezi mitatu mfululizo, watahamishiwa ‘Tariff D1’. Kazi ya kuwahamisha wateja hao tayari imeanza na inatarajiwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Machi 2016.
Mteja wa kijijini atakaye hamishiwa kwenye ‘Tariff D1’ atapewa namba maalum (Key Change Number) kwa ajili ya kubadilisha Tariff kwenye mita yake pia. Namba hizo pamoja na maelezo yake zitatolewa wakati mteja atakaponunua umeme kwa mara ya kwanza baada ya kuhamishwa kwenye ‘Tariff D1’.
Mteja anaweza pia kupata Key Change Number pamoja na maelezo yake kwenye kituo cha huduma kwa njia ya simu kwa kupiga simu namba 022 2194400 au 0768 985100.

Imetolewana: OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO – MAKAO MAKUU.
 
really?itakuwa poa,wan ukawa tutapenda hilo

Haina ukweli wowote, mtoa mada amekuruuka, hii ni kwa watumiaji wa vijijini ambao matumizi yao kwa mwezi hayazidi unit 75 kwa mwezi ambao ni kwa wateja wa vijijini
 
Inawezekana hizo charge zimehamishiwa kwene unit cost, ujanja ni kwamba wakisha declare kuwa wamefuta angalia matumiz kama yatakuwa yako vile vile kwene units unazonunua.

KUBADILISHA TARIFF KWA WATEJA WANAOISHI VIJIJINI
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuwataarifu wateja wake wote wa maeneo ya vijijini kuwa kuanzia tarehe 20 Januari, 2016 wateja wote wa maeneo ya vijiji watakaounganishiwa umeme kwa kutumia njiamoja (single phase) wataingizwa kwenye ‘Tariff D1’ kuanzia mwanzo.
Wateja wa umeme wa njia moja wa maeneo ya vijijini ambao kwa sasa wapo kwenye ‘Tariff T1’ na ambao matumizi yao ya umeme hayazidi wastani wa uniti 75 kwa miezi mitatu mfululizo, watahamishiwa ‘Tariff D1’. Kazi ya kuwahamisha wateja hao tayari imeanza na inatarajiwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Machi 2016.
Mteja wa kijijini atakaye hamishiwa kwenye ‘Tariff D1’ atapewa namba maalum (Key Change Number) kwa ajili ya kubadilisha Tariff kwenye mita yake pia. Namba hizo pamoja na maelezo yake zitatolewa wakati mteja atakaponunua umeme kwa mara ya kwanza baada ya kuhamishwa kwenye ‘Tariff D1’.
Mteja anaweza pia kupata Key Change Number pamoja na maelezo yake kwenye kituo cha huduma kwa njia ya simu kwa kupiga simu namba 022 2194400 au 0768 985100.

Imetolewana: OFISI YA UHUSIANO,
TANESCO – MAKAO MAKUU.
 
Hili nalo lilikuwa jipu kubwaaa. Ni wizi uliochificha. Kama ni kweli ni jambo jema. Bado cement na bati


What is service charge?
A type of fee charged to cover services related to the primary product or service being purchased. For example, a concert venue may charge a service fee in addition to the initial price of a ticket in order to cover the cost of security or for allowing electronic purchases. Another example would be a fee for using the
ATM of a competing bank.
Mimi nadhani Service charge ni muhimu kwa shirika hila la uma kwa sababu zifuatazo

  1. Gharama kubwa za uwekezaji kuanzia kuzalisha,kusafirisha na kusambaza umeme,Gharama hizi kubwa zinapelekea wawekezaji kuona kuwa kuwekeza kwenye umeme kunachelewa sana kulipa (Long payback period),Hivyo shirika hili la uma limejitahidi kufikisha umeme hata maeneo yasiyo na faida hivyo kulichangia service charge ni kulipa nguvu Zaidi.
  2. Mteja anapopata tatizo kama nguzo kuanguaka,nyaya kukatika,meter kuharibika mafundi wa TANESCO wamekuwa wakitoa huduma bure kabisa kitu ambacho ingekuwa private company ingeingizwa kwenye gharama za mteja ,Service charge imesaidia hili
  3. Service charge ni kama bima ambayo tunawekeza kwenye shirika la umeme nchini ili liweze kuhudumia wateja wote pale wanapopata hitilafu ya umeme.
  4. Sio wateja wote wanaolipa service charge bali na kwa wateja wa kundi la T,Wanaotumia umeme kuanzia unit 75 mpaka 7500 kwa mwezi,Waleo wanaotumia umeme chini ya unit 75 wanalipa kwa bei ya ruzuku naamini kabisa service charge inawasaidia watanzania wenzetu wa hali ya chini.
 
