Serikali, hiki mnachokifanya hakikubaliki!

Serikali, hiki mnachokifanya hakikubaliki!

Huu ni ujinga na upumbavu wa kiwango cha lami! Haiwezekani mie nitaandamana kwa huu upuuzi wao
Nadhani lami sometimes hua inachoka na kuhitaji viraka. Huu ni ujinga wa kiwango Cha zege lile kali kabisa.

Hii nchi kua ya chama kimoja ni upuuzi uliopitiliza. Wananchi waliohusika kukipitisha hiki chama wote walaniwe
 
Wazanzibar walikua wakimbizi kipindi cha magufuri?

Unajua Lipumba na Slaa walijeruhiwa kipindi gani?

Nani alimuua Mwangosi

Kipigo cha ulimboka na sumu ya mwakiembe?

Vp kuhusu Filikunjombe?

Umeyasahau au hukuwepo?
Unataka kujustify Nini mkuu hebu tusaidie, unataka tuseme matukio haya Ni sababu ya kuona tunachoketewa hakina mchango wa Magufuli, as per Magufulfication?

Watangulizi wake walijitenga na hayo matukio lakini yeye aliambatana nayo Tena kwa extent kubwa ilivyokua inatisha kulingana na Mila na desturi za kitanzania, aliyekua msaidizi wake Sasa ameyaimarisha na anayaweka kimfumo zaidi! Yani kwa lugha nyeoesi anajifanya kujitenga nayo kama sio yeye yanaingia kwenye mfumo!

Si umeona umeme na kero zake? Lawama Ni kwa January, Kodi na tozo lukuki lawama Ni kwa Madelu!

Labda utuambie yte hayo Ni Sera na maisha ya CCM ambapo hata hivyo hatutaweza kumtenga Magufuli kwa sababu alikua mwenyekiti wa chama na top katika maamuzi ya Chama.
Na alihubiri Sera hizo hizo kandamizi na za kibaguzi akiwa na Shati la chama.
 
Unataka kujustify Nini mkuu hebu tusaidie, unataka tuseme matukio haya Ni sababu ya kuona tunachoketewa hakina mchango wa Magufuli, as per Magufulfication?

Watangulizi wake walijitenga na hayo matukio lakini yeye aliambatana nayo Tena kwa extent kubwa ilivyokua inatisha kulingana na Mila na desturi za kitanzania, aliyekua msaidizi wake Sasa ameyaimarisha na anayaweka kimfumo zaidi! Yani kwa lugha nyeoesi anajifanya kujitenga nayo kama sio yeye yanaingia kwenye mfumo!

Si umeona umeme na kero zake? Lawama Ni kwa January, Kodi na tozo lukuki lawama Ni kwa Madelu!

Labda utuambie yte hayo Ni Sera na maisha ya CCM ambapo hata hivyo hatutaweza kumtenga Magufuli kwa sababu alikua mwenyekiti wa chama na top katika maamuzi ya Chama.
Na alihubiri Sera hizo hizo kandamizi na za kibaguzi akiwa na Shati la chama.
Emu soma ulichoandika halafu unambie watangulizi wa Magufuli walijitenga vipi na matukio yale...

Ninachokiona, Magufuli hakua mnafiki na hao wengine waliumiza watu huku wanatabasamu.
 
Hii ni nzuri sana we hujui TU hakuna aliye salama Hadi wao wenyewe viongozi nchi inakwenda kuwa ya TISS HAKUNA CHA SIASA TENA KIONGOZI AKILETA FOKOFOKO ALAKIWA KICHWA
Kila mtu ataogopa uovu maana hajui siku wala saa atakavyodakwa...Ache inyeshe tuone panapovuja
 
Wazanzibar walikua wakimbizi kipindi cha magufuri?

Unajua Lipumba na Slaa walijeruhiwa kipindi gani?

Nani alimuua Mwangosi

Kipigo cha ulimboka na sumu ya mwakiembe?

Vp kuhusu Filikunjombe?

