Mr. JF
Member
- Dec 14, 2015
- 79
- 107
Power to the People Wanajamvi!!!
Kama umekuwa ukifuatilia mwenendo wa SARAFU yetu pendwa ya TZS kuanzia mwezi wa 5, utagundua kwamba imeporomoka sana kwenye soko la ubadilishaji wa fedha za kigeni.
Kiwango ambacho TZS imeporomoka sasa hivi, hakijawahi kufikiwa tangu uwepo wa TZS duniani, yaani ipo kwenye ukanda wa A.T.H (All the Time High), na wala hakuna anayelizungumzia hili, wala tamko lolote sio waziri sio gavana.
Cha ajabu ukicheck rates za exchange, zilizopo kwenye website ya BOT, utakuta rates za chini kabisa, ila sasa, nenda kafanye transaction ya Dollar Online, au kabadilishe kwenye Bureau De Change, ndio utaona shughuli yake!