don-oba
JF-Expert Member
- Dec 8, 2011
- 1,387
- 680
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Mt. Augustine-Mwanza wamemtupia lawama mbunge wao mh. Wenje kwa kile kinachoelezwa kwamba amewatelekeza.
Ikumbukwe kwamba Mh Wenje wanafunzi wa SAUT ambao idadi yao ni zaidi ya 15000 ndio waliomwezesha kiasi kikubwa kupata ushindi. Pia ni hawa hawa wanafunzi ndio walikesha kwenye vituo kulinda kura zisichakachuliwe.
Chanzo cha kumtupia lawama mbunge wao Wenje ni kutokana na wanafunzi wenzao 215 hadi sasa semister imeisha hawajapata pesa zao za kujikimu kutoka bodi ya mikopo.
Inaelezwa kwamba uzembe mkubwa kutoka uongozi wa chuo na serikali ya wanafunzi SAUTSO inayojipambanua kwamba ni makamanda wapiganaji wameshindwa kufuatilia pesa za wanafunzi hawa kitendo kilichopelekea wawasiliane moja kwa moja na Wenje kupata msaada zaidi.
Lakini hadi sasa si Wenje ambaye amewapa taarifa juu ya hatima yao huku wakidai muda mwingine wakimpigia simu hapokei.Imefikia baadhi yao kuacha chuo, wengine wameanza kujiuza miili yao ili wapate pesa za kujikimu.
Ikumbukwe kwamba Mh Wenje wanafunzi wa SAUT ambao idadi yao ni zaidi ya 15000 ndio waliomwezesha kiasi kikubwa kupata ushindi. Pia ni hawa hawa wanafunzi ndio walikesha kwenye vituo kulinda kura zisichakachuliwe.
Chanzo cha kumtupia lawama mbunge wao Wenje ni kutokana na wanafunzi wenzao 215 hadi sasa semister imeisha hawajapata pesa zao za kujikimu kutoka bodi ya mikopo.
Inaelezwa kwamba uzembe mkubwa kutoka uongozi wa chuo na serikali ya wanafunzi SAUTSO inayojipambanua kwamba ni makamanda wapiganaji wameshindwa kufuatilia pesa za wanafunzi hawa kitendo kilichopelekea wawasiliane moja kwa moja na Wenje kupata msaada zaidi.
Lakini hadi sasa si Wenje ambaye amewapa taarifa juu ya hatima yao huku wakidai muda mwingine wakimpigia simu hapokei.Imefikia baadhi yao kuacha chuo, wengine wameanza kujiuza miili yao ili wapate pesa za kujikimu.