SAUTI ya ALIYEBAKWA!

SAUTI ya ALIYEBAKWA!

Mjanga

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2011
Posts
1,238
Reaction score
325
Asalam aleikum, ni majira ya kuelekea kufunga mwaka 2012 na kuingia 2013;Happy new year to all!

Mwisho wa mwaka huu tunashuhudia mambo mazito ya kutia simanzi na majonzi mazito, katika yote linalovutia hisia za watu duniani ni hiki kifo cha mwanafunzi wa Udaktari aliyebakwa huko India, angalau wahindi wenzake wamepaza sauti na kuonessha ni jinsi gani wamechukizwa na tendo hilo huku moja ya bango likisomeka "REAL MEN NEVER RAPE"! na nyingine: "DEHLI IS THE HQ of RAPE" hii ni baada ya mtu mmoja tu kuwa mhanga! angalau dunia yote imeonesha masikitiko yake juu ya huyu dada: maswali mengi yanaibuka; je watu wanasikitika kwasababu victim alikuwa ni Daktari mtarajiwa, au kweli watu wameguswa?

Hoja yangu ya msingi ni: vipi waafrika Wanawake na Mabinti wanaobakwa kila kukicha, hata hapa kwetu tunaona kwenye magazeti; wale wanaobakwa huko Congo DRC; wale wanaobakwa huko Sudan na kwingineko? Jamii zetu za kiafrika wamefanya nini kuiambia dunia kwamba hatufurahishwi na jambo hili, wanaSIASA wetu wamefanya nini kuondoa hili tatizo, wahasi(wanaojiita wakombozi) na wadai haki wamefanya nini juu ya hili? Au kwa sababu ni wanawake wa mashambani wasio na thamani hivyo ni haki yao kubakwa??? Serikali zetu zinafanya nini?? au kwa kuwa ni Afrika kila kitu tunamwachia Mungu??

manake tunapojaribu kukemea matatizo kama rushwa, ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi: utawasikia viongozi wa kisiasa na wa kidini wakiandaa mikesha ya kuiombea taifa: hivi matatizo yetu yatatatuliwa na sala pekee??

Sauti ya Wanawake wa kiafrika wanaobakwa kila kukicha itapazwa na nani na lini????
 
dah kwa kweli hili tatzo tanzania inachangamoto nyingi sijui itakuwaje I dn knw jmn, ukienda hospital kitengo cha unyanywasaji na ubakaji wa kinjisia utapata matukio ya ajabu sana watu wanabaka hadi watoto wao
 
Ni muda muafaka sasa wa wanawake wa Afrika nao kuamka na kukemea kwa sauti moja huu unyama wanaofanyiwa.
 
Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi. Wanaume wanaruhusiwa kuwa WEAK pale ambapo viungo vya mwanamke vikiwa exposed. Huoni Swaziland wametunga sheria ya kupiga vita vimin na vitop; ila kupita kwa Mswati tu ndipo wanaporuhusiwa matiti kuwa nje!
 
Hawa watoto wa kike wanaobakwa kama ilivyo kwa wanafunzi wanaopigwa mimba, wanakutwa na maswahibu hayo kwa kiherehere chao"
 
Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi. Wanaume wanaruhusiwa kuwa WEAK pale ambapo viungo vya mwanamke vikiwa exposed. Huoni Swaziland wametunga sheria ya kupiga vita vimin na vitop; ila kupita kwa Mswati tu ndipo wanaporuhusiwa matiti kuwa nje!

Huyu mswati naye kazidisha tamaa sasa, yani anataka yeye tu ndo aone vimini loh
 
Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi.

Very sad!

Kuna kipindi humu kuna picha ya mwanadada mmoja ilionyesha akiwa kazongwa na kundi la wahuni Iringia mjini kisa tu eti kavaa sketi ambayo ilionekana kuwa ni kama zile underskirts.

Lawama alizopewa humu zilishangaza sana. Eti kosa lilikuwa lake kwa nini alivaa vile. Na wadada ndiyo walikuwa mstari wa mbele kumnanga.

Kwa hiyo unachosema kina ukweli mwingi tu. Blame the victim mentality imeshika hatamu kwenye sehemu kubwa tu ya jamii.
 
