Samsungs wanashida gani?

Hiyo chai simu utumie internet lazima ichemke Tena ukiongeza na joto la nje kama upo Dar au ukanda wa Pwani betri inaisha haraka haiwezi kukaa masaa 24 labda kama unaiwasha na kuizima na kuiwasha baada ya masaa kadhaa
Labda hiyo unayotumia wewe.
Mimi simu yangu haiwahi kuwa na huo ukanjanja.
 
Hio battery natumia within10hrs naimaliza kabisa ..nyie ni wale mnàsema full data on kumbe mmewasha na hamtumii. Hakuna simu hata hizi zenye 5000mah inaweza kaa 16hrs ikiwa inatumika ..nyie labda hamtumii simu...yangu ina 4000mah mwanzoni íkiwa mpyà ilikuwa inatumia 7% kwa lisaa mtandaoni bila screen kuzima hata kidogo muda wote ni ku scroll tu

2hrs ndo unajikuta imebaki 86% bila screen kuzima .. on WiFi ilikúwa 5% kwa lisaa

Imagine namna inakaa na chaji kwa matumizi heavy screen haizimi ila bàdo unafuta chaji vizuri tu. Kwa ulaji huo means ikiwa imejaa hadi ibaki 10%unatúmia 2hrs sasa how mtu anasema simu imekaa karbu siku mbili kwa data ...hio simu yako inabd ulete uone ñamna inatumika
Rejea niliposema matumizi ya kawaida.
Data ipo on full time
Sichezi game
Zaidi ya kubrowse twitter na jf

Nimezima background data app zisizo muhimu. Background data nimeipa Bluemail na Whatsapp.

Sasa kwa nini simu isikae chaji tu
 
Ipo hivi, kwanza kabisa Hii fact ni maalum tuu kwa flagship(high end) Maana ukiliweka hili katika ujumla wake, hamna anayemkuta Samsung kwa technology ya ku compress battery kubwa mpaka sasa kwa hizi kampuni kubwa zote unazozisikia, hapa nazungumzia Iphone, Oppo, infinix, nokia, tecno, Xiaomi, n.k

Samsung M51 na F62, wote hawa wana 7000mAh(# doesn't lie endurance rating za gsmarena zinaongea, hivyo hawadanganyi), ni mara mbili ya hio uliyotaja, kwenye hizi kampuni kubwa hakuna aliyefikia hapo, wengi wamegota kwenye 6000mAh.

Kwahio unakuja kugundua sio kwamba hawawezi, ila kuna sababu.

1. Sifa ya flagship ili ipendwe inaanzia kwenye muonekano, na huwezi zungumzia muonekano huu bila ku consider unene wa simu, battery kubwa inahitaji space kubwa, na kwa sababu ukubwa wa simu kwa juu(urefu×upana) ni limited kwa size ya kioo unachotaka kutumia, basi sehemu itakayo kua affected ni Unene, matokeo yake ni simu kubwa ambayo ni ngumu ku i manage mkononi.
NOTE : Moja ya sifa ya flagship ni display kubwa, sasa imagine simu kama Note 20 ultra yenye kioo cha inch 7 kasoro nukta halafu iwe nene, utaishikaje?

2. Uzito, ieleweke battery ni hardware, hivyo size inavyokua kubwa uzito unaongezeka, Sasahivi kampuni nyingi za simu zinashindana katika kuhakikisha wanatengeneza simu nyepesi isimkere mtumiaji hata akiweka mfukoni, na tukumbeke ushindani huo ni wa kwenye hizi high end sababu ndio zinaipa kampuni sifa na kutambulisha technologia yao mpya.
Flagship zinatengenezwa na material/hardware bora/imara mfano tempered glass, Aluminium flame n.k, hivi vyote vinaongeza uzito kwenye simu, while low end wanatumia ma plasti kote,
Hivyo basi kuachana tuu na battery simu inakua nzito tayari, sasa ukibugi kwenye battery unashangaa unatengeneza simu ya nusu kilo na ushee, sitanii (ulefone power Armor 13, ina nusu kilo), sasa hii uite flagship? Angalia Samsung S21 ultra mwenye 5000mAh pamoja na battery ndogo kulinganisha na M51 lakini material yake mazito yameifanya imzidi Uzito M51 yenye 7000mAh iliyotengenezwa kwa plastic, haya angeongezewa na hizo 2000mAh ingekuaje? Na ukija upande wa pili huyu M51 amemzidi S21 ultra unene tena kwa mbali tuu(ana 9.5mm, bado 0.5mm tuu agonge 1cm), sababu ni nini? Utagundua ni battery, kitu ambacho Samsung hawezi kubali kwenye flagship zake.

3.Space, Ieleweke ukisikia simu ina kitu hiki na hiki cha ziada, jamani hivi vitu vinaanzia kwenye hardware, hivyo vinahitaji space kuvi accommodate, flagship hua inaongezewa features mfano heart rate sensor, wireless charging, camera bora, speaker bora, au hio note 10 uliyoitaja, inahitaji space zaidi kwa ajili ya ku accommodate ile S-pen, ambayo kimahesabu hio pen tuu imechukua sehemu ya 900mAh, umeona sasa? n.k n.k, hivi vitu vyote vinahitaji space, hivyo kufanya eneo la battery kua finyu..

