Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Scotland: 'No vote' haina maana 'No change'

Mkuu Mkandara nakubaliana na wewe kuwa tunatakiwa tuwe na takwimu halisi za uchumi, ziwe wazi ili uelewe.

Lakini kabla ya kupata takiwmu kuna kitu kunaitwa equity na equality. Mchango wa wa Zanzibar kwenye muungano unafuata msingi wa Equity, yaani kubeba mzigo kutokana na uwezo wake. Bahati mbaya hata hilo haifanyi.

Lakini kwemnye kunufaika wanakuwa wa kwanza kusema wanataka equality, yaani nusu nusu. Wanataka idadi ya mabalozi wa Tanzania katika nchi za nje iwe sawa kwa wabara na wavisiwani, bila hata kujali proportion ya idadi ya watu au hata bila kujali mchango wao kwenye MoFA.....huwa nacheka sana nikisikia wanasema, nafasi za udhamini elimu ya juu (nusu kwa nusu) mabalozi wetu nje nusu kwa nusu(equality), lakini kwenye kuchangia gharama za kuendesha wizara hizo hata siku moja hawasemi nusu kwa nusu (wanataka equity).

Mkuu Mkandara litakuwa ni jambo la maana kama tukipata takwimu na kuziweka hapa uangalie wazi ndio utajua kuwa, ni vizuri ikiwepo Zanzibar na ikiwepo Tanganyika. Otherwise Zanizbar ife kama ilivyokufa Tanganyika.
Let me ask you a simple question,
Je, zanzibar ina "Potential" ya kukusanya 1 trillion Shs kwa mwaka?
 
Maine na California zinawakilishwa na Senators wawili kwa kila state.
State power is balanced by the Senate, kwa hiyo population itself is not a determinant of representation. Thats what you failed to explain, unless you purposely ommitted that fact, which is not only low, but a bit trashy.
Aaah! ndugu yangu utawaweza hawa. yaani wanashindwa kabisa kuelewa kwamba Bungeni ni mahala muswada, sheria na usimamizi wa serikali unakwenda kwa idadi ya wawakilishi kwa nchi. Sasa kweli Zanzibar ikiwa na wabunge 10 kuna kitu kitakachopitishwa kwa niaba yao (upigaji kura) zaidi ya bara kufanya maamuzi yote! Kuna umuhimu gani wa kupiga kura ikiwa haitapatikana akidi jambo ambalo wao wenyewe leo wanailalamikia CCM juu ya rasimu hii ya katiba jinsi CCM walivyowachezea rafu.

Mwambie hivi kama tungefanya inavyotakiwa kwa lugha yake basi ni upande wa Tanganyika ingetakiwa kuwa na wabunge wengi zaidi kwa sababu wabunge wale wale karibu 300 ndio wanatuwakilisha pande zote mbili, hivyo Znz wangekuwa na hao hao 83 bunge la Muungano na bara wangetakiwa wabunge 560 au zaidi kwa uwakilishi pande zote. Na hao hao California na Maine ina wabunge wake wengine ndani ya states zao mktk bunge la State hivyo ukijumlisha wote unapata wabunge wangapi?

Halafu basi sisi tuliwaambia hawa hawa toka mwanzo kwamba wamefanya makosa makubwa sana kumchagua Sitta, walifanya makosa kwenda kunywa juice Ikulu na tukasema tena wanafanya makosa kwenda bungeni kutokana na idadi ya wabunge wa CCM. mwisho wamefganya makosa kulisusia bunge, sisi tulionekana wajinga muda wote tusoitakia mema katiba Mpya. haya yakowapi, wamekwama sasa matusi yote Sitta, JK na CCM na sasa rasimu ya 3 wakati wao wenyewe ndio waloondoka Bungeni.

Alaa! kwani hatukuwaambia haya toka mwanzo? Yaani kila siku ni kulalamika tuu na kibaya zaidi hakuna hekima kubwa isotokana na USIKIVU (Listening) kwani mbora baina yetu ni yule anayependa sana kusikiliza kuliko kusema sana na ndio yanayowakuta wanasiasa wetu. maneno meengi lakini hawajui wanalolizungumzia..
 