Uongo serikali haijafuta service charge zaidi shilika linabadili tariff tu kama ifuatavyo

KUBADILISHA TARIFF KWA WATEJA WANAOISHI VIJIJINI

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuwataarifu wateja wake wote wa maeneo ya vijijini kuwa kuanzia tarehe 20 Januari, 2016 wateja wote wa maeneo ya vijiji watakaounganishiwa umeme kwa kutumia njiamoja (single phase) wataingizwa kwenye ‘Tariff D1’ kuanzia mwanzo.

Wateja wa umeme wa njia moja wa maeneo ya vijijini ambao kwa sasa wapo kwenye ‘Tariff T1’ na ambao matumizi yao ya umeme hayazidi wastani wa uniti 75 kwa miezi mitatu mfululizo, watahamishiwa ‘Tariff D1’. Kazi ya kuwahamisha wateja hao tayari imeanza na inatarajiwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Machi 2016.

Mteja wa kijijini atakaye hamishiwa kwenye ‘Tariff D1’ atapewa namba maalum (Key Change Number) kwa ajili ya kubadilisha Tariff kwenye mita yake pia. Namba hizo pamoja na maelezo yake zitatolewa wakati mteja atakaponunua umeme kwa mara ya kwanza baada ya kuhamishwa kwenye ‘Tariff D1’.

Mteja anaweza pia kupata Key Change Number pamoja na maelezo yake kwenye kituo cha huduma kwa njia ya simu kwa kupiga simu namba 022 2194400 au 0768 985100.

Imetolewana: OFISI YA UHUSIANO TANESCO – MAKAO MAKUU.
 
ILI NI JIPU ZAIDI YA DONDA NDUGU LAFAA LIBINYWEE KWANI LIMEWIVAAAAA
 
Tanesco ni Jipu lililokosa mtumbuaji.
 
Utakua poa sana! Tena sana mana ukikua ni wizi uliopitiliza....

Bado REA na EWURA nayo ni majizi mengine tena ni majipu yaliyokomaa.

Hebu angalia hapo nilijikusuru kununua umeme wa 10000/= nilichezea makato hadi kero hebu angalia UNIT nilizopota!!

Ni hatari sana hawa jamaa


Haina ukweli, iwapo kuna mabadiliko yoyote yatatangazwa na TANESCO habari zingine msiziamini
 
Ndugu yangu alisafiri toka mwaka juzi, juzi jumanne amerudi kutaka kununua umeme akadaiwa service charge 138000 ya miaka 2. Hana hamu.
Mimi nilijisahau umeme ukaisha usiku kumbe ikawa tar 1. Nikanunua kwa simu wa 7000 nikapata unit 1. Sikuwa nimejiunga kwenye huduma ya kuhamisha fedha toka benki. Wageni wapo wengi tukalala giza. Hii service charge sina hamu nayo naiona kama Lowassa.
 
Service charge haiwezi ondolewa, ndo kodi ya kumiliki umeme iyo kama wenye magari wanavolipa kodi ya kumiliki gari
Hata maji tunalipia service charge vile vile
 
Hiyo sio kweli hakuna Waraka unaotaka kuhamisha wateja tariff,
Labda uko njiani,tariff 0 ni mahususi Kwa watumiaji wadogo ambao matumizi Yao hayazidi unit 75!
Mkuu, kuingia kwenye tariff 0 hatua gani zinafuatwa?
 
Back
Top Bottom