4. Businesses strategies, battery ni hitaji kubwa sana kwenye simuu, kuna watu hilo tuu ndilo kipaumbele chake kikubwa kwenye simu, hivyo atatafuta lets Say M31s sababu ya battery then ametosheka, Mwingne anahitaji vyote, atanunua flagship kupata features bora, halafu atachukua yenye battery kubwa itakayomsaidia kwenye bussy days, hiki ni kitu cha kawaida, sema tuu wengine pengine kutokana na hali za kiuchumi hio option inaangukia kwenye viswaswadu.
Mfano binafsi nina Samsung kubwa, halafu nina kijisamsung Duos cha Batani kwa ajili ya backup, tayari mpaka hapo ni deal kwa kampuni.

5. Upgrade, Kila Mwaka Kampuni zinatoa flagship mpya yenye features mpya za kuvutia, binadamu hata kama alichonacho kinamtosha, ila ana shauku ya kupata kikubwa zaidi kadiri ya mda. Hivyo hata kama wana uwezo wa kuweka 7000mAh leo hii, hataweka ila ataanzia kwenye 3500mAh ili mwakani akiweka 4000mAh bado uone kuna improvements, mfano note 10 plus ana 4100mAh na note 20 ultra ana 4500mAh, tayari kuna watu wanashawishika kununua note 20 ultra kwa sababu hio,
Sasa mtu alinunua S21 ultra kwa sababu ya battery ya 5000mAh, leo hii ukamletea s22 ultra ina 5000mAh tena atanunua ya nini?..

Mtazamo wangu,
Nunua Simu ambayo utaitumia bila kua na mawazo ya kuangalua battery percentage, Simu ambayo Bila kuzima Data basi inakufikisha mda wako wa kulala huku ikiwa imebaki na charge incase ya dharura ya umeme, binafsi sikumbuki ni lini nilizima data kwenye simu yangu, naperuzi kokote na kwa kujiyosheleza ila jioni nachezea 50%-40%, Sikumbuki ni lini niliwasha simu yangu, mana sijawa na sababu ya kuizima na haijawahi zima sababu ya charge.

Moja ya stress ambazo ni kero kwenye simu basi ni charge, simu ni yako lakini unaitumia kwa kuichungulia,

Sitaki kuzungumizia wale rafiki zangu wa,
please wait.....
Unfortunately Jamiiforums has stoped...
Camera is not responding.......
Twitter has crashed......
Naweza nisababishe watu wagombane na keyboard huko.
Mkuu reyzzap umefafanua kwa weredi mkubwa kabisa. Ni kweli katika flagship kampuni haiwezi ku-compromise na design ya simu for the sake of battery. Kwa kuwa nakuona una uelewa wa simu naomba unisaidie kujua, Je Galaxy A22 inakaa na charge muda gani? Ninataka ku-upgrade kutoka kwenye hizi Tecno and co. Je camera yake ina kiwango kizuri? Binafsi nimeridhika na sAmoled tech, 90 hz refresh rate, OIS tech na miaka 2 ya software updates ila bado sijainunua kwa sababu sina uhakika na battery pamoja na camera yake.
 
Habari za muda huu sons and beautiful daughters of men.

Ninyoke kwenye mada. Hivi hawa samsung wameshindwa kabisa kutengeneza batteries au vip yaani simu kama note 10 ina 3500mah s10 3400mah ? Simu hizi na nyinginezo ni nzuri lakini kwenye batteries capacity ni shida.

Wenda kuna sababu siijui ebu karibuni kwa michango na mitazamo yenu
Me natumia vivo v21 na ina battery 4000 mAh na inakaa na chaji siku nzima ...
 
Mkuu reyzzap umefafanua kwa weredi mkubwa kabisa. Ni kweli katika flagship kampuni haiwezi ku-compromise na design ya simu for the sake of battery. Kwa kuwa nakuona una uelewa wa simu naomba unisaidie kujua, Je Galaxy A22 inakaa na charge muda gani? Ninataka ku-upgrade kutoka kwenye hizi Tecno and co. Je camera yake ina kiwango kizuri? Binafsi nimeridhika na sAmoled tech, 90 hz refresh rate, OIS tech na miaka 2 ya software updates ila bado sijainunua kwa sababu sina uhakika na battery pamoja na camera yake.
Daa hii simu nimeiachia last week, Camera ni nzuri, battery ni uhakika siku nzima Data ON na unalala na charge, Display nzuri, kwa ufupi niliridhka nayo karibuni kwenye kila kitu, ukinunua wahi kuweka hizi Silicone cover zenye kama wax kwa chini mana inakwaruzika kirahisi.

Kati ya simu ambazo sikushauri uziwaze ni A21s, A12, A11, bora hata A10s ina camera na display nzuri practically, hizi A-series nimecheza nazo sana
 
Daa hii simu nimeiachia last week, Camera ni nzuri, battery ni uhakika siku nzima Data ON na unalala na charge, Display nzuri, kwa ufupi niliridhka nayo karibuni kwenye kila kitu, ukinunua wahi kuweka hizi Silicone cover zenye kama wax kwa chini mana inakwaruzika kirahisi.