Mkuu Mkandara
Idadi ya wabunge hai determine maamuzi kwa mfumo wetu wa bunge.
1. Zanzibar imepewa 2/3 katika masuala ya muungano. In other words ni 2/3 ya 84 au 2/3 ya 15 bado itabaki 2/3
2. Kuna wawakilishi 5 kutoka BLW wanoingia bunge la JMT. Hao wanabeba maamuzi ya wawakilishi wa znz ndani ya bunge

Hoja yetu kubwa ni kuwa, kwavile wanakuja kwa sababu mahususi ya znz na wamepewa prerogative power ya 2/3 si kama wabunge wa Mwanza au Kigoma, SMZ inawajibika kuwalipia wao na si JMT ambako hawana mchango.
Ni weird idea lakini ukitazama ukweli kuwa hawana mchango wowote, basi huo ungekuwa mchango wao.

Kobello, tunaposema znz ichangie hatuna maana ichangie sawa. Tunajua ukubwa wa uchumi wake.
Msome Bongolander kaeleza kinaga ubaga kuhusu dhana halisi. kama hawezi ku raise 1 trillioni,

Kuchangia kwa namna nyingine kunaweza kuwa kupunguza gharama anazobeba Mtanganyika.

Mfano, znz ina Maritime organization yake, hakuna sababu ada zake kule International maritime (IMO) zilipwe na solely Tanganyika huku znz ikikusanya mapato yasiyoingia muungano.

@Bongolander pia kazungumzia dhana ya wazanzibar kudai haki bila kuangalia uwiano au uwajibikaji.

Wznz wanataka fursa sawa, wanataka haki katika mgao. Je, wanawajibika kiasi gani katika muungano?

Mfano, kama miaka 30 Mchambuzi) kaonyesha na gavana kathibitisha hawachangii hata ile sehemu wanayopaswa, wapi wanapata haki ya kudai wasichochangia tena kwa usawa. Kumbuka kauli yao ya muungano wa haki na usawa

Leo wamedai asilimia 21 ya ajira, labda mtueleze ni formula gani imetumika kuwapa na kwanini formula hiyo isitumikekuchangia muungano.

Imefika mahali kwamba wanadai haki hata zisizowahusu.
Kwanini shirika lao la umeme likusanye kodi, bill ya umeme wa znz alipe Mtanganyika kwa kutumia jina la JMT. Hivi kama wangelipa bill zao, huo si mchango katika muungano kwa kumpungiza mtanganyika zigo nene analohema nalo mgongoni.

Na mwisho, Kobello, kama unaamini znz hawawezi kuchangia muungano, ni kwanini basi tumeungana.

Huwezi kusema suala la kuoleana maana Scotland na England wameoleana miaka 300 na bado walikuwa watengane.

Mchambuzi, hao wanaosema mikopo na misaada, lazima pia waeleze, deni la ndani la znz linalipwa na nani?
Wapi bajeti ya znz ina usalama na ulinzi, mambo ya ndani na nje.

Kwa maana kuwa deni la kukopa la Mtanganyika linatumika kwa huduma za znz kama ulinzi na usalama.
Je, deni lao ambalo Mtanganyika analipa kwa asilimia 90 kama ulivyosema, linatumikaje kwa Mtanganyika?
 
Mkuu hata Bongolander mwenyewe hailewi mahesabu inahitajika mhasibu hata kuwapa darasa zuri zaidi kwa sababu nyie Mnachukulia 10 -1= 9 yaani 10 za Muungano ukitoa 1 za Zanzibar zinazobakia ni za Tanganyika! lakini inavyoonyesha hizi ni za Muungano hamikubalini nalo.. Huu ndio mtazamo wenu lakini ukweli ni kwamba 10 - 1, hiyo moja ni kwa matumizi ya maswala ambayo Zanzibar ina mamlaka nayo, ambayo ni kidogo sana hivyo mambo mengi makubwa bado yapo kwenye Muungano na yanashughulikiwa na serikali hiyo. Hivyo nasi huku ktk hiyo 9 tutatoa yetu sawa na 1 ya Zanzibar kwa matumizi yetu kisha zile zilizobakia ndio kwa ajili ya kuendesha serikali ya Muungano.

Ukilitazama swala hili ki juu juu hutaelewa kamwe, hivyo ni muhimu sana kwa mwenye kuonyesha matumizi lazima atuonyeshe kwanza hesabu ya bara ktk mambo ambayo tuna mamlaka nayo tumetumia ngapi na zilizobakia zimegawanywa vipi kwa kuonyesha mfuko huo. Kwa hiyo 4.5 kutoka 100 sio swala la kusema tumeubeba mzigo, wakati uwekezaji wa fedha asilimia 95.5 ni ktk matumbo ya watu.
Mwenzetu unayejua uhasibu hebu tusaidie kidogo hili suala. ZNZ wamedai 21% ya ajira. Ni kigezo gani kimetumika kufikia hapo? Hizi ni hesabu hivyo tufafanulie mkuu. Halafu tutaendelea baada ya hapo.
 
