Sekretariet ya ajira katika utumishi wa umma inafanya kazi nzuri: Isiingiliwe, mapungufu tuyaainishe ili wayarekebishe.

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,037
Mazuri ya sekretarieti ya ajira kwenye utumishi wa umma:
1. Imejitahidi kuweka uwanja sawa kwa wote wanaotafuta ajira. Kama ni ugumu basi huo ugumu uko kwa wote!! Kinachotafutwa kwa sasa ni kutaka kuboreshwa uwanja kwa baadhi ya watu almaarufu kama "watoto wa wakubwa". Wanataka kuwapitishia mlango wa nyuma kupitia kinachoitwa eti WALIOJITOLEA WAPEWE KIPAUMBELE. Ieleweke kuwa ni watoto wa wakubwa tu ndio watapewa fursa ya kujitolea kwenye taasisi za serikali zenye maslahi mazuri kama TRA, BOT, NSSF nk
2. Imerahisisha sana namna ya kuomba ajira kupitia recruitment portal. Ukishaweka vyeti vyako huko huhitaji tena kila unapoomba ajira utambatanishe na vyeti!!
3. Kila mwenye sifa huwa anaitwa kwenye usaili hata kama ni wengi. Hii humpa fursa kila mwenye sifa ajaribu bahati yake. Hii inaondoa kabisa hisia ya rushwa! Wengine wamelalamika kuwa sekretarieti huwa inaita watu wengi sana! Lakini ni sawa kwa sababu kama sifa za msingi wanazo acha waje wachujwe kwa usaili.

Mapungufu ya Sekkretarieti ya ajira katika utumishi wa umma:
1.Kutokuweka wazi marks/alama za wasailiwa kwenye ngazi ya oral interview. Hii inasababisha hisia ya upendeleo. Tunawataka sekretarieti waweke waqzi pia alama za wasailiwa kwenye oral interview.
2. Kutokuweka wazi orodha ya wasailiwa ambao wamefaulu usaili lakini hawakupata nafasi na majina yao kuwekwa kwenye kanzidata/database kusubiri upatikanaji wa nafasi ya ajira. Tunawataka sekretarieti waainishe marks za wasiliwa wa oral kama wafanyavyo kwenye written interview. Na orodha ya kwenye kanzidata/database iwe wazi kwa kigezo cha marks za oral. Vinginevyo kanzidata inaweza kutumika kama mlango wa nyuma wa kupitishia watu kwa upendeleo maana hiyo database iko gizani kwa sasa!

Ushauri kuhusu mawazo ya baadhi ya watu (hasa watu wakubwa) kutaka sekretariet itoe kipaumbele kwa waliojitolea:
1. Tusiwatwike mzigo sekretariet kushughulika na watu ambao hawakuhusika katika kuteuliwa kwao kwenye kujitolea kwao. Kama tunataka kujitolea iwe ni sifa mojawapo ya kupata ajira, basi waomba ajira wote wapewe fursa ya kushindania kila nafasi ya kujitolea inapopatikana maana haiwezekani waombaji wote wapate hiyo nafasi ya kujitolea. Kwa hiyo haki ni kuwapa fursa wote kushindania hizi nafasi za kujitolea kwa kufanya usaili wa written na oral. Wanaofaulu wanaingizwa kwenye database na kupewa fursa ya kujitolea. Nafasi ya ajira ikitokea HAKUNA TENA HAJA YA KUWAFANYIA USAILI bali wanapewa ajira moja kwa moja toka kwenye database!!
2. Kila nafasi ya kujitolea ikipatikana LAZIMA itangazwe na wote wapate fursa ya kuiomba na kuifanyia usaili unaofanywa na sekretarieti. Viongozi serikalini na kwenye taasisi wasihusike kabisa kwenye kutoa nafasi ya kujitolea kwa watu ili kutokutoa mwanya wa rushwa na upendeleo.

NAOMBA USHAURI HUU UMFIKIE WAZIRI MWENYE DHAMANA NA UTUMISHI PIA UMFIKIE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAMA SAMIA H. SULUHU.

Tujihadhari maana tunataka kupigwa changa la macho kupitia mlango wa nyuma wa ajira kwa kujitolea!!
 
Tusitumie shida ya vijana ya kutafuta ajira tukawalazimisha kujitolea. Ni kuwanyanyasa, watalazimika kukubali kwa ajili ya shida lakini siyo sawa! Ikiwa lazima sekretariet ya ajira ihusike katika kutoa hizo nafasi za kujitolea kwa usaili!
 
Ninachikiona sharti la kujitolea ili mtu afikiriwe kwenye ajira litapanua sana mlango wa rushwa lisipotazamwa vizuri!!
 