Umeyasahau au hukuwepo?
Sijasema kabla ya Magufuli kulikuwa hakuna matatizo, ila yaliongezeka kipindi cha Magufuli
 
Which one is advocating for transparency and accountability hebu fafanua mkuu..
Magulification does advocate for transparency and accountability. Period

My broda, You have to separate your definition of Magulification as stipulated by one and only Prof. PLO Lumumba
and your twisted one....of which I am sure is a combinations of picked/made up conspiracies. Below is the real.....
Magulification
This has a lot to do with Magufulication, yeye ndio alijenga msingi wa kutumia vyombo vya dola kuwadhibiti wakosoaji wake, kwahiyo hii Ni maboresho In a more sophisticated way!
Unajua aliwahi kusema I WISH I I COULD BE AIJIIPI?
Nadharia ya Magulification haikujengwa kwa msingi/misingi wa kutumia vyombo vya Dola! au Ya!
Hayo yako hayana uthibitisho wowote ule. Nenda ukamzodoe Rais sasa hivi uone moto wake! Unacheza na dola....mfyuuuuu😅
WAFUKUZE HUKO BUNGENI WAKIJA HUKU NITAWASHIGHULIKIA SABABU HUKU HAWANA KINGA?
Unataka kusema wewe hujawai kupiga mkwara? Ati 'njoo mtaani kwetu uone?' Wacha hizo!
Hatahivyo....

....alizungumza hayo kwa muktadha upi?? Wapi na kwa walengwa gani? wacha upotoshaji na maneno ya kumezeshwa
.AKALIAMBIA GAZETI LA MWANANCHI KUWA "YOU ARE NOT FREE TO THAT EXTENT"
Are you free? and to what extent? Cheza wewe!
Sasa kwa Sheria hii mpya hutaskia sehemu hayo yakisemwa mkuu! Unless umekua pro-magufuli kupitiliza hutaona Hilo! And umoja party haitasajiliwa nimekaa hapa utaniambia
Unajichanganya.
Wewe wacha ukuu na muumba. Syllo will do!
 
Ajabu mkaacha kumuomba Mungu aiuwe ccm badala yake mkamuomba amuuwe Magufuli na kweli akawajibu huku tukitegemea mabadiliko, ila cha kusikitisha bado Magufuli anaendelea kuonekana ni tatizo hadi sasa pamoja na kumsema kote kule kwa madai ya kwamba ili tujifunze tusirudie tena makosa ila wapi.

Nadhani maombi ya kifo yangeelekezwa kwa chama cha ccm tungekuwa tumeondoa mzizi wa tatizo.
 
Mkuu samahani labda Mimi nina tongo tongo!
Ninachojua mimi kwenye mchakato wa kutunga Sheria bunge halitungi Sheria bali linajadili muswada wa sheria na kushauri kipi kiongezwe na kipi kipunguzwe!

Wizara husika hukaa na kuona mahitaji ya kisheria katima wizara au Idara husika!
Wataalamu wa sheria wa wizara wanadraft mapendekezo kwa kishirikina na mwanasheria mkuu wa serikali.

Draft husika huwasilishwa kwenye kikao cha Baraza la mawaziri ambapo Rais ndiye mwenyekiti, baada ya Baraza la mawaziri kuijadili na kukubalika juu ya Hiyo Draft inaandikwa Kama Billl of law au muswada wa sheria.

Wakati wa vikao vya Bunge waziri huwasilishwa muswada huo Bungeni ili wabunge waweze kuusikia na kuujadili kwa pamoja huku wakitoa mapendekezo na marekebisho mbalimbali.

Serikali hurudi na kukaa na kupitia mapendekezo yaliyotolewa na wabunge pamoja na wadau wa swala husika.

Baada ya hapo hurudihswa tena bungeni ili kupigiwa kura na kupitishwa ili kuwa Sheria.
Aidha baada ya kupitishwa muswada huo hurudishwa kwa rais ili atie saini kuwa Sheria hiyo imeanza kutumika.
Kwa mujibu wa katiba yetu na mtiririko huo ni dhahiri kwamba sheria au mapendekezo ya Sheria yanaanza na Rais na sio wabunge unless mbunge aje na hoja binafsi katika sheria husika.

Na inapotokea Bunge na serikali wakashindwa kuelewana katika Sheria husika Rais anaweza kulivunja Bunge na tukarejea kwenye uchaguzi!

