Sasa mkuu wangu fedha za kutoka nje ulitaka zidhaminiwe na nani? na Je ikiwa serikali 3 fedha hizi zitadhaminiwa na nani? sii ndio maana ya muungano ama kuna maana nyingneyo ambayo ulitaka wewe mikopo ya fedha za mendeleo kutoka nje zidhaminiwe na serikali ndogo!.
Ebu Rudia swali lako Katika muktadha wa nchi Mbili, serikali Mbili kisha urudi tuendelee na mjadala husika. Pia USiache kujadili gharama za muungano kwa sura ya:
1. Mapato.
2. Matumizi.
2. Uchangiaji.
Hiyo development budget ya bara ni kiasi gani cha fedha zake ni AID mbona hukuzungumzia hili?
.
Mbona Nimesema hapo juu Kwamba haivuki 30%. Lakini Kama unataka thamani kwa shiliingi, vyanzo vya fedha za bajeti 2013-14 kwa mfano ilikuwa ni jumla la shillingi trilioni 18.2 Kama ifuatavyo:
1. Misaada na mikopo nafuu ya kibajeti. 7%.
2. Misaada na mikopo nafuu ya miradi ya maendeleo 15%.
3. Mikopo ya nje ya kibiashara 7%.
Vyanzo vya nje ilikuwa ni 28% ya bajeti yote tofauti na upotoshaji wa
Barubaru Kwamba hadi Leo tunategemea fedha za nje asilimia 40, sijui 60...;
Kwa mwaka huu wa fedha (2014-15), mikopo mipya ya nje ni shillingi 2.7 trillion, sawa na 14%.
na bajeti yetu ni mara ngapi ya ile ya Zanzibar kwa ukubwa?
Bajeti ya Zanzibar (shillingi trilioni 700 na ushee) ni 35% ya bajeti ya muungano which stands at 19.8 trillion shillings. Bajeti ya Zanzibar Ipo Katika muktadha wa fiscal autonomy, Ina Mapato ambayo hayamhusu mtanganyika. Badala ya kuwa wabunifu Kama Tanganyika kupunguza aid dependence, ubunifu wao ambao na wewe unawatetea ni more aid dependence kwa Zanzibar. Nimeuliza, nchi gani duniani imefanikiwa kupitia foreign aid?
Tukija kwenye bajeti ya muungano, hii ni ya watanzania (Tanganyika + Zanzibar), ambayo inagharamiwa na mtanganyika aliyebeba koti la muungano. Do I need to say more?
Zanzibar imeacha kuchangia kutokana na kutokuwepo mfuko wa Muungano, mfuko ambao sio sehemu ya mapato juu ya maswala ya maendeleo umedhihirisha. Ni swala la Kimfumo lilopangwa na huwezi kusema zanzibar ndio mkosa wakati Tanganyika yenyewe haichangii mfuko huo maana haupo.
Hakuna anayesema Zanzibar Ina Makosa, ebu tuonyeshe wapi Mimi Najenga hoja hiyo. Naomba niseme pia hili:
Mijadala yako juu ya kutokuwepo na mfuko wa pamoja huwa inapwaya sana kwani licha ya Ukweli wa kutokuwepo kwa mfuko huo, unashindwa kusema Kwamba JFC imekwama kwa sababu ni Vigumu kutenganisha Mapato ya muungano na Mapato ya Tanganyika. Jina Tanganyika unaliogopa mno. Vinginevyo sababu ya kitaalam, kiuchumi, world all over juu ya kukwama kwa JFC ni kutokuwepo kwa serikali ya Tanganyika. Haya ni marudio tu kwani I have explained this over and over again.
Na hata kama ukiwekwa kesho na tukaunda serikali 3 Tanganyika itagharamia zaidi kuliko ilivyo sasa. Kiswahili gani tuzungumze...
Wewe Ndio hauelewi Kiswahili Chetu. Let me repeat again Mara Mia moja - hatusemi Zanzibar wachangie kwa usawa na Tanganyika, basi Zanzibar wachangie kwa kiwango ambacho kitajadilika, Katika masuala machache yanayotakiwa kuwa ni ya muungano, na mengine nje ya muungano, kila upande ugharamie kwa urefu wa Kamba yake. Kwanini kwa miaka miwili sasa hauelewi lugha Rahisi namna hii?
Hata Marekani leo wana madeni ya matrillioni na haisemi nchi ngani ilosababisha madeni hayo bali chama gani na sera gani zimewafikisha hapo kisha ni serikali kuu inadhamini madeni hayo iweje utumie mfano huu wakati hata kwenye S3 ingelikuwa hivyo hivyo.
Naona unachagua hoja zangu zipo ujadili, Zipi ukwepe. Nimejadili awali Kwamba regardless of udogo wa states marekani, kila Raia nchini marekani Anachangia kwenye muungano in one way or another kupitia Mfumo wa kodi uliopo USA. Nilitaka hata aina ya kodi husika.
Mkuu hata sikuelewi kabisa, yaani mnachoandika ni vichekesho vitupu.
Hoja yoyote ya muungano kiuchumi lazima iwachekeshe wenye hoja za muungano kisiasa. Hii ni kwa sababu mtazamo wenu ni Kwamba uchumi unatakiwa kutumikia siasa.
Mlisema toka zamani kwamba Zanzibar ina fiscal auotonomy wakati Tanganyika haina, sawa - nikawauliza je Zanzibar ina fiscal auotonomy katika mambo gani? yaorodhesheni ili tuone kama Tanganyika ndani ya serikali ya Muungano haina mamlaka hayo, mkaingia mitini
kimyaaa...maana kipimo halisi sio maneno matupu bali ni mamlaka yenyewe yapo ama hayapo sio hadith za Alinacha.
Hili ni swali hopeless Kabisa, halina mantiki ndio maana huwa nalipuuza, huku wewe ukitafsiri kufanya hivyo ni kuingia mitini. Ngoja nikujibu basi Kidogo:
Ndio Zanzibar is fiscal autonomy to deal with her national development strategies and policies. Kwa mfano rejea mjadala wangu wa awali juu ya MKUZA, Vision 2020, zote kwa upande wa Zanzibar Wakati Katika suala la MKUKUTA na vision 2025, Zanzibar wapo pia Kama watanzania.
Your analysis becomes even more hopeless pale Unaposema Kwamba - unakubali Zanzibar Ina fiscal autonomy halafu hapo hapo unauliza hiyo autonomy ni Katika masuala gani, vipi mkuu, Mbona Unajichanganya hivyo? Mbaya zaidi ni Kwamba unasema Zanzibar Ina fiscal autonomy Kama ilivyo Tanganyika ndani ya serikali ya muungano, hivi hauoni Kama kukaa Kwangu Kimya kwa hoja mbovu Kama hizi ni kukutunzia heshima na sio kuingia mitini?
Sent from my iPhone using JamiiForums