Pamoja na ugumu uliopo tushukuru kuwa psrs wamejitahidi sana kuufanya uwanja wa kinyang'anyiro cha ajira kuwa sawa kwa kiasi kikubwa! Kuna watu wanataka kuleta utofauti ili lipatikane kundi la wateule watakaopewa kipaumbele kwenye ajira!! Hilo hapana. Inatumika lugha nzuri lakini nyuma yake kutakuwa na upendeleo sana!! Acha wote wapambane kwenye usaili wa psrs!! Kama mtu alijitolea basi huko kujitolea kumwezeshe kufaulu usaili, na si kumwezeshe kubebwa!!
 
PSRS pamoja na mapungufu tunayoyaainisha lakini kusema kweli mnastahili pongezi sana kwa kazi kubwa na ngumu mnayofanya. Kwa kiasi kikubwa sana mnajitahidi kutenda haki. Ninaamini hayo mapungufu mtayafanyia kazi!! Niwashauri tu kuwa wanaowasumbua na vimemo washitakini kwa mama Samia
 
Kati yamambo mazuri sana katika mchakato wa ajira ni PSRS kukataa kutambua TESTMONIALS. Hili linawakera sana wanaoitwa "wakubwa" maana ndio vinara wa kutoa testmonials letters kwa wateule wao. Haya mambo ya kujitolea ni kuturudisha kwenye testmonials ambazo nyingi ni za mchongo!!
 
Nampongeza sana kairuki ambaye naye alikataa kwenye mtego wa wabunge ambao waling'ang'ania sana eti walimu na manesi waliokuwa wanajitolea wapewe kipaumbele kwenye ajira kiduchu za walimu na manesi zilizotangazwa.Hakuna mtu yeyote Tz anayeweza kuacha shughuli zake za kutafuta maisha eti awe anajitolea .Nia ya wabunge ilikuwa ni kutengeneza loophole ya kuweza kuingiza watu wao kwa faida za kisiasa.Achane waombaji wa computer katika fair ground.
 
Nampongeza sana kairuki ambaye naye alikataa kwenye mtego wa wabunge ambao waling'ang'ania sana eti walimu na manesi waliokuwa wanajitolea wapewe kipaumbele kwenye ajira kiduchu za walimu na manesi zilizotangazwa.Hakuna mtu yeyote Tz anayeweza kuacha shughuli zake za kutafuta maisha eti awe anajitolea .Nia ya wabunge ilikuwa ni kutengeneza loophole ya kuweza kuingiza watu wao kwa faida za kisiasa.Achane waombaji wa computer katika fair ground.
Tatizo kubwa ni huyo RIZIONE KIk*eTE!! Amelikomalia sana suala kutoa kipaumbele kwa "waliojitolea". Tuwe wakweli kwa maisha haya magumu ni nani anaweza kujitolea kwa kufanya kazi bila malipo kwa mwaka mzima? Tusiwatese watu eti tu kwa sababu wana shida ya kupata ajira!! Watoto wa mafisadi wanaweza kujitolea maana watakuwa wanahudumiwa na pesa za umma zilizoporwa na wazazi wao, huku wakisubiria kubebwa!
 
Hao wabunge wanaotaka watu wajitolee waonyeshe mfano wa kujitolea. Muda wote wa bunge la kikao cha bajeti wasilipwe posho wala mshahara! Zile walizolipwa wazirudishe! Waone kama kujitolea ni kutamu!!
 
Tatizo kubwa ni huyo RIZIONE KIk*eTE!! Amelikomalia sana suala kutoa kipaumbele kwa "waliojitolea". Tuwe wakweli kwa maisha haya magumu ni nani anaweza kujitolea kwa kufanya kazi bila malipo kwa mwaka mzima? Tusiwatese watu eti tu kwa sababu wana shida ya kupata ajira!! Watoto wa mafisadi wanaweza kujitolea maana watakuwa wanahudumiwa na pesa za umma zilizoporwa na wazazi wao, huku wakisubiria kubebwa!
Tuna wabunge wasio na vision wanachoangalia ni kwa namna gani wanaweza wakatumia hizo ajira chache za kwenye public sector kama gear ya kuombea kura 2025.Kwa nini wasiishauri serikali iandaa mazingira wezeshi ya watu kuweza kujiajiri?
 
