Samuya na Lissu wote wako gerezani

Samuya na Lissu wote wako gerezani

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
27,640
Reaction score
65,112
Lisu kazuiliwa na gereza na analindwa na askari magereza tu ili asije akachoropoka. Umma na dunia yote wako naye kwa sala na maombi. Tuzo na nyadhifa zinamfuata huko huko gerezani. Kuta za gereza hazimfanyi Lisu kutokuonekana wa hazimnyimi usingizi.

Samuya yuko gereza la kukataliwa na watanzania, analindwa sana ili nafsi yake isije ikachoropoka. Gereza hili halina kuta zinazoshikika, lkn zinampoteza kabisa Samuya kwenye uso wa dunia. Uhuru wake hauoni hata kwenye kuta 4 za chumba chake. Umma wa watanzania na dunia yote unamng'ong'a. Mashitaka na tuzo za uovu zinamfuata chumbani kwake alikofichwa.

Samuya hata akilamba sukari, ulimi wake unampa taarifa kuwa kalamba shubiri. Samuya yuko gereza baya kuliko lile la Lisu.
 
Lile gari lake jipya sidhani kama ana lifurahia. Kwa Sababu anapita nalo mtaani mkuku mbio sana

Hapati hata wasaa wa kuangalia maendeleo aliyo waletea watanzania 😁😁(kama yapo)

Mara ya mwisho kupitia nalo kwa mwendo wa kawaida ilikuwa siku amekula kiapo.

Aaah mama Samia ungesikiliza ushauri kabla ya uchaguzi sasa hivi ungekuwa unaheshimika bila mitutu ya bunduki
 
Kazi ya kuuwa na kupoteza watu, ni kazi ya shetani, na kwa hivyo, mtu akishiriki mauwaji, yeye na shetani ni kitu kimoja, na mwenye kuumba nafsi na roho za watu, naye atawahukumu kwa mauwaji shetani na ndugu zake walioyoyafanya!

CCM na genge lao lote wameshiriki vema kunyima uhai na nafsi za watu
 
Screenshot_20251222-120716~2.png
 
Back
Top Bottom