Mwendabure
JF-Expert Member
- Mar 10, 2011
- 2,138
- 1,040
Huu uzi ni muafaka sana. Heko mleta uzi!
Mi naona kila siku watu wanatafuna maneno yao wenyewe lakini Laigwanan anachanja mbuga. Kwa vile sehemu kubwa ya NEC ya CCM ilikuwa Arusha jana sioni uwezekano wa kutopitishwa kwa kuwa wanaCCM ni watu wa kuangalia upepo wa mafanikio ulipo na wanaenda huko. Kwa jeuri ya fedha aliyonayo EL na desturi ya CCM ilivyo, EL is now unstoppable. Only UKAWA to stop him
Unasahau kuwa EL ni miongoni mwao tena wa ndani Zaidi ... Kanisa Katoliki mikakati yake inajulikana na tayari Pengo anapigwa na wengi kwa kuonekana anaegemea upande wa ndugu yake Pinda ... Hawa watu wa Vatikan Pinda, Membe, Nchemba, wassira, Mwandosya, Mwakyembe, Magufuli, Sumaye et al wanajulikana syndicate yao na haihusiani na TISShata chembe... Ndani ya kitengo kina watu wenye weledi mpana ambao hautawaliwi na emotions za kibinaadamu Zaidi ya facts ambazo Kingunge ameziainisha kwa niaba ya JK ...
Tazama CC inayopitisha majina halafu utajua kama huyu bwana kapita au laa..,like it or not, wafanya maamuzi halisi CCM walijua hii siku itafika wakajizatiti.
huu mtifuano bado mmbichi sana. at the end of the day,this is very good news for UKAWA.
Kitu kimoja ambacho watu hawajui, au wanapotosha kwa makusudi ni nguvu ya NEC. NEC ndio inayochagua mwenyekiti, NEC inaweza kusema hatuna imani na mwenyekiti na atang`oka. Wataenda na mkwara huo kwa vile EL ashawapata tayari, kauli mbiu itakuwa kata jina la Lowassa tukuvue uenyekiti.
Namsikitia EL kwa kuwepo serikalini kwa zaidi ya miaka 30 thelathini lakini akashindwa kufahamu jinsi akina Apson wanavyofanya kazi na muundo wa kampuni yao ukoje. Kazi hiyo ya kumpoteza njia na kumpeleka asikokuhitaji ilianza mara tu JK alipoapishwa! Chezea kampuni wewe! Rais kwa mtizamo wangu japo simkubali ni yule ambaye tayari ana endorsement ya Kanisa Katoliki (tafuta picha za Cardinali Pengo wakati sherehe za Pasaka mwaka huu na zile Askofu Valentino Mokiwa kwenye maadhimisho ya miaka 100 ya Kanisa la Anglikani Tanzania). Halafu unganisha na dots zingine.
kuna issue ya mgombea binafsi ilisikika mdomoni mwake...kwa mawazo yangu sidhani kama anategemea ccm tu. miaka yote amekuwa anatafuta watu na ameshawapate. Inawezekana ccm ni option namba moja. Wakimkataa sidhani kama watakwamisha safari yake ya matumaini. Tusubiri tuone.
Tazama CC inayopitisha majina halafu utajua kama huyu bwana kapita au laa..,like it or not, wafanya maamuzi halisi CCM walijua hii siku itafika wakajizatiti.
huu mtifuano bado mmbichi sana. at the end of the day,this is very good news for UKAWA.
Naona mnaanza kuleta option D na C, mshajua option A na B ni ndoto.
hakuna mtu wa kumtoa JK kwenye uenyekiti wa CCM pale, msitegemee kina Pinda, Membe,mwakyembe, Sitta, Makongoro na CCM heavyweight wengine wakamtazama tu Lowasa.
Lowassa may be rich, but in terms of muscle inside CCM he is no bigger than the other folks combined.he knows that.
kuna issue ya mgombea binafsi ilisikika mdomoni mwake...
Nimeanza kuunganisha dots na kwa mbaali naiona picha kuwa kitendo cha Jasusi mkuu mstaafu wa nchi yetu kujiunga na kambi ya Lowasa kilikua ni cha kimkakati zaidi. Kwa wanaomfajamu Apson na utendaji wake tulijiuliza sana lakini tulikosa majibu.
Leo hii mara baada ya Edward kumaliza kufanya kampeni (Ninasisitiza kuwa ni kampeni na si kutangaza nia) yake pale uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ndipo nikazinduka na kutambua kuwa Apson alikua 'under cover' akiwa na jukumu maalum la kumdhoofisha Edward and Kingunge nailed it. Hili suala la magenge ya wasaka madaraka yaliyumbisha sana idara yetu ya usalama wa taifa kitu kilichopelekea idara hii kushutumiwa sana mitandaoni pia na makundi mbalimbali ya kijamii.
Ilikua si kazi rahisi kulimudu hili genge maana lilishajijenga vya kutosha na namna pekee ya kulisimamisha ilikua ni lazima the big man aingie in the war front and to begin with ilibidi ku step down then kujipenyeza ndani ya kambi hii ambapo na ku gain trust. Seems lengo la yeye kwenda front ilikua ni kulinda nguvu kazi ambazo idara hii ilikua ikizipoteza mara tu magenge haya yalipooa maslahi yao yanahatarishwa, (kujua zaidi unaweza ukarejea kingo za sakafu za mzee Kapinga na Daudi Mwakawago and others of a like zilipoishia).
Kwa kuwa magenge haya yanawakilisha maslahi mapana zaidi ya mataifa ya kigeni yanayoangalia namna ya kubena rasilimali zetu na yenye mitandao ya nguvu ya kijasusi, seems yali smell something fishy with Apson na hapo ndipo tukatangaziwa the return of The Kingmaker ambapo tukasikia kuwa Apson anawekwa kando (thou it was too late) kimtindo and the Kingmaker took over.
Kwa speech ya Edward na kila kitu kilichoendelea pale na kinachoendelea ndani ya kambi yake I can draw the conclusion kwamba the Game is Over. Ninaanza kupata hisia kuwa kutakuwa na transition kubwa zaidi mwaka huu.
Tanzania inarudi katika ubora wake, this is my country, I belong here. Hakika moyo wangu una furaha sana kuliko wakati wowote ndani ya miaka hii kumi. Si jambo dogo kuachia nafasi kubwa kama ile katika ofisi nyeti wakati muda ukiwa unamruhusu na kuamua kwenda under cover, hakika napata hisia idara yetu bado ingaki hai na nguvu na makali yake.
NB: Hizi ni hisia zangu baada ya kuunganisha dots kadhaa. Hazina uhusiano na taarifa yoyote rasmi. Unaweza ukawaza tofauti na kuwasilisha au kuchangia kwa namna yako mimi sitakuwa na cha kuongeza wala kupunguza.