Kwahiyo tutaonana eenh?? Hivi mimi si ndiyo nimetoka kusema siwezi kuonana na mtu yeyote wa JF jamani?? Moyo unanikosea sana aise yaani unashindana na Kichwa khaa
Haki mie kuna muda JF huwa nashindwa kabisa kuielewa yaani kuna muda unaweza kuta watu wanachat kama wanajuana kuna muda unakuta wanachat kama hawajuani unashindwa kuelewa unabaki na mfurugano na hapo ndipo moyo wako unapokusuta na kukuambia "mind your own business young lady"
halafu kuna mtu (me) tunafahamiana aliwahi kukuta nachat na mtu humu (ke) kama tunajuana vile akanifuata inbox kuniuliza kama mimi na huyo dada tunajuana na mimi vyenye akili zangu nazijua mwenyewe nikamuambia ndiyo tunajuana kabisa
Akasema nimtumie namba yake na picha yake nikamuambia siwezi kupa bila ridhaa yake muombe mwenyewe akaniuliza yukoje nikaanza kuelezea yuko hivi na hivi basi ndiyo akazidi kuchanganyikiwa kutaka kumfahamu kumbe wapi mie mwenyewe simfahamu hata robo