Ukitaka kuelewa hasa upekee wa huyu mwamba ni lazima uangalie muktadha na mazingira ya wakati huo. Na umlinganishe na mababa wa taifa wengine wa wakati huo...
Angeweza kufanya cho chote na kuiba anavyotaka kwa sababu hakukuwa na mtu ambaye angeweza kumhoji. Lakini hakufanya hivyo. Hata watoto wake hawakusoma Harvard na Cambridge japo wangesoma kama angetaka. Na angewatajirisha sana kama angetaka lakini leo wapo wanaishi maisha ya kawaida tu. Akina Madaraka. Akina Makongoro. Alikuwa mjamaa kabisa kabisa na aliamini katika falsafa zake za utu, usawa, umoja, uzalendo na kuheshimiana pamoja na kupeana haki bila rushwa na kujali matabaka.
Alitaka kila Mtanzania ajue kusoma na kuandika. Akapambana kufa na kupona kumaliza ukabila. Watu wake wawe wamoja. Waipende nchi yao....na alitaka ndoto hii ichomoze mpaka Afrika nzima. Tanzania ikawa kitovu cha harakati za ukombozi Kusini mwa jangwa la Sahara...
Mwalimu