Mwenzetu unayejua uhasibu hebu tusaidie kidogo hili suala. ZNZ wamedai 21% ya ajira. Ni kigezo gani kimetumika kufikia hapo? Hizi ni hesabu hivyo tufafanulie mkuu. Halafu tutaendelea baada ya hapo.
Kwani wanawake wanapodai 50% ya uwakilishi huwa wanatumia hesabu gani? Kuiomba serikali ajira kwa asilimia 21 ni wazo zuri hata kama mimi ningekuwa mwakilishi wa sehemu yoyote, hii ni kuitaka serikali i invest kwa watu kama wewe umelala unataka nao walale?

Idadi ya wabunge hai determine maamuzi kwa mfumo wetu wa bunge.
1. Zanzibar imepewa 2/3 katika masuala ya muungano. In other words ni 2/3 ya 84 au 2/3 ya 15 bado itabaki 2/3
2. Kuna wawakilishi 5 kutoka BLW wanoingia bunge la JMT. Hao wanabeba maamuzi ya wawakilishi wa znz ndani ya bunge
Mkuu nikwambie mara ngapi Bunge la Dodoma ni Bunge la Muungano zinapopigwa kura kutokana na MUUNGANO lazima kuwepo na kipimo kama hiki ktk makubaliano baina ya nchi mbili zilizoungana. Hivyo hata sisi tuna asilimia 2/3 ambayo ni wajumbe wengi kuliko wao ukitazama kwa jicho hilo. Hii nikuweka mfumo bora wa kufikia makubaliano baina ya pande mbili sio swala la ukubwa wa nchi.

2. Kuna wabunge wangapi kutoka vyama vya bara sijui wanawake, vilema na kadhalika ambao hawakuchaguliwa na wananchi mbona haongezi hesabu zao. Kuna wengine wa rais mwenyewe, mawaziri na hata vyama ambavyo hata havikushinda uchaguzi mkuu mbona huzungumzii hilo!. Bara tuna watu wasohitajika walobebwa wengi tu (kwa sababu maalum) ukijumlisha wote na wako bunge la muungano, hii kutokana na maagizo ya katiba yetu na kama hukuiafiki ulitakiwa ukae Bungela katiba mpya kulipiga vita na sio vita ya upande mmoja tuone kama ungefika mahala popote.
 
Kwani wanawake wanapodai 50% ya uwakilishi huwa wanatumia hesabu gani? Kuiomba serikali ajira kwa asilimia 21 ni wazo zuri hata kama mimi ningekuwa mwakilishi wa sehemu yoyote, hii ni kuitaka serikali i invest kwa watu kama wewe umelala unataka nao walale?

Mkuu nikwambie mara ngapi Bunge la Dodoma ni Bunge la Muungano zinapopigwa kura kutokana na MUUNGANO lazima kuwepo na kipimo kama hiki ktk makubaliano baina ya nchi mbili zilizoungana. Hivyo hata sisi tuna asilimia 2/3 ambayo ni wajumbe wengi kuliko wao ukitazama kwa jicho hilo. Hii nikuweka mfumo bora wa kufikia makubaliano baina ya pande mbili sio swala la ukubwa wa nchi.

2. Kuna wabunge wangapi kutoka vyama vya bara sijui wanawake, vilema na kadhalika ambao hawakuchaguliwa na wananchi mbona haongezi hesabu zao. Kuna wengine wa rais mwenyewe, mawaziri na hata vyama ambavyo hata havikushinda uchaguzi mkuu mbona huzungumzii hilo!. Bara tuna watu wasohitajika walobebwa wengi tu (kwa sababu maalum) ukijumlisha wote na wako bunge la muungano, hii kutokana na maagizo ya katiba yetu na kama hukuiafiki ulitakiwa ukae Bungela katiba mpya kulipiga vita na sio vita ya upande mmoja tuone kama ungefika mahala popote.
Mkuu hujajibu swali, unachofanya ni hadithi.

