Serikali imefuta service charge za TANESCO (Kanusho)

Serikali imefuta service charge za TANESCO (Kanusho)

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,151
Reaction score
20,076
Taarifa nilionayo ni kwamba serikali imeagiza watu wote kubadilishiwa taarif za Tanesco na kusajiliwa taarifu 0 au D1 ambayo haina service charge za kila mwezi.

Mameneja wote wa Tanesco wa wilaya wameagizwa wahakikishe hili linafanikiwa..

Inaweza kuwa habari njema kwa watu wasiopenda service charges.

========

Tofauti na ilivyoripotiwa na wachangiaji mbalimbali katika vyombo vya habari, Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO) limekanusha taarifa kwamba limefuta tozo ya huduma kwa wateja (service charge) ambayo huwa linawatoza wateja wake kila mwisho wa mwenzi pale wanaponunua umeme, FikraPevu linaripoti.

Akizungumza na FikraPevu, Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud, amekanusha taarifa hizo zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii, ukiwemo mtandao wa JamiiForums, ambao ni mtandao dada na gazeti hili. “Hakuna kitu kama hicho,” alisema kwa kifupi kwa njia ya simu.

Soma zaidi >> TANESCO yakomalia Tozo ya Huduma kwa Wateja
 
7000 ya service charge ilikuwa inatosha kunuua umeme wa wiki nzima.

Hizi ni habari njema.
 
Hiyo sio kweli hakuna Waraka unaotaka kuhamisha wateja tariff,
Labda uko njiani,tariff 0 ni mahususi Kwa watumiaji wadogo ambao matumizi Yao hayazidi unit 75!
 
Taarifa nilionayo ya kuaminika ni kwamba serikali imeagiza watu wote kubadilishiwa taarif za tanesco na kusajiliwa taarifu 0 au D1 ambayo haina service charge za kila mwezi.

Mameneja wote wa tanesco wa wilaya wameagizwawahakikishe hili linafanikiwa .

Inaweza kua habari njema kwa watu wasiopenda service charges.
Hilo bado halijatekelezwa bali limetelekezwa... Kwakuwa Leo nimekatwa zaidi ya elfu sita
 
Habari isiyo na source haiwezi kuwa ya kweli..
 
Hii habari iwe kweli. Nafikiri ni baada ya ule uzi wa majuzi
 
Naomba msaada nikitaka kuomba kubadilishwa kwenda zero tarriff
 
Imebidi niangalie tarehe ya hii post isijekua ni 01 April...
 
Hilo ni sawa na jipu la bandari wafute ila wasije ongeza unit charge kupalilia vichaka vyao
 
Back
Top Bottom