Grahams
JF-Expert Member
- Mar 19, 2016
- 18,844
- 57,504
Ni shida aisee!Sindano zake kali sana, ilibidi niingie gharama kutiwa na wageni kuepuka kusimwanga, maana nilikuwa mwenyewe najilaimu kosa la siku moja limeleta aibu, jamaa walichoma kasindano kadogo tu kamoja, then drip ( vile vidogo) ndani ya dk 10 kameisha, then kuna machine wakawa wana niweke kwenye kibofu hivi kama dk nne.. Kwa mda wa siku saba, ili wao kujirizisha ila ndani ya siku ya siku mbili ile hali ilipotea kabisa. Shida hii wao wanajua mlaji wa mizoga, kumbe wakati mwingine sio ila ndio ivyo huwezi jitetea 😂😂😂.. Kuna rafiki yangu tulikuwa nae chuo yeye alikuwa chronic hadi akawa anatembea na ka sindano ka kujidunga maana ilimla kisawa sawa
Wabebaji wa maradhi haya asilimia kubwa ni Wanawake na bahati mbaya kwao kutokana na maumbile wanaweza kujikuta wanakaa nalo hata miezi 3 hadi Mwaka bila kujijua, wakati Mwanaume ni ndani ya siku Moja tu tayari amejua.
Nisije kufunguka sana Vijana wakapata maswali Kwa Babu yao hapa kwamba inakuwaje na Umri wote huu nikawa Mhanga, hawajui kuwa Ukiona Nyani Mzee ujue amekwepa mishale mingi 🤸🤸