1. Ni kigezo gani kimetumika kupata asilimia 21 ya ajira? Wewe umesema hatujui hesabu za std 7, na hilo si kosa ni mapungufu yetu. Sasa wewe unayejua hebu tueleze hizo zimepatikana kwa kutumia kigezo gani.
Niamshe mkuu, nimelela. Hakuna hadithi wala tararira, ni swali na jibu. Kama huna jibu una mambo 2. kukaa kimya wenye hoja waongee au una hoja uweke jamvini

2. Hatupo hapa kulinganisha akina mama na znz. Wanawake na wabunge wa kuteuliwa wapo pande zote.
Hilo ni la kuangaliwa. Na hao akina mama na wa kuteuliwa wapo kwa kutumia katiba ya JMT, hawana kakatiba kao pembeni kama nchi au taifa. Tunaongelea hawa wanaowakilishi kata(watu 2,500)

Hata hivyo tuna hoji uhalali wa watu 84 wanaokuja kuwakilisha znz tu, I mean wapo kwa masilahi ya znz walipiwe na Tanganyika. Hawa kama ulivyosema wanakuja kwa mambo machache yanayogusa znz, kwanini Mtanganyika awajibike kuwalipia?
Mtanganyika analipia kwasababu hakuna mahali umetuonyesha mchango wao. Au ni mikopo ndio mchango wao


Hebu tuendelee hapo mkuu, hakuna sababu ya kutoka povu na kuandika kashfa, hoja ndizo zinatawala jamvi
 
Mkuu hujajibu swali, unachofanya ni hadithi.

1. Ni kigezo gani kimetumika kupata asilimia 21 ya ajira? Wewe umesema hatujui hesabu za std 7, na hilo si kosa ni mapungufu yetu. Sasa wewe unayejua hebu tueleze hizo zimepatikana kwa kutumia kigezo gani.
Niamshe mkuu, nimelela. Hakuna hadithi wala tararira, ni swali na jibu. Kama huna jibu una mambo 2. kukaa kimya wenye hoja waongee au una hoja uweke jamvini

2. Hatupo hapa kulinganisha akina mama na znz. Wanawake na wabunge wa kuteuliwa wapo pande zote.
Hilo ni la kuangaliwa. Na hao akina mama na wa kuteuliwa wapo kwa kutumia katiba ya JMT, hawana kakatiba kao pembeni kama nchi au taifa. Tunaongelea hawa wanaowakilishi kata(watu 2,500)

Hata hivyo tuna hoji uhalali wa watu 84 wanaokuja kuwakilisha znz tu, I mean wapo kwa masilahi ya znz walipiwe na Tanganyika. Hawa kama ulivyosema wanakuja kwa mambo machache yanayogusa znz, kwanini Mtanganyika awajibike kuwalipia?
Mtanganyika analipia kwasababu hakuna mahali umetuonyesha mchango wao. Au ni mikopo ndio mchango wao


Hebu tuendelee hapo mkuu, hakuna sababu ya kutoka povu na kuandika kashfa, hoja ndizo zinatawala jamvi
Kwani hesabu zilizokupa ni zipi kiais kwamba uchanganye ujazo na wingi? nilichokwambia ni jinsi ya mgawanyo wa mapato unavyoweza kuwa kwa wale wanaofikiria kwamba 10-1 kicnachobakia ni cha Tanganyika, haya ya ubunge yanatoka wapi kwani ukiw ana wabunge wengi ndio mgawanyo utaongezeka.

Kwani wajumbe wa BLW hawapo katika katiba? ebu nenda sura ya tatu sehemu ya pili ya katiba (Bunge) uisome vizuri na unambie kifungu cha 78 na 79 vinasema nini. na Umeenda umoja wa wanawake kujua kwamba hawana katiba yao? katiba nini hata shirika lina katiba iwe Zanzibar. Katiba ni mwongozo tu mkuu wangu, watu hawajiendei hovyo pasipo dira. Yaani wewe unaandika tu madudu bila kuijua katiba yako.. hatari kubwa hii.
 
Copy and paste au weka link.... ili tujue source ni ipi na tuwe na easy accessibilty.
Copying and pasting is better than printing your own data....
because you know damn well the total revenue of "Sindiga" annually is not close to a trillion Shillings. C'mon brah!!