Kwa Sheria hii iliyoletwa na Waziri Simba chawene Ni Sheria inayoenda kulinda Maslahi ya Viongozi wa CCM ikiwemo Rais wabunge mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali ambao kwa nafasi zao wanaweza kuwatumia watu wa usalama wa taifa katika kutimiza majukumu yao au kutimiza matarajio yao kisiasa.

Kufungua kinacholalamikiwa Ni kuwaongezea kinga za kijinai maafisa wa usalama wa taifa au wafanyakazi wa idara ya usalama wa taifa wanapokua wanatimiza majukumu yao.
Swali je Nani anajua mstari wa majukumu ya afisa wa usalama wa taifa kiusalama au binafsi!? Kwamba anaweza kuutwaa uhai wa mtu lakini katika Mazingira ambayo hayana uhusiano na usalama wa taifa lakini sheria itamlinda! (Kinga ya kutishtakiwa) kwa makosa ya kijinai.


Sheria inaenda kubadilishwa kwamba Idara ya usalama wa taifa haitakua Tena chini ya waziri Bali Rais!

Lakini pia kuna kuongezewa kwa kiapo Cha kutunza siri hata baada ya kustaafu au kuacha kazi, kwamba kwakua watakua na Kinga ya kijinai I maana hata makosa ya hovyo watakayofanya kwa kutumiwa na watawala hakuna namna watatoa taarifa kwa vyombo vingine vya dola au serikali nyingine!
Kwahiyo Sheria hii inaonekana kujenga Mazingira ya kuminya wakisoaji wa serikali kwa namna ya tofauti kuliko wakati uliopita!
Maelezo mazuri sana
 
Uhuu ni ugese na ugese hauna chama tujiandae kuandamana
 
Ni upuuzi na Ulimbukeni kufikiria kati ya Mashirika hayo tajwa ya Kijasusi ulaya na marekani hayana Kinga. Au majasusi wao hawana kinga.
Ni upotoshaji wa hali ya Juu sana.

Atakaye niwekea Jasusi yeyote yule aliyewahi fanya kazi kati ya taasisi hizo za nje, na kuvunja sheria akiwa kazini na akafunguliwa mashitaka ya jinai aweke hapa. TUSIDANGANYANE na uharakati uchwara.
 
Ccm wanafanya watakalo
Nilikua nazurura huko Fb nikakutana na video moja nadhani Ni huko Isimani kwa mheshimiwa Lukuvi, kiongozi wa CCM anawahutumia wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na Kadi ya CCM na mpango wa CCM kuhakikisha kwamba ifikapo mwezi wa nane kila mtanzania na kila Mwana CCM atakua nakadi ya CCM .

Miongoni mwa Mambo anayoyataja kiongozi huyu wa chama Ni kwamba Kadi ya CCM inakuwezesha kupata huduma muhimu kumi na nne.

Miongoni mwa huduma anazozitaja Ni Kadi hiyo kutumikaa Kama bima ya afya kwa akina mama, kutumika kwa ajili ya huduma za kibenki kwa maana Ni mbadala wa ATM card , kutumika kama kitambulisho cha mifuko ya hifadhi ya jamii.

Kilichonisitikisha sio yeye kuongea maneno hayo , Bali Ni ujinga na umbumbu wa watu waliokua wanamsikiliza, na kumpigia makofi kwa shangwe kabisa na naamini watajitokeza kujiandikisha na kutoa fedha kwa ajili ya kusubiri kadi za CCM kwa ajili ya matumizi katika huduma zaidi ya kumi na nne.

Unaweza kuona kwamba CCM imewanyima wananchi elimu ya uraia na elimu ya kujitambua na kwa maana hiyo wanaweza kusema na kufanya watakalo pasina kuhojiwa na wananchi ambao ni wanachama na walipa Kodi wako.

Kumbe Ni kwamba determination ya chama Ni uchaguzi tu na kubakia madarkani huku wakidelay kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli.

Video hiyo inapatikana kwenye ukurasa wa askofu Emausi Bandekile Mwamakula.

Mh Lukuvi imebidi aangalie kwa masononeko na huruma kubwa kwani anajua kabisa huo Ni ulaghai uliopitiliza.
 
Back
Top Bottom