Sensa 2012: Yanayojiri

watu wataesabiwa X10, majumbani, kwenye train, mabasi, pikipiki, bicycle etc, ilimradi form zijae tu, mgomo uwe umefail

Tanzania mbona tunachekesha ulimwengu?? Kwa nn wasihesabiwe hao waliopo waliogoma tukatafuta mathematical formula ya kuwaingiza kuliko ku cheat? au kwa nn zoezi lisingeachwa kwanza hadi pawepo na muafaka kuliko kuchezea pesa za walipa kodi halafu mnatuletea takwimu za kupika??
 
Onyo! Nyumba hii ni ya waisilamu hatuhesabiwi! Awamu ya nne kazi kweli kweli!
 
Bamukunda inawezekana umechangia kwa Ustadh Ponda kuhesabiwa kama kweli ni jirani yako.Lakini inasemekana baadhi ya Wapinzani wa Sensa walipoitwa Ikulu na kupewa vidonge vyao walitoka wakiwa ndembendembe.Usishangae hilo ndio hali halisi ya baadhi ya Wabongo.
 

Umesahau ili 62% iliyompeleka Magogoni ni ya waislamu. kwa hiyo lazima awe makini na majibu yake vinginevyo atapinduliwa na hiyo 62% ya waislamu. wewe hujiulizi kwanini CUF imeshuka daraja safari hii
 
tunawatakia sensa njema ila muangalie maana tanzania kila jambo linanasababu wanoogoma wanasababu zao nawanaokubali wanasababu zao kikubwa serikali haijaelimisha watu / wananchi maana halisi ya sensa na udini ndio uliochangia kuharibu sensa
 
Watu kwa ku copy na ku paste mko juu...ungeandika Kiswahili tungekuelewa wengi Mkuu..


 
Mpaka sasa bado waislam wengi wapo misikitini wanafanya ibada sijui makarani watawafauata?
Maana walilala msikitini na hawakufutwa usiku.

jk kawaambia hawawezi kukaa huko mda wote njaa itawauma watatoka tu na kuhesibiwa.!
 
Wakahesabu madawati kwenye shule za kata,hahesabiwi mtu hapa LIWALO NA LIWE KUDADADADEKIII!!!!
 

Ukileta mfano wa Igunga na mie takupa mfano wa Kanisa Sumbawanga unaukumbuka huo mgogoro au wewe unakumbuka Igunga, kwa hiyo kwa akili yako ndio unatuambia kura walizopata Chadema zilikuwa za Wakiristo tu.

Unaweza kutupa ushaidi kuwa mwaka 2010 Waislam Misikitini waliambiwa waipigie kura CCM? Kama kuropoka hata mie naweza kukuambia Wakiristo waliambiwa Makanisani waipigie kura Chadema.
 
Duh! Lumande tena,hivi sisi ambao tunaishi wenyewe hamna ata msaidizi kazini nako mpaka saa kumi ukiongeza na folen unafika saa mbili usiku ata lumande inabidi watuvumilie sababu kama leo hawajaonekana kwangu basi kuniona mpaka jpili la sivyo tutafukuzwa kazi.
 

Unazungumzia wale walio sema Jamaa Chaguo la Mungu (wakatoliki) na Malasusa au wale waliompamba Padri MZINIFU:spy:
 

Asante kwa taarifa za kifo cha Neil Armstrong, jamaa alipenda sana anga, kumbe alipata leseni ya urubani kabla hajapata leseni ya kuendesha gari!
 


Mkuu wa mkoa flani alisema Jana watakaogoma wataipata fresh ya Mwaka na wasipoonekana watakadiriwa maana wanazaa sana takwimu za awali zinaonyesha Tuko 45 million ivo kwa sasa wakikadiria 47-50 million watakuwa hawajakosea maana watz wanazaa Kama kuku Tehe Tehe Tehe Mimi sijabandika angalizo mlangoni kwani mwalimu wangu alinifundisha kuwa (don't trouble trouble unless trouble trouble you) ila hawafiki toka Jana usiku nawasubiria ila naambiwa wanapiga kazi mpaka Baa Naona bora wakanikute huko huko Baa.
 

Si ndio hao BAKWATA waliopewa millioni 100 ili kuhamasisha waislamu washiriki sensa na serikali hiyohiyo iliyowatumia mwaka 2010. Ndo upate picha Chombo cha BAKWATA kipo kwa ajili ya nani na si kukazani Mufti kasema ndo huyo huyo anaeipigia kampeni CCM.
 
Kuna karani mmoja rafiki yangu yeye kapangiwa Mwananyamala Kisiwani ananiambia mpaka saa 9 kaishahesabu nyumba 12 tu kila nyumba akiingia anakutana na upinzani mkali watu hawataki kuhesabiwa.
 
Wadau mi niko border Tunduma hapa navuka, kurudi huko mpaka baada ya wiki mbili itakuwaje?

Wewe ukirudi utakuwa umehesabiwa na uliowaacha nyumbani, si lazima uwepo physically wakati wa kuhesabiwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…