Mchango wa singida kwa pato la taifa na mchango wa singida kwa Mapato ya kodi kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa mtazamo wako, nini tofauti ya analysis? Maana naona sasa tuanze kufundisha vidudu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mchambuzi,
Iwapo hadi mwaka 1979, Tanganyika ilijulikana Kama Tanzania Bara na Zanzibar Kama Tanzania Visiwani, kwanini nMshirika mmoja wa muungano - Zanzibar hakurudishiwa jina lake halisi sambamba na Tanganyika? Mkandara, ebu tusaidie Katika hili. Kwa maana nyingine mkuu mkandara, kwanini katika kipindi chote cha miaka 50 ya muungano, Zanzibar kapitia majina ya Tanzania Zanzibar na Tanzanka visiwani, Kabla ya kurejeshwa Kama Zanzibar lakini Haki hiyo Tanganyika haikuipata?
Kwa sababu Tanzania leo hii ndilo jina letu tunalotumika nje, Ukisafiri kwenda Dar kutoka nchi yoyote tunasema naenda Tanzania na najivunia jina hilo. Ukitaka kuzungumzia ya ndani hata wewe nakwita Mchambuzi hutaki na wala hujarudisha jina lako halisi na unaeleweka kuwa mchambuzi nani, na ndio muhimu kwetu sisi. Zaidi ya hapo nimeshakwambia mimi niko vizuri sana na Tanzania ikiwa hao Zanzibar watajitoa ktk Muungano huu mimi bado naona jina hili libakie kwetu kwani wamejitoa wao likiwa na maana ya Tanganyika na Azania, ushindi wetu..
 
Kwani hesabu zilizokupa ni zipi kiais kwamba uchanganye ujazo na wingi? nilichokwambia ni jinsi ya mgawanyo wa mapato unavyoweza kuwa kwa wale wanaofikiria kwamba 10-1 kicnachobakia ni cha Tanganyika, haya ya ubunge yanatoka wapi kwani ukiw ana wabunge wengi ndio mgawanyo utaongezeka.

Kwani wajumbe wa BLW hawapo katika katiba? ebu nenda sura ya tatu sehemu ya pili ya katiba (Bunge) uisome vizuri na unambie kifungu cha 78 na 79 vinasema nini. na Umeenda umoja wa wanawake kujua kwamba hawana katiba yao? katiba nini hata shirika lina katiba iwe Zanzibar. Katiba ni mwongozo tu mkuu wangu, watu hawajiendei hovyo pasipo dira. Yaani wewe unaandika tu madudu bila kuijua katiba yako.. hatari kubwa hii.
Haya tuache hayo ya wabunge kwanza ili tusipate nafasi ya kukimbia hoja zinazohitaji majibu

Asilimia 21 ya ajira, ni kigezo gani kimetumika?
Na ile asilimia 79 ya Tanzania, wznz nao wanaruhusiwa?

Ni kigezo gani kimetumika kupata asilimia 21, kuanzia hapo tutakwenda mbele taratibu.
 
Mchambuzi,
Kwa sababu Tanzania leo hii ndilo jina letu tunalotumika nje, Ukisafiri kwenda Dar kutoka nchi yoyote tunasema naenda Tanzania na najivunia jina hilo. Ukitaka kuzungumzia ya ndani hata wewe nakwita Mchambuzi hutaki na wala hujarudisha jina lako halisi na unaeleweka kuwa mchambuzi nani, na ndio muhimu kwetu sisi. Zaidi ya hapo nimeshakwambia mimi niko vizuri sana na Tanzania ikiwa hao Zanzibar watajitoa ktk Muungano huu mimi bado naona jina hili libakie kwetu kwani wamejitoa wao likiwa na maana ya Tanganyika na Azania, ushindi wetu..
Mkuu mbona ukiulizwa maswali hutoi majibu? Jamvi linahitaji majibu.

Swali ni hivi, wakati Tanzania uilipokuwa Tanzania bara na visiwani, wale wa visiwani wakarudishiwa jina la Zanzibar.Kwanini hawa wa bara hawakurudishiwa jina la Tanzania.

Hayo ya kujivunia ni yako binafsi, tunaongele mambo ya taifa. Hatuongelei nani anajivunia ubondei au Ukara.
Jibu maswali, huna jibu kaa kimya wenye nayo wajibu. Weledi si kuandika hata kujifunza ni weledi pia.
 
Haya tuache hayo ya wabunge kwanza ili tusipate nafasi ya kukimbia hoja zinazohitaji majibu

Asilimia 21 ya ajira, ni kigezo gani kimetumika?
Na ile asilimia 79 ya Tanzania, wznz nao wanaruhusiwa.