Very sad!

Kuna kipindi humu kuna picha ya mwanadada mmoja ilionyesha akiwa kazongwa na kundi la wahuniRingia mjini kisa tu eti kavaa sketi ambayo ilionekana kuwa ni kama zile underskirts.

Lawama alizopewa humu zilishangaza sana. Eti kosa lilikuwa lake kwa nini alivaa vile. Na wadada ndiyo walikuwa mstari wa mbele kumnanga.

Kwa hiyo unachosema kina ukweli mwingi tu. Blame the victim mentality imeshika hatamu kwenye sehemu kubwa tu ya jamii.

Hata pale inapochagizwa na Mkuu wa nchi utaona jinsi gani we have a long way to go
 
Kaunga kwani kuvaa vivazi vifupi unakaribisha wabakaji? na hawa wanaobakwa katika maeneo yenye uasi inakuaje?
Serikali imeshindwa je na raia nao wameshindwa??
Naamini kuwa siku zote serikali haiwezi kufanya mambo(mabadiliko) mpaka isimamiwe na raia wake!

Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi. Wanaume wanaruhusiwa kuwa WEAK pale ambapo viungo vya mwanamke vikiwa exposed. Huoni Swaziland wametunga sheria ya kupiga vita vimin na vitop; ila kupita kwa Mswati tu ndipo wanaporuhusiwa matiti kuwa nje!
 
Very sad of Baba Ritz! mzee wa kaya bana huwa anatoa tata kweli!!

Hawa watoto wa kike wanaobakwa kama ilivyo kwa wanafunzi wanaopigwa mimba, wanakutwa na maswahibu hayo kwa kiherehere chao"
 
Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi. Wanaume wanaruhusiwa kuwa WEAK pale ambapo viungo vya mwanamke vikiwa exposed. Huoni Swaziland wametunga sheria ya kupiga vita vimin na vitop; ila kupita kwa Mswati tu ndipo wanaporuhusiwa matiti kuwa nje!

we Mhindi nini?
 
mimi sidhani kama kuvaa nguo fupi ndiyo sababu ya kubakwa nahisi wanaume tumekuwa watu wenye tamaa.
Mbona zamani wanawake walikuwa wanatembea maziwa nje wamevaa nguo za asili lakini hakuna kubakana. Mbona bado kuna makabira afrika bado wanakaa uchi na hawabakani?
Being naked is a picture inside someones mind
 
Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi. Wanaume wanaruhusiwa kuwa WEAK pale ambapo viungo vya mwanamke vikiwa exposed. Huoni Swaziland wametunga sheria ya kupiga vita vimin na vitop; ila kupita kwa Mswati tu ndipo wanaporuhusiwa matiti kuwa nje!

Kinga ni bora kuliko ajali. Lazima tuwaelimisha watoto wetu na wadogo zetu kwamba kupendeza sio lazima uvae nguo fupi. Unaweza ukavaa vazi refu na ukapendeza vizuri. Kama tunajua kuna wanaume wanaochachawa kiasi cha kutamani kubaka wakiona wanawake wamevaa vimini na vitopu, basi sehemu ya suluhisho ni kujisitiri vizuri.

Ni kama vile unajua ukitembea usiku wa manane vichochoroni utakabwa na kuibiwa, ndo maana watu huwahi kurudi majumbani au kwenda kwenye shughuli zao. Dada zetu mnataka sisi wanaume tuweze kuzishinda hisia zetu, lakini mnasahau kwamba baadhi ya wanaume ni mateja na wavuta bangi-hana muda wala utashi wa ku-reason ktk namna mnayotaka. Trauma ya kubakwa ni kubwa sana, ni bora kuwa defensive kwa kujisitiri vizuri na kutokaa mazingira hatarishi.

Mwisho, ktk africa hakuna nchi inapiga mini na top kama sauzi! Madhara yake yanaonekana, takwimu za watu kubakwa sauzi zinatisha, ni kama kila dakika (kwa wastani)! Mim nawapenda dada zangu, pokeeni ushauri huu wa kujisitiri vizuri maana wengi wanaobaka wanakuwa hawako ktk hali ya kawaida (sababu ya drugs na bangi). Sio lazima tuige kila kitu wanachofanya wazungu! Kwa kujisitiri vizuri, jamii za pwani na waislam kwa ujumla nawapa heko.
 
mimi sidhani kama kuvaa nguo fupi ndiyo sababu ya kubakwa nahisi wanaume tumekuwa watu wenye tamaa.
Mbona zamani wanawake walikuwa wanatembea maziwa nje wamevaa nguo za asili lakini hakuna kubakana. Mbona bado kuna makabira afrika bado wanakaa uchi na hawabakani?
Being naked is a picture inside someones mind

Ndugu, tukianza na zamani, mgawanyo wa kazi ulikuwa tofauti na sasa. Zamani kazi zilikuwa za shuruba kama kuwinda kulima n.k. Hali sasa ni tofauti, kazi za shuruba zimepungua, mfano mpigadebe anaamka, anavuta bangi au unga then anaenda stendi kazi yake kuita abiria na kutukana au kupigana-mtu wa aina hii kubaka ni rahisi. Zamani kila sehem ilikuwa pori kubwa, kwahiyo hata kuonana haikuwa rahisi kama leo, sanasana utaonana na jirani yako-ambaye kwa aibu ya ubinadamu na kufahamiana ilikuwa ngumu kubaka. Leo tunabana kwenye daladala na watu ambao wamepiga vimini-na hapo ndipo tofauti inapokuja.

Ni kweli kwamba kuna jamii ambazo mwanamke anaweza akatembea titi nje bila kuleta shida kwa wanajamii wengine-jamii kama za wahadzabe, watindiga na hata wamasai. Lakini angalia wanaishi wapi? Wanaishi porini, msituni-sehemu ambayo haina muingiliano mkubwa wa watu, kama kariakoo! Na jamii za namna hiyo kila mtu yuko bize na kazi tofauti na mijini unakuta kijana au binti anazurura mitaan, ati anafanya matembezi ya jioni! Naomba isieleweke kwamba ni haki ya mwanaume kubaka akiona mwanamke yuko uchi, langu ni kwamba, trauma ya kubakwa ni kubwa sana na inaweza ikamsumbua mwanamke kwa miaka mingi, basi asijiweke kwenye mazingira hatarishi mfano kwenda kwenye shereha na kulewa kupita kiasi, kuvaa nusu uchi, kuchelewa kurudi nyumban usiku n.k.
 
Huku Africa mwanamke akibakwa amesababisha yeye; kwa kuvaa nguo fupi au nusu uchi. Wanaume wanaruhusiwa kuwa WEAK pale ambapo viungo vya mwanamke vikiwa exposed. Huoni Swaziland wametunga sheria ya kupiga vita vimin na vitop; ila kupita kwa Mswati tu ndipo wanaporuhusiwa matiti kuwa nje!
unazidi kuchemsha hasira zangu! Na kuna wanawake wanabakwa na bf ama waume zao wa ndoa. Na inaonekana ni haki. I love black brothers, but they can be really disgusting!
 
Kuwe na sheria maalum kwa ajili ya ubakaji, sheria izungumzie ubakaji kwa maana ya ubakaji na si kuiweka ndani ya sheria eti inaitwa ya kujamiiana,hapo ubakaji haupewi uzito unaostahili, haiwezekani Uuaji kupitia ubakaji uchanganywe na kukonyeza eti viwe pamoja.
Wakati umefika ambapo ubakaji utungiwe sheria yake na hukumu yake ambayo itahukumu tendo lenyewe. wanawake wanao uhuru wa kuvaa, huwezi kuhalalisha ubakaji eti kwa kuwa mwanamke kavaa nguo fupi then abakwe,basi ijulikane na leseni zitolewe kwa wabakaji wa wanawake wenye nguo fupi kama akiri zetu ni fupi kiasi hiki.
Tuutafsiri ubakaji kwa maana hasa ya ubakaji tuache mbwembwe za wanaharakati,jamii ya dunia nzima izinduke kuwaokoa wanawake na kuwalindi dhidi ya mafisadi wa miili yao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom