Mara nyingi tunapokuwa tuna ibada/sadaka ya shukrani kama familia, huwa tunaomba tusindikizwe na tenzi hii
1. Mungu amenihurumia,
Tendo hili kubwa sana,
Sikustahili jambo hili,
Nimelipata bure tu!
Sasa najua hayo yote X2
Nasifu rehema zake X2
2. Nalistahili kupotea,
Lakini nahurumiwa,
Mungu amenipatanisha,
Na yeye kwa Yesu Kristo,
Sababu hii namtumikia X2
nasifu huruma yake X2
3. Mungu mwenye huruma nyingi,
Usininyime huruma,
Naitafuta siku zote,
Nikiulizwa na watu,
Hivi vyote vyatoka wapi? X2
Nasema ni hurumaβ¦