Nampongeza sana kairuki ambaye naye alikataa kwenye mtego wa wabunge ambao waling'ang'ania sana eti walimu na manesi waliokuwa wanajitolea wapewe kipaumbele kwenye ajira kiduchu za walimu na manesi zilizotangazwa.Hakuna mtu yeyote Tz anayeweza kuacha shughuli zake za kutafuta maisha eti awe anajitolea .Nia ya wabunge ilikuwa ni kutengeneza loophole ya kuweza kuingiza watu wao kwa faida za kisiasa.Achane waombaji wa computer katika fair ground.
Compete
Computer
 
Mazuri ya sekretarieti ya ajira kwenye utumishi wa umma:
1. Imejitahidi kuweka uwanja sawa kwa wote wanaotafuta ajira. Kama ni ugumu basi huo ugumu uko kwa wote!! Kinachotafutwa kwa sasa ni kutaka kuboreshwa uwanja kwa baadhi ya watu almaarufu kama "watoto wa wakubwa". Wanataka kuwapitishia mlango wa nyuma kupitia kinachoitwa eti WALIOJITOLEA WAPEWE KIPAUMBELE. Ieleweke kuwa ni watoto wa wakubwa tu ndio watapewa fursa ya kujitolea kwenye taasisi za serikali zenye maslahi mazuri kama TRA, BOT, NSSF nk
2. Imerahisisha sana namna ya kuomba ajira kupitia recruitment portal. Ukishaweka vyeti vyako huko huhitaji tena kila unapoomba ajira utambatanishe na vyeti!!
3. Kila mwenye sifa huwa anaitwa kwenye usaili hata kama ni wengi. Hii humpa fursa kila mwenye sifa ajaribu bahati yake. Hii inaondoa kabisa hisia ya rushwa! Wengine wamelalamika kuwa sekretarieti huwa inaita watu wengi sana! Lakini ni sawa kwa sababu kama sifa za msingi wanazo acha waje wachujwe kwa usaili.

Mapungufu ya Sekkretarieti ya ajira katika utumishi wa umma:
1.Kutokuweka wazi marks/alama za wasailiwa kwenye ngazi ya oral interview. Hii inasababisha hisia ya upendeleo. Tunawataka sekretarieti waweke waqzi pia alama za wasailiwa kwenye oral interview.
2. Kutokuweka wazi orodha ya wasailiwa ambao wamefaulu usaili lakini hawakupata nafasi na majina yao kuwekwa kwenye kanzidata/database kusubiri upatikanaji wa nafasi ya ajira. Tunawataka sekretarieti waainishe marks za wasiliwa wa oral kama wafanyavyo kwenye written interview. Na orodha ya kwenye kanzidata/database iwe wazi kwa kigezo cha marks za oral. Vinginevyo kanzidata inaweza kutumika kama mlango wa nyuma wa kupitishia watu kwa upendeleo maana hiyo database iko gizani kwa sasa!

Ushauri kuhusu mawazo ya baadhi ya watu (hasa watu wakubwa) kutaka sekretariet itoe kipaumbele kwa waliojitolea:
1. Tusiwatwike mzigo sekretariet kushughulika na watu ambao hawakuhusika katika kuteuliwa kwao kwenye kujitolea kwao. Kama tunataka kujitolea iwe ni sifa mojawapo ya kupata ajira, basi waomba ajira wote wapewe fursa ya kushindania kila nafasi ya kujitolea inapopatikana maana haiwezekani waombaji wote wapate hiyo nafasi ya kujitolea. Kwa hiyo haki ni kuwapa fursa wote kushindania hizi nafasi za kujitolea kwa kufanya usaili wa written na oral. Wanaofaulu wanaingizwa kwenye database na kupewa fursa ya kujitolea. Nafasi ya ajira ikitokea HAKUNA TENA HAJA YA KUWAFANYIA USAILI bali wanapewa ajira moja kwa moja toka kwenye database!!
2. Kila nafasi ya kujitolea ikipatikana LAZIMA itangazwe na wote wapate fursa ya kuiomba na kuifanyia usaili unaofanywa na sekretarieti. Viongozi serikalini na kwenye taasisi wasihusike kabisa kwenye kutoa nafasi ya kujitolea kwa watu ili kutokutoa mwanya wa rushwa na upendeleo.

NAOMBA USHAURI HUU UMFIKIE WAZIRI MWENYE DHAMANA NA UTUMISHI PIA UMFIKIE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAMA SAMIA H. SULUHU.

Tujihadhari maana tunataka kupigwa changa la macho kupitia mlango wa nyuma wa ajira kwa kujitolea!!
Hapo kwenye kujitolea Umeandika madini sana mkuu, mm nashauri hicho kigezo kifutwe kabisa kama mtu anataka kujitolea ni kwa hiyari yake sio eti kwa minajir ya kuajiriwa
 
Hapo kwenye kujitolea Umeandika madini sana mkuu, mm nashauri hicho kigezo kifutwe kabisa kama mtu anataka kujitolea ni kwa hiyari yake sio eti kwa minajir ya kuajiriwa
Kinachotakiwa ni kuungana kwa wingi na kulipinga jambo hili kwa nguvu zote!! Watalazimika kuyaheshimu makelele ya wengi!!
 
