Selfika na JF: Snap it. Show it

UNATAKA KUISHI UMRI MREFU?

Makala iliyoandikwa katika jarida la "New England Medicine" imeelezea siri za umri mrefu.



Watafiti nchini Marekani wamebaini kwamba kutokula kwa masaa 16-18 au kufunga kula kila baada ya muda fulani katika wiki hurefusha maisha na kuzuia magonjwa.
Katika makala iliyoandikwa katika jarida la “New England Medicine”, imebainishwa kwamba kula ndani ya masaa 6-8 katika siku na masaa yaliyobaki 16-18 kukaa mbali na chakula hukinga mwili kutokana na magonjwa tofauti, ikiwa ni pamoja na kupunguza shinikizo la damu na kurefusha maisha.

Katika makala hiyo imesisitizwa kwamba kufunga kula ni moja ya njia zinazowezapendekezwa katika tiba ya kiribatumbo, kisukari na magonjwa ya moyo, katika hilo inapendekezwa kufunga siku 2 kwa wiki au “kula kiasi kidogo kila siku”
Utafiti uliofanywa kwa kutumia binadamu na wanyama umeonyesha kwamba kufunga kila baada ya muda maalumu huweza michakato katika mwili “metabolism” kuhuishwa upya kitu ambacho hufanya afya ya chembe hai za mwili "cell" kuboreka.

Jr
 
Hakika nimeokota kitu hapa mzee wa sangoma
 
Siku hizi kazi zinazofanywa na wanaume hata wanawake wanafanya ndiyo hoja yangu kuu, hali ya uchumi imeforc 50%=50% ni vile hukunielewa tu, kuna malori wanawake wanatandika gia transit ndani na nje ya nchi wanapeleka mizigo,
 
Oohh yeah sikukuelewa,, nikajua na wewe ni moja ya wale wanaume ambao wao kila kitu wanawaza usawa tu yaani 50/50..

Sijui kwanini ila eti mie mambo magumu magumu ndiyo huwa napenda kuyajua,, na huwa najivunia kabisa kuyajua..
Siku hizi kazi zinazofanywa na wanaume hata wanawake wanafanya ndiyo hoja yangu kuu, hali ya uchumi imeforc 50%=50% ni vile hukunielewa tu, kuna malori wanawake wanatandika gia transit ndani na nje ya nchi wanapeleka mizigo,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…