DOKEZO Serikali iingilie kati huu ubadhirifu unaofanyika Shule ya Sekondari Venance Mabeyo-Busega

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Madukani

Member
Nov 25, 2022
6
6
Sisi wazazi tunaosomesha watoto wetu shule ya sekondari Venance Mabeyo tulikaa kikao cha wazazi na kukubaliana kila mzazi kuchangia limu moja kwa kila mtoto ili kufanikisha zoezi la ufundishaji shuleni hapo,cha kushanga watoto wetu wamekuwa wakipigwa kila Mara wanapokuwa kwenye mitihani ikiwa watatumia karatasi zaidi ya moja.Sababu ya kuchapwa watoto ni kuwa shule imekuwa ikuuza rimu pamoja na kupokea pesa za rimu hivyo kuishia kwenye mifuko ya walimu hivyo kupelekea uhaba wa rimu(Karatasi) shuleni

Mfano hivi juzi watoto walifanya mtihani wa Mock mkoa ,shule ilikosa limu na kupelekea sisi wazazi kuingia gharama ya kununua karatasi kwa ajili ya kujibia mitihani.

Kuna taarifa kuwa shuleni hapo hakuna rimu(karatasi) hata moja,zote zimeuzwa mbaya zaidi mwalimu aliyekuwa anahusika na kuchangisha rimu(karatasi) amekuwa akiwataka watoto wampe pesa shilingi 10,000 ili wasidaiwe rimu(karatasi) na matokeo yake huwa anakula hizo pesa.

Wazazi baadhi tulimfuata mkuu wa shule lakini hakuweza kuweka bayana aliahidi kulishughulikia lakini mpaka muda huu hakuna rimu hata moja shuleni hapo ambapo shule hii ina watoto 600,huku watoto waliolipia rimu(karatasi) wakiwa zaidi ya mia nne(400),huku mitihani iliyofanyika shuleni hapo ni mitihani minne tutoka January hadi muda huu ninapoandika uzi huu ila shuleni hakuna hata karatasi moja ,ikumbukwe kuwa rimu moja ina karatasi 500,hata kama iweje mtoto mmoja hawezi tumia karatasi 500,kwa mitihani minne maana yake mtoto ametumia karatasi zaidi ya 125 kwa mtihani mmoja

Hivyo sisi wazazi tunaomba serikali iingilie kati kwani hali hii inatuumiza sisi wazazi na kutukatisha tamaa maana tunajitoa ili kufanikisha elimu lakini walimu wanauza rimu na kutumia pesa kwa matumizi binafsi
 
Hivi suala la rimu shuleni ni lakuleta humu? Si mrudushe mwitikio na malalamiko kikao cha wazazi? Ikishindika si yupo mratibu elimu kata? Ofisi za Elimu zipo halimashauri zote na zina maafisa elimu. Huko mmeenda?
 
Hivi suala la rimu shuleni ni lakuleta humu? Si mrudushe mwitikio na malalamiko kikao cha wazazi? Ikishindika si yupo mratibu elimu kata? Ofisi za Elimu zipo halimashauri zote na zina maafisa elimu. Huko mmeenda?
Duh mkuu kote huko tumefika hadi kwa mkuu wa shule ila wanalindana,tuntaka watumwe watu waje kuchunguza,ujue rimu 400 kuisha ndani ya miezi mitano ni hatari sana
 
Mtoa mada, umeshindwa nini kumuona Afisa elimu kata au mtendaji kata kumueleza hii habari?

Au umeshindwa nini kumuona mwenyekiti wa wazazi!!!

Sio kila kitu unakimbilia huku, acha utoto!!

Waone hao watu, unipatie mrejesho.
 
Hata jipu lilianza kama kipele. Jamaa anayo haki ya kulalamika, kama wewe una milioni yeye ana elfu
Ndicho kipato chake. Na ni unafiki huu kujidai unazo kumbe huna, haki udaiwa kuanzia chini kupanda juu
Uwezi kudai divai wakati mkate huna. Mwacheni apiganie kinachostahili kuna wengi nyuma yake wenye kipato kama chake.
KONGOLE MCHIZI
 
Mkuu fuatilia ngazi kwa ngazi mtapata ufumbuzi wa kudumu
Mkuu sisi kama wazazi tulimfuata mkuu baada ya kupokea malalamiko toka kwa watoto wetu lakini majibu yalikuwa ya kumlinda mwalimu,sasa muda wa kwenda mjini ni shida,ninaimani viongozi wa serikali wako humu watachukua hatua dhidi ya tuhuma hizi
Mkuu fuatilia ngazi kwa ngazi mtapata ufumbuzi wa kudumu
 
Una ushahidi wa kulipia pesa ya "limu"?

Join instruction si huwa ina michango yote? Tuwekee hapa mkuu
 
Sisi wazazi tunaosomesha watoto wetu shule ya sekondari Venance Mabeyo tulikaa kikao cha wazazi na kukubaliana kila mzazi kuchangia limu moja kwa kila mtoto ili kufanikisha zoezi la ufundishaji shuleni hapo,cha kushanga watoto wetu wamekuwa wakipigwa kila Mara wanapokuwa kwenye mitihani ikiwa watatumia karatasi zaidi ya moja.Sababu ya kuchapwa watoto ni kuwa shule imekuwa ikuuza rimu pamoja na kupokea pesa za rimu hivyo kuishia kwenye mifuko ya walimu hivyo kupelekea uhaba wa rimu(Karatasi) shuleni

Mfano hivi juzi watoto walifanya mtihani wa Mock mkoa ,shule ilikosa limu na kupelekea sisi wazazi kuingia gharama ya kununua karatasi kwa ajili ya kujibia mitihani.

Kuna taarifa kuwa shuleni hapo hakuna rimu(karatasi) hata moja,zote zimeuzwa mbaya zaidi mwalimu aliyekuwa anahusika na kuchangisha rimu(karatasi) amekuwa akiwataka watoto wampe pesa shilingi 10,000 ili wasidaiwe rimu(karatasi) na matokeo yake huwa anakula hizo pesa.

Wazazi baadhi tulimfuata mkuu wa shule lakini hakuweza kuweka bayana aliahidi kulishughulikia lakini mpaka muda huu hakuna rimu hata moja shuleni hapo ambapo shule hii ina watoto 600,huku watoto waliolipia rimu(karatasi) wakiwa zaidi ya mia nne(400),huku mitihani iliyofanyika shuleni hapo ni mitihani minne tutoka January hadi muda huu ninapoandika uzi huu ila shuleni hakuna hata karatasi moja ,ikumbukwe kuwa rimu moja ina karatasi 500,hata kama iweje mtoto mmoja hawezi tumia karatasi 500,kwa mitihani minne maana yake mtoto ametumia karatasi zaidi ya 125 kwa mtihani mmoja

Hivyo sisi wazazi tunaomba serikali iingilie kati kwani hali hii inatuumiza sisi wazazi na kutukatisha tamaa maana tunajitoa ili kufanikisha elimu lakini walimu wanauza rimu na kutumia pesa kwa matumizi binafsi
Wewe siyo mzazi mkuu! Wewe ni mwalimu uliyechangamka. Hakuna mzazi ajue hesabu za rimu shuleni kama wewe!

Acheni kuchanga hizo rimu. Kwani ni lazima? Halafu, kama suala ni rimu kwa nini mnapeleka pesa shuleni? Hivi rimu ni 10,000/= kweli?

Halafu, shule inauza rimu zipi ilihali nyie mnapeleka pesa shule!

Mwisho fanya mtego, ukamate wanunuzi wa rimu za shule. Uwalete tuwashughulikie.

Tunaheshimu mawazo yako ila chukua hatua! Siyo kulalamika tu.
 
Acha kulia lia! Yaan serikali iache mambo ya msingi kama kuuza bandari, waje wafatilie rimu! Ndo maana ndo maana makabila mengine yameendelea sana, huwez kuta mzazi anaelipa ada mil 4 analalamikia rimu
We mwalimu rudisha hela za rimu hizo ,mambo ya bandari tutakutana nayo mbere huko
Rimu kwanza,
Tule tulipopeleka mboga na urefu wa kamba zetu.
 
Sisi wazazi tunaosomesha watoto wetu shule ya sekondari Venance Mabeyo tulikaa kikao cha wazazi na kukubaliana kila mzazi kuchangia limu moja kwa kila mtoto ili kufanikisha zoezi la ufundishaji shuleni hapo,cha kushanga watoto wetu wamekuwa wakipigwa kila Mara wanapokuwa kwenye mitihani ikiwa watatumia karatasi zaidi ya moja.Sababu ya kuchapwa watoto ni kuwa shule imekuwa ikuuza rimu pamoja na kupokea pesa za rimu hivyo kuishia kwenye mifuko ya walimu hivyo kupelekea uhaba wa rimu(Karatasi) shuleni

Mfano hivi juzi watoto walifanya mtihani wa Mock mkoa ,shule ilikosa limu na kupelekea sisi wazazi kuingia gharama ya kununua karatasi kwa ajili ya kujibia mitihani.

Kuna taarifa kuwa shuleni hapo hakuna rimu(karatasi) hata moja,zote zimeuzwa mbaya zaidi mwalimu aliyekuwa anahusika na kuchangisha rimu(karatasi) amekuwa akiwataka watoto wampe pesa shilingi 10,000 ili wasidaiwe rimu(karatasi) na matokeo yake huwa anakula hizo pesa.

Wazazi baadhi tulimfuata mkuu wa shule lakini hakuweza kuweka bayana aliahidi kulishughulikia lakini mpaka muda huu hakuna rimu hata moja shuleni hapo ambapo shule hii ina watoto 600,huku watoto waliolipia rimu(karatasi) wakiwa zaidi ya mia nne(400),huku mitihani iliyofanyika shuleni hapo ni mitihani minne tutoka January hadi muda huu ninapoandika uzi huu ila shuleni hakuna hata karatasi moja ,ikumbukwe kuwa rimu moja ina karatasi 500,hata kama iweje mtoto mmoja hawezi tumia karatasi 500,kwa mitihani minne maana yake mtoto ametumia karatasi zaidi ya 125 kwa mtihani mmoja

Hivyo sisi wazazi tunaomba serikali iingilie kati kwani hali hii inatuumiza sisi wazazi na kutukatisha tamaa maana tunajitoa ili kufanikisha elimu lakini walimu wanauza rimu na kutumia pesa kwa matumizi binafsi
Rimu mia sita(600) ukizitumia kama tofari umaweza kujenga madarasa mawili.
 
Back
Top Bottom