Kati ya simu ambazo sikushauri uziwaze ni A21s, A12, A11, bora hata A10s ina camera na display nzuri practically, hizi A-series nimecheza nazo sana
Asante sana kwa ufafanuzi huo. Nimetatanika sana kati ya simu tatu za A22, Redmi note 10S na realme 8 kwa sababu they are around the same price range lakini sikuwahi kupata mtu ambaye ametumia simu hizi hasa kwa mazingira ya hapa nilipo.Lakini sasa nimehakikishiwa.
 
Balaa tupu

Mwaka juzi simu hii hii yenye 4000mah..kuna game laitwa maleo tunacheza online hadi umalize ñi kama 20-25min muda huo wote inatumia 4% ..hivo hadi nimalize 20% ni kama game tano online ..kabla ya hapo nilikuwa nacheza na simu moja ukicheza round mbili ya tatu lazima ukae kwenye chaji ndo úcheze

Haya kuna mtu ana smart 5 kachaji j3 leo anakwambia ina 73% muda huu wakati simu hio hio nilitumia siku mbili mfululizo kila siku namaliza chaji ila mwenye nayo leo siku ya tatu ina 73%
Hilo game la maleo limenifanya mpaka nimeuza galaxy S7 edge sababu ya chaji kuisha haraka nikicheza masaa mawili mfululizo simu inazima chaji alafu inakua ya moto balaa sasa nimekamata galaxy A12 sasa nacheza mpaka hamu inaisha na bado nakuwa nimebakiwa na% nyingi tu za matumizi mengine
IMG-20220304-WA0001.jpg


Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app
 
Daa hii simu nimeiachia last week, Camera ni nzuri, battery ni uhakika siku nzima Data ON na unalala na charge, Display nzuri, kwa ufupi niliridhka nayo karibuni kwenye kila kitu, ukinunua wahi kuweka hizi Silicone cover zenye kama wax kwa chini mana inakwaruzika kirahisi.

Kati ya simu ambazo sikushauri uziwaze ni A21s, A12, A11, bora hata A10s ina camera na display nzuri practically, hizi A-series nimecheza nazo sana
Kaka sasa unafeli yani A10s ubora wake ni upi mpaka iishinde A12 au A12 body design yake ilivyo kaa vibaya ndio unaiona ni simu ya hovyo mpaka ukaishusha kwa A10s angalia specification mwenyewe kisha ujisahihishe

Galaxy A10s

Display 6.2 PLS IPS
720×1520 pixels

13 mp
1080p

2/3 RAM
helio p22

4000 mAh

Storage 32gb



Galaxy A12

Display 6.5 PLS IPS
720×1600

48MP
1080p

4/6 RAM
helio p35

5000 mAh

Storage 32/64/128

Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app
 
H
Siwezi tumia simu ambayo si flagship and current ndo tatizo. Nimeshazoea premium features so mi ni mwenzo wa Samsung S series au Iphone tena current versions.
hivi kwa iphone 11pro max na xs max ukaaji wa chaji maana naona watu wanaipondea sana.
 
Daa hii simu nimeiachia last week, Camera ni nzuri, battery ni uhakika siku nzima Data ON na unalala na charge, Display nzuri, kwa ufupi niliridhka nayo karibuni kwenye kila kitu, ukinunua wahi kuweka hizi Silicone cover zenye kama wax kwa chini mana inakwaruzika kirahisi.

Kati ya simu ambazo sikushauri uziwaze ni A21s, A12, A11, bora hata A10s ina camera na display nzuri practically, hizi A-series nimecheza nazo sana
mi naulizia kati ya iphone 11 pro max/ xs max na oneplus 9RT 5G.

Na kwa hapa bongo kuna sehemu duka la 1+ wenye unboxing phone
 
Hii samsungs sijui ni kampuni gani!

Nakushauri hachana na makumpuni feki ya kichina kama Samsungs, Dunia tunafahamu Samsung tu.
 
Hilo game la maleo limenifanya mpaka nimeuza galaxy S7 edge sababu ya chaji kuisha haraka nikicheza masaa mawili mfululizo simu inazima chaji alafu inakua ya moto balaa sasa nimekamata galaxy A12 sasa nacheza mpaka hamu inaisha na bado nakuwa nimebakiwa na% nyingi tu za matumizi mengineView attachment 2138170

Sent from my SM-A127F using JamiiForums mobile app
Hivi simu gani ipo vizuri hapo?? Kuna ka itel kamoja kalikuwa balaa,, hakawezi kukutoa mchezoni ..labda istuck ila utacheza hadi uleave room mwenyewe,, nikaja jarbu na samsung moja unashangaa imerudi home yenyewe...
 
Habari waungwana ,asee nna Samsung A22 ambayo ni mpya ,,ila inatatizo la kutoweza kukubali line ya halotel ,line zingine zinasoma ,,line ha halotel inasoma ilaninaweka ''emergency calls only"
Screenshot_20220320-233051.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom