Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,151
Lazier lipa bana atujazoea kuringishana huku tunadhulumu watu
ARUSHA: Mfanyabiashara Maarufu wa Madini ya Tanzanite katika Mji wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Saninu Laizer maarufu kwa jina la Bilionea wa Tanzanite amemwangukia Mwekezaji raia wa China, Jun Fang akiomba wakae mezani kutafuta suluhisho ya mgongano wa kimaslahi kati yao.
Bilionea Laizer ameyasema hayo Jijini Arusha baada Fang kutaka kutaka kuomba msaada wa Balozi wa China nchini ili apate haki yake ya fedha na mali vyenye thamani ya Sh bilioni 8.5 ambazo (Laizer) anadaiwa kuonesha dalili za kutaka kumdhurumu.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha Laizer alikiri kuingia ubia na mwekezaji Fang toka mwaka 2011 hadi mwaka 2021 kwa mwekezaji huyo kumiliki hisa asilimia 70 na yeye kama mzawa kumiliki hisa asilimia 30 kwa makubaliano kuwa Fang kuleta vifaa vyote vya kisasa vya uchimbaji,mtaji na kulipa gharama zote za uendeshaji ikiwemo mishahara ya wafanyakazi na alifanya hivyo.
Alisema baada ya mkataba kumalizika mwaka 2021 alimtaka mwekezaji Fang kuingia makubaliano (MOU) ya awali ambayo hakuyataja lakini raia huyo wa China aligoma kusaini makubaliano hayo.
‘’Mimi niko tayari kufanya kazi na Mchina wakati wowote na aje mezani tutatue changamoto zilizopo na tufanye kazi ya uchimbaji madini ya Tanzanite katika kitalu D kama zamani’’alisema Laizer.
Picha na John Mhala
Una maoni usisite kutuandikia
-
#MwangwiwaUkarimu
#echoesofkindness
#HabarileoUPDATES
ARUSHA: Mfanyabiashara Maarufu wa Madini ya Tanzanite katika Mji wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Saninu Laizer maarufu kwa jina la Bilionea wa Tanzanite amemwangukia Mwekezaji raia wa China, Jun Fang akiomba wakae mezani kutafuta suluhisho ya mgongano wa kimaslahi kati yao.
Bilionea Laizer ameyasema hayo Jijini Arusha baada Fang kutaka kutaka kuomba msaada wa Balozi wa China nchini ili apate haki yake ya fedha na mali vyenye thamani ya Sh bilioni 8.5 ambazo (Laizer) anadaiwa kuonesha dalili za kutaka kumdhurumu.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha Laizer alikiri kuingia ubia na mwekezaji Fang toka mwaka 2011 hadi mwaka 2021 kwa mwekezaji huyo kumiliki hisa asilimia 70 na yeye kama mzawa kumiliki hisa asilimia 30 kwa makubaliano kuwa Fang kuleta vifaa vyote vya kisasa vya uchimbaji,mtaji na kulipa gharama zote za uendeshaji ikiwemo mishahara ya wafanyakazi na alifanya hivyo.
Alisema baada ya mkataba kumalizika mwaka 2021 alimtaka mwekezaji Fang kuingia makubaliano (MOU) ya awali ambayo hakuyataja lakini raia huyo wa China aligoma kusaini makubaliano hayo.
‘’Mimi niko tayari kufanya kazi na Mchina wakati wowote na aje mezani tutatue changamoto zilizopo na tufanye kazi ya uchimbaji madini ya Tanzanite katika kitalu D kama zamani’’alisema Laizer.
Picha na John Mhala
Una maoni usisite kutuandikia
-
#MwangwiwaUkarimu
#echoesofkindness
#HabarileoUPDATES