Proved
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 36,957
- 49,473
Mtaji wa Ccm ni ujinga wa Watz, na wanautumia vizuri sana.Nilikua nazurura huko Fb nikakutana na video moja nadhani Ni huko Isimani kwa mheshimiwa Lukuvi, kiongozi wa CCM anawahutumia wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na Kadi ya CCM na mpango wa CCM kuhakikisha kwamba ifikapo mwezi wa nane kila mtanzania na kila Mwana CCM atakua nakadi ya CCM .
Miongoni mwa Mambo anayoyataja kiongozi huyu wa chama Ni kwamba Kadi ya CCM inakuwezesha kupata huduma muhimu kumi na nne.
Miongoni mwa huduma anazozitaja Ni Kadi hiyo kutumikaa Kama bima ya afya kwa akina mama, kutumika kwa ajili ya huduma za kibenki kwa maana Ni mbadala wa ATM card , kutumika kama kitambulisho cha mifuko ya hifadhi ya jamii.
Kilichonisitikisha sio yeye kuongea maneno hayo , Bali Ni ujinga na umbumbu wa watu waliokua wanamsikiliza, na kumpigia makofi kwa shangwe kabisa na naamini watajitokeza kujiandikisha na kutoa fedha kwa ajili ya kusubiri kadi za CCM kwa ajili ya matumizi katika huduma zaidi ya kumi na nne.
Unaweza kuona kwamba CCM imewanyima wananchi elimu ya uraia na elimu ya kujitambua na kwa maana hiyo wanaweza kusema na kufanya watakalo pasina kuhojiwa na wananchi ambao ni wanachama na walipa Kodi wako.
Kumbe Ni kwamba determination ya chama Ni uchaguzi tu na kubakia madarkani huku wakidelay kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.
Video hiyo inapatikana kwenye ukurasa wa askofu Emausi Bandekile Mwamakula.
Mh Lukuvi imebidi aangalie kwa masononeko na huruma kubwa kwani anajua kabisa huo Ni ulaghai uliopitiliza.