Ni kigezo gani kimetumika kupata asilimia 21, kuanzia hapo tuatkwenda mbele taratibu.
Hakuna Hesabu zinzotumika isipokuwa ni moja ya mbinu za uwezo wa kujenga hoja kwa sababu nenda kazitazame wizara zao na mambo wanayoshughulikia halafu utaona kwamba ipo haja kubwa ya kuwaongezea mamlaka laa sivyo ndio gharama zake hizi. kwani hiyo serikali zote ina watumishi wangapi hawafiki hata laki 4, ajira zinapatikana toka mashirika binafsi na ndizo tunazijenga zaidi ya utumishi wa serikali. Kama kuna viongozi bora wawajibikaji kutoka Zanzibar hata iwe asilimi 50 sintojali kwa sababu hawa wote wanafanya kazi chini ya mwongozo wa katiba mama wakiitumikia serikali ya Muungano. Nikimyima yeye kwa sababu ni Mzanzibar ndio tunarudi kule kule kwenye Kula nyama ya mtu, watapewa kina Chenge yatakuwa mabaya zaidi kuliko Mzanzibar.

Sasa nakupa majibu nya kihuni...
Hivi unafikiri kwa nini wenye mashirka binafsi wanapenda kuajiri Wakenya? ni kwa sababu sisi hatuna nidhamu kazini, wezi, wazembe na tunataka Utajiri wetu utoke humo humo. Mimi naafiki kabisa kuwaajiri Wazanzibar kuliko Wabongo maana kila mtu mchumia tumbo na kihulka ni sifa kuiibia serikali.
 
Kwani wajumbe wa BLW hawapo katika katiba? ebu nenda sura ya tatu sehemu ya pili ya katiba (Bunge) uisome vizuri na unambie kifungu cha 78 na 79 vinasema nini. na Umeenda umoja wa wanawake kujua kwamba hawana katiba yao? katiba nini hata shirika lina katiba iwe Zanzibar. Katiba ni mwongozo tu mkuu wangu, watu hawajiendei hovyo pasipo dira. Yaani wewe unaandika tu madudu bila kuijua katiba yako.. hatari kubwa hii.
Kama katiba ni mwongozo hata mashirika wanayo, hebu tuambie shirika gani lililowahi kuvunja katiba kama znz walivyofanya 2010? Na pili, mwongozo gani unaomuondolea Rais madaraka tuna ufaninisha na wa KIUTA au UFI?

Una maana katiba ya znz ni sawa na Standard operating procedure ya CHIBUKU(SOP)! Mkuu hapo usinitaje maana huko mwembe ladu, kibanda maiti na kwa mtipura watu wanachemka damu.

Anyways, mkuu hao akina mama na wa kuteuliwa tumeshasema ni mzigo. Hilo halihalalishi tubebe zigo la watu 84 kwa bilioni 126 wanaokuja kutete nchi yao nzuri na mwanana ya znz.

Hospitali ya muhimbili inalaza wagonjwa 800 kwa wakati mmoja na siku moja. Kwa mgao wa bilioni 100 kwa miezi 3 wakati kuna watu 84 na wake zao wanakuja Dodoma kupiga domo na soga wakilipwa bilioni 126 ni pathetic, sidhani mwenye akili timamu anaweza kuliona sawa achilia mbali kulitetea.

BLW lina wajumbe 50 kwasababu wanalipwa na SMZ(ingawa zinatoka hazina Dar). Kwavile hawana uchungu na kodi za Watanganyika, wameamua kutuletea watalii 84 kudai IGP aliyezaliwa znz kwa miaka 5. Tunawalipa bilioni 126!!

Mkuu, tuambie asilimia 21 za ajira za wznz katika muungano zimepatikana kwa kigezo gani?
Nini uhalali wa ajira hizo?
 
Hakuna Hesabu zinzotumika isipokuwa ni moja ya mbinu za uwezo wa kujenga hoja kwa sababu nenda kazitazame wizara zao na mambo wanayoshughulikia halafu utaona kwamba ipo haja kubwa ya kuwaongezea mamlaka laa sivyo ndio gharama zake hizi. kwani hiyo serikali ina watumishi wangapi hawafiki hata laki 4, ajira zinapatikana toka mashirika binafsi na ndizo tunazijenga zaidi ya utumishi wa serikali. Kama kuna viongozi bora wawajibikaji kutoka Zanzibar hata iwe asimlimi 50 sintojali kwa sababu hawa wote wanafanya kazi chini ya mwongozo wa katiba mama wakiitumiia serikali ya Muungano. Nikimyima yeye kwa sababu ni Mzanzibar ndio tunarudi kule kule kwenye Kula nyama ya mtu, na atapewa Chenge yatakuwa mabaya zaidi kuliko Mzanzibar.

Sasa nakupa majibu nya kihuni...
Hivi unafikiri kwa nini wenye mashirka binafsi wanapenda kuajiri Wakenya? ni kwa sababu sisi hatuna nidhamu kazini, wezi, wazembe na tunataka Utajiri wetu utoke humo humo. Mimi naafiki kabisa kuwaajiri Wazanzibar kuliko Wabongo maana kila mtu mchumia tumbo na kihulka ni sifa kuiibia serikali.
Umekubali kuwa hakuna hesabu za kupata asilimia 21.

Hivyo hakuna hesabu ya wznz kudai chochote, si kwasababu hakuna hesabu bali hawana mchango.

Haya ya uzmebe wa kuajiri Wakenya ni kutuondoa katika mada. Huna data za kwanini wzn ni wazuri kuliko Watanganyika.
Hata hivyo uzembe wa Tanganyika haulalishi wznz kupewa asilimia 21

Asilimia 21 ni kuonyesha kuwa tunawapa hisani ambazo wanadai kama haki. Kiburi cha kipumbavu the least to say

Pili, 21% ina justify kuwa znz hawana sababu za kudai, wanaweza kuomba.

Tatu, 21 inaonyesha jinsi tunavyowaumiza Watanganyika ndani ya nchi yao
1. Kuwalipia ada za kusoma bure
2. Kuwatengea asilimia 21 kwasababu tu ni wazanzibar na si Watanzania.

Nne, hao unaosema wana haki kama wznz si kweli. Wazanzibar ni taifa, lina serikali yake, na vyombo vyake vilivyoweka ubaguzi dhidi ya Mtanganyika na wala si Mkenya wala Mnigeria. Hii roho ya chuki, umimi na inda ndiyo tunaiweka wazi kwa Watanganyika. Katiba yao inasema wao si Tanzania ni wazanzibar.

Hatukubali tena kuwaumiza watoto wa nchi ya Tanganyika wanaosoma kwa mikopo ya kodi za baba zao kisha kuumizwa na raia wa nchi jirani ya zanzibar ambao hawautaki Utanzania.

Watanganyika mnaona jinsi neno Tanzania linavyowaumiza? Hata watetezi kama Mkandara hawana jibu kwanini asilimia 21, lakini wapo mbele kudai znz inaonewa.

Mkandara, swali linalofuata
Kwanini tuwalipe znz kodi ya PAYE?
 
Nimeipenda hii thread

Pamoja sana,,,!! Mijadala km hii ndio.imetushawishi wengi cc tujiunge JF sio upuuz unaondelea humu wa Vijana kuendesha maisha kwa malipo ya elf 7 Unakuta kijana anatokwa povu kutetea Ujinga sababu amewekwa kwapani kwa Mwanasisa,,,! Ukitaka uelewe angalia tangu Mjadala uanze hakuna aliekuja humu wako wanabisha kugawana wagombea wakushabikia,,!!
 
Nguruvi3 na Mchambuzi

You know what they say ndege wanaoruka pamoja utua mti mmoja (or somen similar in saying) argument zenu ziwe za administration ya serikari jumlisha uwakilishi ama mkiwa mnaongelea maswala ya maendeleo na michango ni kutoka kwa perspective za ndani ya Tanzania tu; na kitu kikubwa mnachokwepa ni jinsi muundo wa sasa unavyosababisha malalamiko ya baadhi ya wazanzibari ilihali nyie mnatumia takwimu za muundo huo huo kwenye masimango.

Kwanza kabisa let me declare my interest mimi si muumini wa serikari tatu, vilevile siafiki privileges au hongo ambazo Dodoma inatoa hili kubakiza muungano kwakuwa siamini kama ndio underlying causes za mgogoro sana sana kuongeza tu ukubwa wa serikari au kuweka quotas ambazo aziendani na misingi ya ajira au utaifa kama lengo ni equal rights kwa kila Mtanzania including getting the highest job in the country.

Nikirudi kwenye hoja zenu za takwimu kiuhalisia ingawa sijafanya verification yeyote ya namba za mchambuzi hila anakwepa ukweli wa mambo badala ya kuweka namba tu za michango ungeweka na source of that income on those regions halafu tuone kama kweli Zanzibar wana hizo resources na hawazitumii.

