Selfika na JF: Snap it. Show it

Wakuu kwa anayetumia Airtel naomba aniambie au akiweza anioneshe vifurushi vyao, hasa vya internet vikoje nataka niujaribu na huu mtandao.

Bongo hapa mitandao ambayo sijatumia ni Airtel na Zantel tu, Zantel sijawahi kuwaza kutumia maana nasikia iko vizuri zaidi kwa upande wa Zanzibar kuliko Bara.

Airtel ndiyo nimekuwa nikijishauri nitumie au nisitumie, ila kwa sasa nimefikia muafaka kuwa niangalie kwanza muelekeo wa vifurushi vyao ikishindikana basi narudi TTCL.

Kwa sasa natumia Vodacom na Halotel ila nataka niachane na Halotel maana siwaelewi na Tigo ndiyo kabisa sitaki hata kuwasikia, japo Vodacom wanazingua ila sitakiwi kuuacha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…