Sanaa ya kifo

Sanaa ya kifo

Mshana Jr KIFO NI SAWA NA KULALA USINGIZI AU? KIFO -USINGIZ USIO NA MWISHO?
Screenshot_20190214_132349.png
 
Ya pili ndio sahihi zaidi... Ndio maana wafu huitwa.... Wale waliolala kuzimu... Pamoja na kwamba kutakuwa na tendo la ufufuo lakini ni ufufuo wa kiroho na si kimwili

Jr
Ahaaaa ukifa roho inaenda kuzimu au inaenda wapi? NI roho zipi zinaenda Pepon? Ufufuo wa roho za waliokufa utakuwa lini?
 
Ahaaaa ukifa roho inaenda kuzimu au inaenda wapi? NI roho zipi zinaenda Pepon? Ufufuo wa roho za waliokufa utakuwa lini?
Dhana ya pepo na kuzimu (akhera) iko pale pale kaburini
Roho zisizotaabika ziko pale pale kaburini (dhana ya pepo)
Roho zinazotangatanga zina taabu nyingi, hazina kikao cha kudumu wala makazi na hukutana na hatari nyingi (dhana ya kuzimu)
Wafu wote wamelala kaburini mpaka siku ya kiama(sijui ni lini)

Jr
 
nimeelewa mkuu Mshana Jr
Akhera ni peponi au kuzimu
Kaburini ni Pepon na kuzimu
Kuzimu ni Chini ya ardhi ni makao makuuu ya roho zinazotangatanga zisizokuwa na makaz maaluum zinazurula,
Pepon roho zisizotaabika zimerest in peace.
Mzimu ni riroho likitoka Kaburini/kuzimu linakuja duniani kuvinjari then linaruruka au?
Swali roho gani zinatangatanga nA zipi zimerest in Peace?
 
nimeelewa mkuu Mshana Jr
Akhera ni peponi au kuzimu
Kaburini ni Pepon na kuzimu
Kuzimu ni Chini ya ardhi ni makao makuuu ya roho zinazotangatanga zisizokuwa na makaz maaluum zinazurula,
Pepon roho zisizotaabika zimerest in peace.
Mzimu ni riroho likitoka Kaburini/kuzimu linakuja duniani kuvinjari then linaruruka au?
Swali roho gani zinatangatanga nA zipi zimerest in Peace?
Ukiwa mwema wakati wa uhai wako hata roho yako italala kwa amani pale mwili ulipo! Ukiwa mtenda dhambini roho yako haitakaa itulie itatangatanga

Jr
 
Kifo kwa tafsiri ya rahisi na iliyozoeleka kwa mwanadamu si neno zuri si neno la kuvutia wala kutajwatajwa hovyo ni neno lililonakshiwa kwa vikolombwezo vyote kwa kutisha na kuogofya sana lakini Kifo ni jambo bora na la bahati nadra kutokea, kifo ni daraja la kuvukia kwenda kwenye hatua nyingine ya maisha ya juu zaidi mepesi zaidi mazuri zaidi! Kifo ni mwendelezo wa uumbaji ni kama tunaposema elimu haina mwisho uumbaji nao hauna mwisho.

Jr
 
Kwahiyo hiyo kwa wale wafu ni kwamba wamekwenda kwenye hatua nyingine ya maisha wameingia kwenye daraja lingine wamefaulu mtihani wa kifo ndio maana wamevuka na kuendelea...kwahiyo kifo ni mafanikio....kwahiyo kama bado unaishi maana yake ni kwamba hujafikia hatua ya kwenda kifoni au umefeli mtihani wake...
Hapa duniani tupo binadamu tunaokadiriwa kufikia bilioni sita wake kwa waume ni katika dakika hizi zenye sekunde sitini masaa 24 siku Saba na miezi 12 watu hufaulu kuingia kwenye daraja lingine la maisha
Kifo ni siri kama ulivyo mtihani ni wale tu wanaofaulu ndio huifahamu siri hiyo...! Tumeshawahi kusikia watu wakisema kuwa Eti fulani kanusurika kifo! Huyu hajanusurika bali kafeli mtihani wa kifo
Siri iliyo wazi ni kwamba kila mwanadamu ana siku saa na dakika yake ya kufanya mtihani wa kifo kufaulu na hatimaye kuendelea mbele

