Scandinavia Bus: Jamani nimelimiss hili basi...

Scandinavia Bus: Jamani nimelimiss hili basi...

Nini kiliiua hii kampuni ya mabasi??w

Kuna wengine wanasema ni 'Politics', kwamba kuna vigogo walikuwa na hisa zao mle, sasa waliziondoa.

Sababu za kifo cha Scandinavia (possible)
Ila mie nime-base zaidi kwenye uchumi. Scandinavia walikuwa na mikakati mibovu ya upanuzi wa soko.
1. Walikuwa wanasafirisha abiria wachache kwenda maeneo ya mbali, mfano basi la abiria 60 linasafirisha abiria 15 kutoka Dar hadi Arusha (650 km), au Dar hadi Kyela (1000 km), eti kwa sababu wanajali muda. Hii iliwagharimu sana, kwa sababu kusafirisha abiria kwa idadi hiyo ndogo kwa umabli huo ni hasara sana. Hilo hawakuliona, walijali muda zaidi.
2. Walijiingiza kwenye usafirishaji wa fedha na mizigo midogo (parcels) bila kujipanga. Mara nyingi sana walilazimika kulipia upotevu wa fedha na mizigo hiyo kutoka wizi wa wafanyakazi wao na ajali za mara kwa mara za magari yao, kutoka na huduma mbovu (poor vehicle services). Hili nalo liliwagharimu sana.
3. Walipanua masoko ya Uganda na Kenya bila kujipanga (waliongeza mabasi na routes) bila kuwa na mkakati wa kuimarisha routes zilizopo. Ushindani ukawa mkubwa, kwa hiyo wakawa kicked out of the market.
Matokeo yake, suppliers wa mabasi, mafuta, magurudumu na vipuri wakaanza kudai madeni yao, ambayo yalipelekea mabasi mengi kupigwa mnada kufidia madeni.

All in all, hii ilikuwa ni moja ya kampuni kongwe kabisa za usafirishaji abiria na mizigo kwa nchi yetu, ilikuwa ni icon kubwa kwa nchi.
I stand to be corrected.
Nawasilisha

 
P ushawahi kulipanda hili??

attachment.php

si mchezo mkuu
 
hahahah na kuingizwa mabasi kama haya

setra%20s315nf%20bus%20azur.jpg
Naona hadi lina internet ndani yake!! Full wifi mwanzo mwisho, liko connected na satelites, DSTV, EPL hukosi hata ukiwa polini! raha hii bongo jamani!
 
Nakumbuka hili lilikuwa la mwanzoni (UJIO WA PILI),
hii ilikuwa ni miaka ya 1997/98 Mnazi Mmoja Scandnavia waliondoa gari wakiwa na abiria sita tu, nikiwa mmoja wao.
Ilipata vikwazo vingi sana lakini hatimaye wakaja ku lead market
P ushawahi kulipanda hili??

attachment.php
 
Nakumbuka hili lilikuwa la mwanzoni (UJIO WA PILI),
hii ilikuwa ni miaka ya 1997/98 Mnazi Mmoja Scandnavia waliondoa gari wakiwa na abiria sita tu, nikiwa mmoja wao.
Ilipata vikwazo vingi sana lakini hatimaye wakaja ku lead market

na kabla ya hapo mkuu nikiwa mdogo walikuwa na zile Leyland DAF enzi za Fresh ya Shamba, Kwacha, Zainabu.. wakati huo wanapiga route za Mbeya - Dar
 
na kabla ya hapo mkuu nikiwa mdogo walikuwa na zile Leyland DAF enzi za Fresh ya Shamba, Kwacha, Zainabu.. wakati huo wanapiga route za Mbeya - Dar

Yes.
Nadhani ni late '70s na '80s ndo sababu hapo juu nikasema ni aibu kwa kampuni kama hizi kufifia katika soko. Wametoka mbali sana kibiashara. Zainab's walifilisika mnamo 2002, Fresh ya shamba sina uhakika sana, ila amebadili biashara kwa sasa.
 
scandnavia ilikuwa ndio mpango mzima,kwanza sehemu yao ya kupandia bus na kutelemkia ilikuwa kama mwl nyerere intl airport,walitishaje!! sasa hivi bado sijaona bus ambalo lilitoa huduma kama scandnavia,kwanza ndani ya bus ukuweza kuchoka adi safari unaiona fup
 
Imetoka kivingine, inaitwa Green Star inatumia magari aina ya Yutong, sio Scania Marcopolo tena.
Precisely mkuu!ni Green Star Express,tofauti ni rangi lakini huduma ni zilezile!
 
attachment.php


attachment.php


Nimelimiss sana hili bus, sijui lini hii kampuni itafufuka tena maana nakumbuka miaka ya nyuma iliwahi kupotea katika ulimwengu wa usafirishaji lakini baadae ikarudi tena...

Enzi za kuchimba dawa. Hivi siku hizi ukibanwa njiani inakuwaje
 
umenitouch sana katika hili nimesoma form one mpaka nimemaliza chuo kutokana na hii kampuni naijua in and out imag.jpg image.jpg images.jpg k.jpg Luxury_interior.jpg
nimechukua wanawake wengi sana kupitia hii kampuni nimefanya mambo mengi tu kupitia hii kampuni
 
Back
Top Bottom