Mazuri ya sekretarieti ya ajira kwenye utumishi wa umma:
1. Imejitahidi kuweka uwanja sawa kwa wote wanaotafuta ajira. Kama ni ugumu basi huo ugumu uko kwa wote!! Kinachotafutwa kwa sasa ni kutaka kuboreshwa uwanja kwa baadhi ya watu almaarufu kama "watoto wa wakubwa". Wanataka kuwapitishia mlango wa nyuma kupitia kinachoitwa eti WALIOJITOLEA WAPEWE KIPAUMBELE. Ieleweke kuwa ni watoto wa wakubwa tu ndio watapewa fursa ya kujitolea kwenye taasisi za serikali zenye maslahi mazuri kama TRA, BOT, NSSF nk
2. Imerahisisha sana namna ya kuomba ajira kupitia recruitment portal. Ukishaweka vyeti vyako huko huhitaji tena kila unapoomba ajira utambatanishe na vyeti!!
3. Kila mwenye sifa huwa anaitwa kwenye usaili hata kama ni wengi. Hii humpa fursa kila mwenye sifa ajaribu bahati yake. Hii inaondoa kabisa hisia ya rushwa! Wengine wamelalamika kuwa sekretarieti huwa inaita watu wengi sana! Lakini ni sawa kwa sababu kama sifa za msingi wanazo acha waje wachujwe kwa usaili.

Mapungufu ya Sekkretarieti ya ajira katika utumishi wa umma:
1.Kutokuweka wazi marks/alama za wasailiwa kwenye ngazi ya oral interview. Hii inasababisha hisia ya upendeleo. Tunawataka sekretarieti waweke waqzi pia alama za wasailiwa kwenye oral interview.
2. Kutokuweka wazi orodha ya wasailiwa ambao wamefaulu usaili lakini hawakupata nafasi na majina yao kuwekwa kwenye kanzidata/database kusubiri upatikanaji wa nafasi ya ajira. Tunawataka sekretarieti waainishe marks za wasiliwa wa oral kama wafanyavyo kwenye written interview. Na orodha ya kwenye kanzidata/database iwe wazi kwa kigezo cha marks za oral. Vinginevyo kanzidata inaweza kutumika kama mlango wa nyuma wa kupitishia watu kwa upendeleo maana hiyo database iko gizani kwa sasa!

Ushauri kuhusu mawazo ya baadhi ya watu (hasa watu wakubwa) kutaka sekretariet itoe kipaumbele kwa waliojitolea:
1. Tusiwatwike mzigo sekretariet kushughulika na watu ambao hawakuhusika katika kuteuliwa kwao kwenye kujitolea kwao. Kama tunataka kujitolea iwe ni sifa mojawapo ya kupata ajira, basi waomba ajira wote wapewe fursa ya kushindania kila nafasi ya kujitolea inapopatikana maana haiwezekani waombaji wote wapate hiyo nafasi ya kujitolea. Kwa hiyo haki ni kuwapa fursa wote kushindania hizi nafasi za kujitolea kwa kufanya usaili wa written na oral. Wanaofaulu wanaingizwa kwenye database na kupewa fursa ya kujitolea. Nafasi ya ajira ikitokea HAKUNA TENA HAJA YA KUWAFANYIA USAILI bali wanapewa ajira moja kwa moja toka kwenye database!!
2. Kila nafasi ya kujitolea ikipatikana LAZIMA itangazwe na wote wapate fursa ya kuiomba na kuifanyia usaili unaofanywa na sekretarieti. Viongozi serikalini na kwenye taasisi wasihusike kabisa kwenye kutoa nafasi ya kujitolea kwa watu ili kutokutoa mwanya wa rushwa na upendeleo.

NAOMBA USHAURI HUU UMFIKIE WAZIRI MWENYE DHAMANA NA UTUMISHI PIA UMFIKIE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAMA SAMIA H. SULUHU.

Tujihadhari maana tunataka kupigwa changa la macho kupitia mlango wa nyuma wa ajira kwa kujitolea!!
Umeandika vizuri ila ukweli Tume ya ajira ina mapungufu makubwa mwishoni kuanzia matokeo ya usaili wa oral ( mdomo) na hili jambo limefanywa makusudi ili waweze kuwapa ajira watu wao mwa upendeleo na tusiweze kuhoji.

Haisaidii kitu kam usaili wa mchujo unafanyika na maksi za wale waliofanya ambao hawana ndugu zao huko Tume zinatangazwa kwa haki na wanaitwa hatua ya pili lakini maksi za hatua ya pili hazitangazwi. Haiwasaidii kitu.

Hakuna excuse inayohalalisha kutotangaza matokeo kwa maksi zaidi ya loophole ya kufanya umafia kwenye selection.

Wabunge wetu kama mko humu tunaomba hili mlivalie njuga hatutaki sababu za visingizio.
 
Back
Top Bottom