Vifungu gani vya biblia vizuri kwa mtu anaefunga tatu kavu?
3 kavu
Vifungu inategemea na mwenyewe Roho wa Mungu anapomsukuma asimamie.
Mimi nampa hili;
Mathayo 19:27-29
"Ndipo Petro akajibu,akawaambia,Tazama,sisi tumeacha vyote tukakufuata;tutapata nini basi?
Yesu akawaambia,Amin,nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi,katika ulimwengu mpya,atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake,ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israel.
Na kila mtu aliyeacha nyumba,au ndugu wa kiume au wa kike,au baba,au mama,au watoto,au mashamba,kwa ajili ya Jina langu atapokea mara mia na kuurithi uzima wa milele.
................
●Basi kwa ajili ya Bwana ameacha chakula kwa muda,atapokea majibu na Mungu atamtendea na kumzidishia katika mengi.
● Anafuata mwenendo na nyayo za Kristo katika utakatifu (utii) 1Petro 1:14-16,2:21-22
●Atapokea majibu kwa ushindi maana maombi ya kufunga kujitaabisha yana nguvu
Mathayo 17:21
●Kuomba kwake kwafaa sana
Yakobo 5:16-18