Nyongeza ya hapo nimejaribu kuingia kwenye sources za kimataifa zinazotowa takwimu za GDP ambapo ZnZ pekee aitambuliki so as other nationals in the unions elsewhere; lakini kikubwa kwenye mchango wa GDP yetu ni resources za bara sasa why doesn't Zanzibar contribute much as opposed to other nationals overall contribution in their unions.

Kama utafata takwimu tu tena ambazo bwana Mchambuzi anapenda kuzitumia unaweza kuamini ZnZ ni mzigo lakini kama ukipekua siasa za Tanzania unaweza kuona kuna umuhimu wa kutatua malalamiko ya Zanzibari through further devolutions economically maana hapo ndio msingi mkuu kwa sasa ata na kwa wao.

Kutokana na geographical composition ya Zanzibar kilimo kwao akina maslahi na wala awana hiyo ardhi ya kufanya exploitation, awana madini wala viwanda (kwa sasa) vya kusema wana uwezo wa kushindana na bara ili kuchangia sasa. With all those disadvantages bado wananyimwa nafasi ya kuchochea uchumi wao. For instances lately nchi tatu katika EA pekee wameweza pewa uero bonds totalling 3.1 billion dollars. Hela ambazo wanaenda wekeza kwenye miradi yao wewenye ya maendeleo.

Kati ya hizo hela Rwanda imeweza pata almost 400 millions, Tanzania tumepata $700 mills. kati ya hizo ni ngapi zinaenda ZnZ, nchi ambayo kutokana mazingira yake inabidi hii invest ili kuweza kushindana kimataifa katika soko la utalii wa ufukweni. Wakati bado tupo kweny muktadha huo huo Tanzania bara imewekeza kiasi gani cha fedha kwenye kilimo kwanza nationally na kiasi gani ZnZ imepata kwenye sector yeyote yenye kuchochea ajira kutokana na mazingira yake.

Ukienda nchi zingine kama huko Scotland serikari inawekeza strategically mbali na government investment kama kuweka ship yards huko na kufunga vile vilivyokuwa England yote ni kwa sababu ya kuchochea uchumi wa Scotland, bado uvuvi, bidhaa za kilimo na mambo mengi serikari ina encourage industries huko hili waweze jikwamua kiuchumi.

Kwa hivyo swala la unyonyaji pia linachangiwa na room to manouver in ZnZ, awawezi pata strategic partners internationally kwenye kuchochea maendeleo na wala awana fursa za kuweza tafuta ziada kwa mantiki ya investment zao. Haya maswala si ya kuweka maraisi wangapi kinacho itajika ni ubunifu kwenye ecenomic devolution wa kuwapa nafasi wazanzibari kuweza ku manipulate uchumi wao na kutoa mchango kitaifa ili kuboresha muungano. Wakiweza pewa nafasi hiyo ndio tunaweza pima kama kweli wanataka muungano ama la kwa sababu wanafursa za kuchochea maendeleo na tunaendelea mbele vipi kama taifa, hongo pekee sio solution kwa sababu kero bado zipo pale pale ilihali sababu zetu za kuungana ni legitimate kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Mchango wa singida kwa pato la taifa na mchango wa singida kwa Mapato ya kodi kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa mtazamo wako, nini tofauti ya analysis? Maana naona sasa tuanze kufundisha vidudu.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Tax and non tax revenues... zipo openly kwenye website ya TRA.
Singida haichangii hata 5billion SHS, let alone 996 billion Shs.
Hebu nifundishe nielewe.
 
Let me ask you a simple question,
Je, zanzibar ina "Potential" ya kukusanya 1 trillion Shs kwa mwaka?

If well managed sure yes, but you know well that uswahili umejikita zaidi Zanzibar kuliko mainland. sisi tuna management mbaya lakini Zanzibar ni mbaya zaidi

Leave alone issue ya kama wanaweza kukusanya au hawawezi. Muhimu ni kuwa wanatakiwa kutambua kuwa wana wajibu na haki, sio haki tu. Tatizo ni kuwa wako mstari wa mbele kwenye kuangalia haki, lakini hata kidogo hatusikii kuzungumzia wajibu.

Linapokuja suala la wajibu inayozungumzwa zaidi ni Mainland, au inapokuja wakati wa opportunities wanakuwa na sauti kubwa sana kwenye equality, lakini kwenye suala la responsibilities hata equity hakuna.
 
Back
Top Bottom