Jr
 
Tunajifunza nini hapa? Hii ndio sanaaa ya kifo huu ndio uhalisia wetu, maisha yetu ni mafupi mno yanapita hima na yamejaa mashaka na hatuna furaha ya kweli tumejawa na stress za kila aina tunatamani kukaa kivulini mahali patulivu penye upepo mwanana, siku zetu za kupumua si lolote bali ubatili mtupu ...Tunalala tukikesha hata alfajiri kunapopambazuka
Sanaa ya ni mtihani usiotabirika, kamwe sisi si wakazi wa hii dunia sisi ni wapitaji kwahiyo tujiandae kama mwanafunzi ajiandaavyo na mitihani ili utakapofika muda wa kuondoka tuondoke kwa amani tukiwaacha wapendwa wetu katika hali njema na bila mitafaruku
Ndugu yetu aliyenukuu hayo maneno ya Biblia takatifu alikufa alikufa kwa kunywa sumu...kabla ya kifo chake alimuaga mkewe vizuri kuwa anaenda kazini (alikuwa meneja wa bar hapa Dar) kule kazini alifanya sherehe ndogo na kuwanunulia wafanyakazi wenzake vinywaji huku akiwaasa kuhusu maisha...alikufa akiwa pekeyake chumbani
Hii ni sanaa ya kifo kamwe haikujulikana kabla..! Wale wafanyakazi wenzake wangekuwepo aliwazalo mwenzao kamwe wasingempa nafasi ya kutekeleza aliwazalo,na pengine wangemlinda na kumsihi a sifanyi hivyo au pengine wengine wangeomba wapige naye picha ya mwisho kama u kumbushio
Cha kushangaza yeye aliweza kujiandaa na kufanya yake aliyoyafanya lakini je ni wangapi ambao waliamua asubuhi wakiwa na mipango lukuki lakini kamwe hawakuweza kufika machweo???
Mitihani ni kwa ajili ya kufaulu! kufeli ni bahati mbaya. ... kwahiyo hata kwa hili tuwe tayari kwa imani zetu tukijua ya kuwa kwa hakika ipo siku saa na dakika tusiyoijua tutatwaliwa kutoka katika maisha haya ila kila mmoja wetu kwa style yake na stahili yake. Bila kujali maumivu yale ya mwisho, mwisho wa yote roho zetu zitaachana na miili yetu nasi tutaitwa marehemu

Jr
 
uhayawani wa kiumbe kiitwacho mwanadamu, mnyama hawezi kufanya haya...nini basi maana halisi ya maisha? Sanaa ya kifo ina mengi ya kutafakari...!kwanini kwenye maisha kuwe na vitu vya kuumiza kiasi hiki ? kwanini mmoja aishi maisha ya raha kuanzia kuzaliwa mpaka kifo wakati mwingine akiishi maisha ya mateso kuanzia kuzaliwa mpaka kifo? ??

Jr
 
HABARI MPYA: Askari Polisi Gideon Clement (30) wa kituo kikuu Cha Polisi Mjini Kahama Mkoa wa Shinyanga amejiua kwa kujipiga risasi asubuhi ya leo wakati akiwa kwenye lindo Benki ya Access tawi la Kahama

Marehemu ameacha ujumbe wa maandishi kwa njia ya simu kwa mke wake akieleza sababu ya kujiua ni kutokana na kukosa mtoto hivyo hajaona sababu ya kuendelea kuishi

Taratibu za mazishi zinaendelea

Habari zaidi...

Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard Abwao amesema sababu za askari huyo kujiua ni kutokana na kutofanikiwa kupata mtoto licha ya kuishi kwenye ndoa na mkewe kwa muda wa miaka mitano.

"Sababu za kujiua kwake ameeleza kwa ujumbe aliotuma kwa mke wake kwamba hana sababu za kuendelea kuishi kwa sababu hajajaliwa kupata mtoto na amekaa kwenye ndoa kwa muda wa miaka mitano na mke wake ambaye ni mwalimu na inasemekana jana alilalamikia sana jambo hilo na alianza kuonesha dalili kwa kumtumia mkewe ujumbe wa simu akieleza kuhusu mali zake vikiwemo viwanja viko wapi",ameeleza Kamanda Abwao.

Kamanda Abwao amesema taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Muleba kwa ajili ya mazishi zinaendelea.

Jr
 
.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom